Entertainment
Justin Bierber Arejea na Album Mpya ‘SWAGG’

Msanii nyota wa muziki wa kimataifa, Justin Bieber, hatimaye ameachia rasmi albamu yake mpya na ya saba kwa jina “Swag”, ikiwa ni albamu yake ya kwanza tangu mwaka 2021 alipotoa Justice. Albamu hii imetoka leo na tayari imeanza kutikisa majukwaa mbalimbali ya muziki duniani.
Swag imejumuisha mastaa kadhaa akiwemo Gunna, Sexyy Red, Cash Cobain, pamoja na wasanii wengine wa kizazi kipya.
Albamu hiyo ina jumla ya nyimbo 20 na tayari baadhi ya vibao kama “Go Baby”, “Soulful” na Butterflies “zimeanza kupokelewa vizuri kwenye mitandao ya Spotify, Apple Music na YouTube.
Hii ni mara ya kwanza kwa Bieber kuachia albamu tangu alipopata matatizo ya kiafya mwaka 2022 yaliyosababisha asitishe ziara yake ya kimataifa ya Justice World Tour ambayo ilikuwa iendelee hadi mwaka 2023.
Ziara hiyo ilisitishwa mnamo Septemba 2022 baada ya Bieber kupatwa na maradhi ya Ramsay Hunt Syndrome, ugonjwa uliomsababishia kupooza upande mmoja wa uso.
Kwa kipindi cha miaka minne bila kazi mpya, mashabiki wa Justin Bieber duniani wamekuwa wakimsubiria kwa hamu ujio wa kazi mpya kutoka kwake. Kupitia Swag, msanii huyo ameonyesha kurejea kwa nguvu na ubunifu wa hali ya juu, huku akiwa katika hali nzuri kiafya na kisaikolojia.
Taarifa na Francos Mzungu
Entertainment
Chris Brown Akanusha Shtaka la Kumshambulia Producer kwa Chupa

Msanii nyota wa Marekani, Chris Brown, amekana mashtaka mawili mahakamani yanayohusiana na madai ya shambulio kwa kutumia chupa katika kilabu cha usiku jijini London miaka miwili iliyopita.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 anatuhumiwa kumsababishia mtayarishaji wa muziki majeraha ya mwili katika tukio ambalo waendesha mashtaka wamelieleza kuwa “halikuwa na uchochezi wowote”.
Pia anakabiliwa na shtaka la kumiliki silaha hatari — ambayo ni chupa ya kileo.
Mashtaka haya mawili yaliongezwa mwezi uliopita kwenye shtaka la awali, kubwa zaidi, la kujaribu kumsababishia mtu majeraha mabaya ya mwili (GBH), ambalo tayari Bwana Brown alilishatupilia mbali kwa kujitetea kuwa si kweli.
Chris Brown anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kesi hiyo mwezi Oktoba mwaka 2026.
Waendesha mashtaka wamesema kuwa mhanga wa tukio hilo, Abraham Diaw, alikuwa amesimama kwenye baa ya kilabu cha usiku kilichopo eneo la Soho mnamo tarehe 19 Februari 2023, wakati Chris Brown alimpiga kwa chupa mara kadhaa.
Mwimbaji huyo alikamatwa mwezi Mei katika hoteli ya nyota tano iliyopo Salford, Greater Manchester, baada ya kurejea Uingereza kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya muziki barani Ulaya.
Alizuiliwa korokoroni kwa takriban wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa dhamana baada ya kukubali kulipa ada ya dhamana ya pauni milioni tano (£5m) kwa mahakama.
Ada ya dhamana ni kiasi cha fedha kinachowekwa kama dhamana ya kifedha kuhakikisha mtuhumiwa atarudi mahakamani kwa kesi yake. Brown anaweza kupoteza fedha hizo endapo atakiuka masharti ya dhamana, ambayo yaliendelezwa katika kikao cha mahakama siku ya Ijumaa.
Kwa mujibu wa masharti hayo, Chris Brown anatakiwa kuishi katika anwani iliyopo Uingereza akisubiri kesi hiyo, na aliamriwa kukabidhi pasipoti yake kwa polisi.
Hata hivyo, ameruhusiwa kuendelea na ratiba ya ziara yake ya kimataifa ya Breezy Bowl XX kwa masharti kwamba atakabidhi pasipoti kila anapomaliza safari, na kuirudishiwa anapohitaji kusafiri kwa ajili ya maonesho.
Katika wiki za hivi karibuni, Brown amekuwa akitumbuiza kwenye viwanja na kumbi mbalimbali za burudani kote Uingereza na Ulaya, na kumaliza burudani mjini Paris mwishoni mwa wiki iliyopita. Sehemu ya ziara hiyo inayofanyika Marekani Kaskazini inatarajiwa kuanza baadaye mwezi huu na kufikia tamati tarehe 18 Oktoba.
Kikao kingine cha mahakama kimepangwa kufanyika tarehe 24 Oktoba.
Chris Brown ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa zaidi wa R&B nchini Marekani, akiwa mshindi wa tuzo mbili za Grammy na nyimbo 19 zilizofika katika nafasi 10 za juu kwenye chati za Uingereza, zikiwemo Turn Up The Music, Freaky Friday, With You na Don’t Wake Me Up.
Mshitakiwa mwenza, Omololu Akinlolu, raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 anayefahamika kisanii kama HoodyBaby, naye pia alikana shtaka la kumsababishia mtu majeraha ya mwili. Awali, alikana pia shtaka la kujaribu kusababisha majeraha mabaya ya mwili.
Chanzo: BBC
Entertainment
Sean “Diddy” Combs Atahukumiwa Katika Kesi Itakayosikilizwa Oktoba 3

Wiki iliyopita, Combs alipatikana na hatia kwa makosa mawili ya usafirishaji kwenda kufanya ukahaba baada ya kesi ya wiki nane. Anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka kumi jela kwa kila kesi, ingawa wachambuzi wa sheria wanatabiri kuwa atapata kidogo zaidi.
Aliondolewa mashtaka mazito zaidi ambayo alishutumiwa kula njama ya ulaghai na biashara ya ngono.
Baada ya uamuzi huo kutangazwa Jumatano iliyopita ya tarehe 2/7/2025, Jaji Arun Subramanian alipendekeza kuratibiwa kusikilizwa kwa hukumu hiyo Oktoba 3, lakini aliambiwa na mawakili wa Combs kwamba wanatarajia kuharakisha mchakato huo wa hukumu.
Awali mawakili wa Combs walipendekeza tarehe 22 Septemba kwa ajili ya kusikilizwa kwa hukumu, lakini baadaye walirekebisha pendekezo lao hadi Oktoba 3 katika barua iliyofuata kwa hakimu muda mfupi baadaye.
Barua ya kwanza ilisema pendekezo la utetezi lilikuwa chini ya idhini kutoka kwa ofisi ya uangalizi. Barua ya pili, ambayo kimsingi iliunga mkono msukumo wao wa kuharakisha hukumu yake, ilirejesha kikao cha hukumu hadi tarehe yake ya awali na kusema ofisi ya uangalizi haikupinga ratiba hiyo.
Mawakili na Combs walipiga simu iliyodumu chini ya dakika moja baada ya naibu wa Subramanian kuwaambia mawakili kwamba hakimu atawajibu kuhusu tarehe yao iliyopendekezwa.
Waendesha mashtaka walikuwa walimshtaki Combs kwa kuongoza biashara ya uhalifu ambapo alidaiwa kutumia vitisho, vurugu, kazi ya kulazimisha, hongo na uhalifu mwingine kuwashurutisha rafiki zake wa kike wa zamani Cassie Ventura na mwanamke ambaye alitoa ushahidi kwa jina bandia la Jane kujihusisha na maonyesho ya ngono yaliyochochewa na wasindikizaji wa kiume wanaoitwa “Freak Offs”
Combs alikana mashtaka hayo huku mawakili wake walidai kuwa kile kinachojulikana kama “Freak Offs” kilikubaliwa kutokana na uhusiano wake wa muda mrefu na Ventura na Jane.
Combs pia anakabiliwa na mashtaka kadhaa ya kiraia, ambayo alikanusha makosa yote.
Mkali huyo wa muziki amekuwa kizuizini katika gereza la shirikisho la Metropolitan Detention Center huko Brooklyn tangu alipokamatwa mwezi Septemba 2024.
Taarifa na Francos Mzungu