News
IPOA: Watu 20 walifariki katika vituo vya polisi mwaka huu

Mamlaka ya kuchunguza utendakazi wa maafisa wa polisi nchini IPOA, imetoa tahadhari kwa taifa kutokana na ongezeko la vifo vya wakenya vinavyotokea katika vituo vya maafisa wa Polisi nchini.
Katika ripoti iliyotolewa na IPOA, takriban watu 20 wamefariki wakiwa chini ya ulinzi wa maafisa wa polisi katika kipindi cha miezi minne pekee iliyopita.
Mwenyekiti wa IPOA Issack Hassan, amesema Mamlaka ya IPOA haijawakamata washukiwa wa visa hivyo kutokana na mamlaka hiyo kutokuwa na uwezo, akisema washukiwa wote wanaohusishwa na kesi hizo wanachukuliwa kama wahalifu.
“Tumenakili visa visivyopungua 20 katika kipindi cha miezi minne pekee kwamba watu hawa walipoteza maisha yao ndani ya seli zetu na kunaendelea na uchunguzi, kesi hizo zitafikishwa kwa Ofisi ya ODDP na wahusika watafunguliwa mashtaka”, alisema Hassan.
Hassan amesema kufikia sasa maafisa wa polisi 17 wamehojiwa kuhusiana na matukio hayo ikiwemo wale waliomkamata Albert Ojwang pamoja na mashahidi 6, akisema haki kwa familia za wale waliopoteza wapendwa wao itapatikana.
Mwenyekiti huyo wa IPOA, ameyasema hayo alipofika mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu usalama, akisema Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Eliud Lagat pia atafika mbele ya Mamlaka ya IPOA kuandikisha taarifa kuhusu kifo cha Ojwang.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.
Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.
Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.
“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi
Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.
Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.
Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.
Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.
Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.
Taarifa ya Joseph Jira