Connect with us

International News

Israel na Iran zakubaliana kusitisha mashambulizi

Published

on

Go back

Your message has been sent

Warning
Warning
Warning
Warning

Warning.

Makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Iran yameanza kutekelezwa huku nchi hizo mbili zikithibitisha tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu hatua hiyo.

Muda mfupi baada ya tangazo la Trump, taifa la Israel lilisema limeafikia malengo yake na ikathibitisha kwamba imesitisha mashambulizi, hatua iliyotafsiriwa kama mwisho wa vita vya siku 12 kati ya Israel na Iran.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya nje wa Iran, Abbas Araghchi, ilikanusha kuwepo kwa makubaliano yoyote ya kusitisha mashambulizi, akisema kwamba Iran haina nia ya kuendeleza mashambulizi, lakini bado haijakubali rasmi kusitisha mapigano.

Licha ya kauli za kusitishwa kwa mashambulizi ya makombora kati ya nchi hizo mbili, Jeshi la Ulinzi la Israel limeripoti mashambulizi mapya yaliyotokea kutoka upande wa Iran.

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz alisema Iran ilikiuka usitishaji wa mapigano kwa kurusha makombora, akisema huenda jeshi la Israel likaanza tena kuishambulia Iran.

Iran ilikanusha habari kwamba imefanya mashambulizi ya makombora kuelekea Israel baada ya nchi hizo mbili kukubali kusitisha mapigano.

Mataifa mbalimbali ulimwenguni yamepongeza hatua ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Iran, huku taifa la China likizitaka nchini hizo mbili kutafuta suluhisho la kisiasa kwa mzozo kati yao.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni

Published

on

By

Mahakama kuu nchini Tanzania imemrejesha kwenye debe mgombea urais wa chama cha upinzani ACT wazalendo, Luhaga Mpina na kupindua maamuzi yaliyotolewa na tume ya uchaguzi nchini humo INEC.

Hii inamaana tume ya INEC ni lazima imjumuishe Mpina katika orodha ya majina ya watakaopigiwa kura, hatua itakayosababisha upinzani kwenye uchaguzi huo mkuu.

Hatua hii sasa inampa Mpina fursa ya kuanzisha kampeni za kutaka kumbandua mamlakani rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 29 mwaka 2025.

Kampeni za uchaguzi tayari zinaendelea nchini humo.

INEC ilimzuia mpina kugombe wadhifa wa urais mwezi Agosti 26, 2025 ikidai chama cha ACT Wazalendo kilikiuka taratibu za chama kwa kumsimamisha Mpina kuwania wadhifa huo.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa katika kampeni za uchaguzi mkuu.

Katika uamuzi uliotolewa Alhamisi  mwezi Septemba 11, 2025, jopo la majaji watatu mjini Dodoma liliagiza INEC kumuidhinisha Mpina kama mgombea wa urais.

Anatarajiwa kujumuika na wagombea wengine 16 kutoka vyama vidogo vya kisiasa katika mapambano hayo ya kuwania urais, ambao wote wanania ya kung’atua rais wa sasa Samia Suluhu Hassan mamlakani.

Chama cha Chadema kilizuiwa kugombea katika uchaguzi huo baada ya kiongozi wake Tundu Lissu kufunguliwa mashtaka ya uhaini.

Kiongozi wa upinzani wa Chadema Tundu Lissu akiwa mahakamani.

Rais Samia Suluhu Hassan alichukua hatamu za uongozi kama rais baada ya kifo cha John Pombe Magufuli mwaka 2021.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

International News

Ghasia zatanda nchini Nepal licha ya marufuku ya kutotoka nje.

Published

on

By

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea kukiukwa nchini Nepal ambako ghasia za uharibifu wa mali na umwagikaji wa damu zinaendelea.

Serikali ya Waziri mkuu KP Sharma Oli, ilipinduliwa ndani ya masaa 48 baada ya kuzuka kwa maandamano hayo, ambapo waandamanaji waliokuwa na ghadhabu walivamia na kuteketeza makaazi ya Waziri mkuu Oli, pamoja na bunge la nchi hiyo.

Licha ya jeshi la nchi hiyo kutanganza hali ya tahadhari na marufuku ya kutotoka nje, Waandamanaji hao waliendelea kukiuka marufuku hiyo na kumiminika katika barabara za mji mkuu wa Kathmandu, huku wakiwashambulia maafisa wa usalama, lakini pia kulenga makaazi ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Wabunge na mawaziri huku wakiteketeza majumba na magari yao.

Kulingana na taarifa za maafisa wa usalama nchini humo, waandamanaji hao pia walivamia magereza na kuwaachilia huru jumla ya wafungwa elfu 13 katika kipindi cha wiki nzima ya maandamano.

Chanzo cha maandamano hayo yaliyoanzishwa na kizazi cha sasa cha Gen Z mapema wiki hii ni kukithiri kwa ufisadi serikalini mbali na sera duni zinazolenga kukandamiza vijana katika matumizi ya mitandao ya jamii.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

Trending