Connect with us

News

Hofu ya Ongezeko la HIV

Published

on

Shirika la umoja wa mataifa la kupambana na virusi vya UKIMWI, UNAIDS, limesema huenda kukawa na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi milioni 6 na vifo milioni 4 vinavyohusiana na ukimwi kufikia mwaka 2029.

Hii ni kutokana na kupunguzwa kwa fedha za misaada ya kiafya kutoka Shirika la Marekani, USAIDS.

Kulingana na takwimu, taifa la Afrika kusini ndio taifa lenye idadi kubwa zaidi ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ulimwenguni lakini pia nchi inayoongoza katika utafiti wa virusi vya ukimwi ulimwenguni.

Miongoni mwa mataifa mengine, Afrika kusini pia imekuwa nchi ambayo pia ilikuwa ni mpokeaji mkubwa wa fedha za UKIMWI kutoka Marekani hadi Machi mwaka huu, wakati utawala wa Rais Trump ulipotangaza kufungwa kwa Shirika la USAID.

Mwezi uliopita vyuo vikuu vya juu vya Afrika Kusini viliomba serikali madola ya mamilioni ili kuendelea na utafiti huu ambao baadhi umesitishwa kwa sababu ya kupunguzwa kwa fedha na Marekani.

Pesa hii ilisaidia nchi hiyo kupunguza kiwango chake cha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi kwa zaidi ya asilimia 60 tangu kilele chake mnamo 2000.

Siku ya Jumatano tarehe 9 Julai 2025, serikali ya Afrika Kusini na wafadhili wa kimataifa waliahidi karibu dola milioni 54 ili kukabili palipo na mapungufu.

Mwaka jana Marekani ilitumia mara nane ya kiwango hicho kwa ufadhili wa Virusi Vya Ukimwi Afrika Kusini kiwango hiki hakitatosha kutimiza hitaji lililopo.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending