Sports
Harambee Stars Yavuna Ushindi Dhidi Ya Chad

Timu ya taifa ya soka Harambee Stars imevuna ushindi wa kwanza chini ya kocha Benni McCarthy baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Chad Ugani Stade De Marrekesh Morocco.
Mshambulizi wa kilabu ya Talanta fc Emmanuel Osoro aliwatanguliza vijana wa nyumbani dakika ya 18 kabila ya mshmabulizi wa Bandari Fc David Sakwa kufunga goli la pili dakika ya 45.
Hata hivyo Chad inayoshikilia nafasi ya 177 kote ulimwenguni ilerejea kwa kishindo kipindi cha pili wakijipatia goli la kufutia machozi dakika ya 60.
Kocha wa Stars anamini angali anajenga kikosi ambacho kitakua bora zaidi katika miaka za mbeleni huku akiahidi vijana wa nyumbani wataleta furaha kwa Wakenya.
“Ushindi ni Muhimu lakini bado najitahidi kuwajua vijana wangu kwa muda mrefu mashabiki wawe na utulivu kwani Stars itafurahisha hivi karibuni.”
Hii ilikua ni ushindi wa kwanza kwa kocha huyo tangu achukuwe mikoba kutoka kwa kocha mkuu Engine Firat alionyeshwa mlango kutokana na msururu wa matokeo duni.
Sports
Florian Wirtz Sasa Mambo Nywee! Kutua Liverpool

Kilabu ya Liverpool imeafikia makubaliano na Bayern Leverkusen kuhusiana na usajili wa kiungo mbunifu Florian Wirtz uhamisho ambao ni rekodi mpya wa uhamisho Uingereza.
Timu hizo mbili zimekua kwenye mazungumzo na sasa kitita cha pauni milioni 116 imeafikiwa kwa tineja huyo mwenye umri wa miaka 22.
Raia huyo Ujerumani sasa atawasili Liverpool kwa ajili ya vipimo vya kimatibabu wiki ijayo na baadaye kutiwa wino kandarasi mpya
Inaaminika Wirtz atamwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Reds na kuwa sajili wa pili kwa kocha Arne Slot baada ya kupata sahihi ya beki Jeremie Frimpong wa taifa la Uholanzi kwa pauni milioni 29.5.
Sports
Thomas Frank Kocha Mpya Spurs

Kilabu ya Tottenham HotSpurs ya Uingereza imemtambulisha Thomas Frank kuwa kocha mpya kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu mwezi jana licha kushinda kombe la Europa ligi na kilabu hiyo wakishinda Manchester United goli 1-0.
Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 51 amemwaga wino kwenye karatasi mktaba wa miaka mitatu na kilabu hiyo ya London Kaskazini huku kibarua cha kwanza ni kutoa kilabu hiyo kutoka nafasi ya 17 Epl na kurejesha katika ubora wake.
Raia huyo wa Denmark amekua na kilabu ya Brenford kwa miaka saba na aliwasaidia The bees kumaliza ya kumi msimu jana na alama 56 ligi ya Epl na amekua akiwindwa ni vilabu kadha wa kadha.