Connect with us

News

IEBC yasistiza usalama kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu

Published

on

Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, Erastus Ethekon, amesisitiza umuhimu wa usalama katika maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2027.

Akizungumza kwenye mkutano wa ushirikiano na vitengo vya usalama kutoka kaunti za Mombasa, Kwale na Kilifi, Ethekon alisema tume ya IEBC imeendelea kushirikiana kwa karibu na vitengo hivyo tangu mwaka 2013, kuhakikisha chaguzi zinakuwa za amani, haki na uwazi.

Hata hivyo Ethekon alikiri kuwepo kwa changamoto kama vile uhaba wa fedha, vitisho vipya vya kiusalama, ukiukaji wa haki za binadamu, pamoja na ghasia za kijinsia dhidi ya wanawake na wasichana wakati wa chaguzi.

Mwenyekiti huyo vile vile alisema usalama wa uchaguzi si wa siku ya kupiga kura pekee, bali ni mchakato unaopaswa kuzingatiwa kuanzia usajili wa wapiga kura hadi kutangazwa kwa matokeo.

Kwa upande wake, kamishna wa IEBC Anne Nderitu alisema tume ya IEBC imeweka mikakati kuhakikisha chaguzi ndogo zipatazo 24, zinafanyika kwa uwazi na kwa kuzingatia sheria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kenya kuzindua utalii wa anga (Astro-tourisim)

Published

on

By

Kenya itakuwa mwenyeji wa uzinduzi wa utalii wa anga(Astro-tourisim) katika kaunti ya Samburi Septemba 7, 2025, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha na kubadilisha aina za utalii nchini.

Uzinduzi huo unaendana sambamba na tukio la mwezi kupatwa maarufu kama Blood moon ambapo litaanza saa mbili na nusu usiku wa septemba 7, 2025, na kudumu kwa dakika 82.

Mpango huu wa kipekee unalenga kuifanya Kenya kuwa kivutio kikuu cha wapenzi wa sayansi ya anga na wasafiri wa kimataifa wanaopenda maajabu ya siri.

Kwa mujibu wa  shirika la Magical Kenya, tajriba hii ya anga inalenga kutumia mazingira ya kipekee ya nchi kufungua ukurasa mpya na endelevu wa utalii.

Waziri wa utalii na wanyama pori Rebecca Miano atakuwa mgeni rasmi akiandamana na wageni wa kimataifa katika hafla hiyo itakayofanyika katika Sopa Lodge kwenye hifadhi ya kitaifa ya Samburu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Serikali kukabiliana na magenge ya uhalifu nchini

Published

on

By

Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen ameonya kuhusu kuongezeka kwa magenge ya wahalifu nchini.

Akizungumza katika kongamano la Jukwaa la Usalama kaunti ya Vihiga, Waziri Murkomen alitoa wito kwa inspekta jenerali wa polisi kutuma vikosi zaidi vya dharura eneo hilo ili kuwasambaratisha wahalifu hao.

Magenge ya wahalifi yamekuwa yakiripotiwa kuhangaisha usalama na maisha ya wakaazi katika sehemu mbali mbali nchini ikiwepo kaunti za hapa Pwani.

Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro aliahidi kushirikiana kwa karibu na maafisa wa usalama kukomesha magenge ya wahalifu yanayowahangaisha wakaazi maarufu mawoza.

Akizungumza mjini Malindi katika kaunti ya Kilifi kwenye mkutano na vijana wa eneo hilo, gavana Mung’aro alisema serikali yake haitawavumilia vijana waliopotoka kimaadili wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Wakati huohuo aliwaonya baadhi ya maafisa wa kaunti wanaowahangaisha wakaazi hususan wahudumu wa bodaboda.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending