Connect with us

Sports

Harambee Stars Yavuna Ushindi Dhidi Ya Chad

Published

on

Timu ya taifa ya soka Harambee Stars imevuna ushindi wa kwanza chini ya kocha Benni McCarthy baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Chad Ugani Stade De Marrekesh Morocco.

Mshambulizi wa kilabu ya Talanta fc Emmanuel Osoro aliwatanguliza vijana wa nyumbani dakika ya 18 kabila ya mshmabulizi wa Bandari Fc David Sakwa kufunga goli la pili dakika ya 45.

Hata hivyo Chad inayoshikilia nafasi ya 177 kote ulimwenguni ilerejea kwa kishindo kipindi cha pili wakijipatia goli la kufutia machozi dakika ya 60.

Kocha wa Stars anamini angali anajenga kikosi ambacho kitakua bora zaidi katika miaka za mbeleni huku akiahidi vijana wa nyumbani wataleta furaha kwa Wakenya.

“Ushindi ni Muhimu lakini bado najitahidi kuwajua vijana wangu kwa muda mrefu mashabiki wawe na utulivu kwani Stars itafurahisha hivi karibuni.”

Hii ilikua ni ushindi wa kwanza kwa kocha huyo tangu achukuwe mikoba kutoka kwa kocha mkuu Engine Firat alionyeshwa mlango kutokana na msururu wa matokeo duni.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending