News
Idara ya Usalama Yalaumiwa kwa Kukosa Kuhamia Mfumo wa Kidijitali

Idara ya Usalama nchini imelaumiwa kwa kushindwa kuzihamisha huduma zake hadi katika mfumo wa kidijitali hali ambayo imerudisha nyuma juhudi za kutafuta usaidizi wa kiusalama.
Kulingana na Wanaharakati wa kijamii, licha ya taifa kupiga hatua katika kuhakikisha haki inapatikana kwa washukiwa na wale wanaofika Mahakamani bado idara hiyo imesalia nyuma kiteknolojia.
Wanaharakati hao wakiongozwa na Victor Kaudo, wamelaumu mfumo wa zamani unaotumika na maafisa wa usalama katika kunakili na kuweka rekodi za kesi mbalimbali zinazowasilishwa katika vituo vya polisi, wakidai kwamba mfumo huo unachelewesha kesi Mahakamani.
“The next Place ambayo tunahitaji zaidi iende digital ni National Police service ili zile faili pale ziwe zinafanywa haraka haraka ndio tukienda pale katika Gender base tuache kuwa frastrated and alot of paper work. Wakifanya kazi zote kuwa katika mtandao tutakuwa tunafanya kazi zetu kwa urahisi”, alisema Kaudo.
Hata hivyo mwaka wa 2019, Idara ya usalama nchini ilianzisha mchakato wa kuweka rekodi za kesi wanazopokea katika mfumo wa kidijitali lakini mpango huo ilikosa kufaulu na kuwarejesha katika mfumo wa zamani wa kutumia vitabu kunakili kesi.
News
Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.
Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.
Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.
Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.
Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.
Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.
Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.
Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.
Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Taarifa ya Joseph Jira