Connect with us

News

IPOA: Watu 20 walifariki katika vituo vya polisi mwaka huu

Published

on

Mamlaka ya kuchunguza utendakazi wa maafisa wa polisi nchini IPOA, imetoa tahadhari kwa taifa kutokana na ongezeko la vifo vya wakenya vinavyotokea katika vituo vya maafisa wa Polisi nchini.

Katika ripoti iliyotolewa na IPOA, takriban watu 20 wamefariki wakiwa chini ya ulinzi wa maafisa wa polisi katika kipindi cha miezi minne pekee iliyopita.

Mwenyekiti wa IPOA Issack Hassan, amesema Mamlaka ya IPOA haijawakamata washukiwa wa visa hivyo kutokana na mamlaka hiyo kutokuwa na uwezo, akisema washukiwa wote wanaohusishwa na kesi hizo wanachukuliwa kama wahalifu.

“Tumenakili visa visivyopungua 20 katika kipindi cha miezi minne pekee kwamba watu hawa walipoteza maisha yao ndani ya seli zetu na kunaendelea na uchunguzi, kesi hizo zitafikishwa kwa Ofisi ya ODDP na wahusika watafunguliwa mashtaka”, alisema Hassan.

Hassan amesema kufikia sasa maafisa wa polisi 17 wamehojiwa kuhusiana na matukio hayo ikiwemo wale waliomkamata Albert Ojwang pamoja na mashahidi 6, akisema haki kwa familia za wale waliopoteza wapendwa wao itapatikana.

Mwenyekiti huyo wa IPOA, ameyasema hayo alipofika mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu usalama, akisema Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Eliud Lagat pia atafika mbele ya Mamlaka ya IPOA kuandikisha taarifa kuhusu kifo cha Ojwang.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Familia ya jamaa aliyezama baharini inalilia haki

Published

on

By

Familia ya Mwanamme aliyezama baharini katika kaunti ya Kilifi siku kadhaa zilizopita, inahimiza serikali kuongeza juhudi na kuwapa msaada wa kumtafuta jamaa wao.

Ikiongozwa na Omar Ali Omar ambaye ni Kakake Marehemu, Familia hiyo ilisema wamekuwa na wakati mgumu wa kuelekea baharini kila siku kwani kufikia sasa ni siku ya nne tangu jamaa wao azame baharini.

Aidha aliitaka serikali ya kaunti kutoa taarifa sehemu mbalimbali zinazopakana na ufuo wa bahari kwani huenda mwili wa Marehemu ukasukumwa na mawimbi hadi ufuoni. 

Familia ya jamaa aliyezama maji inalilia haki

Omar aliitaka idara ya kukabiliana na majanga katika kaunti kushirikiana na wavuvi wengine eneo la Mnarani pamoja na kutuma maboti zaidi kwa ajili ya uokozi wa mwili wa jamaa huyo kwani wamelazimika kugharamikia mafuta ya boti za ziada.

“Rescu timu ni boti moja, hiyo pekee yake kutafuta mtu kwa bahari ni vigumu vyombo vinatakikana vitoke vingi,washirikiene na sisi familia tuwekuongeza vyombo vya baharini kutafuta jamaa wetu, kwa sasa tunagharimika sasa boti kwenda baharini asubuhi na jioni inatugharimu shilingi elfu 16 kwa siku”, alisema Omar.

Kauli ya Omar imeungwa mkono na Mamake Marehemu ambaye ameshinikiza serikali ya kaunti kuingilia kati na kuhakikisha mwili wa mwanawe unapatikana.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Nassir: Kaunti ya Mombasa wametenga milioni 80 za Afya

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Mombasa, Abdulswamad Shariff Nassir amesema serikali ya kaunti ya Mombasa wametenga shilingi milioni 80 kugharamia sehemu ya matibabu ya wakaazi ambao hutibiwa katika hospitali za Level 4 na Level 5.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa, Nassir alisema fedha hizo zitagharamia bima ya afya ya SHA ya wenyeji wa kaunti hiyo kwa muda wa mwaka mmoja.

Gavana Nassir pia alisema fedha hizo zitagharamia madeni ya ziada ya matibabu kwa watoto wa chini ya umri wa miaka 5 ambao wanatibiwa kupitia bima hiyo ya SHA.

“Tumeweka dawati maalum na fedha kuweza kuwalipia ile amana ambayo ilikuwa inalipiwa SHA. Na itakuwa sio ya Public health pekee lakini kando na Public health mnakuwa mumelipiwa kwa mwaka mzima’’, alisema gavana Nassir

Wakati huo huo Gavana Nassir alieleza matumaini kwamba mpango huo utasaidia kwa asilimia kubwa kuimarisha huduma za matibabu kwa wenyeji wa kaunti hiyo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending