Connect with us

Sports

Harambee Stars Yajiondoa CECAFA

Published

on

Timu ya taifa ya soka ya Kenya, Harambee Stars, imejiondoa rasmi katika michuano ya CECAFA inayojumuisha mataifa manne: Tanzania, Kenya, Uganda na Senegal, ambayo yalipangwa kufanyika Karatu, Arusha, nchini Tanzania.
Uamuzi huo umetolewa na kocha mkuu wa Harambee Stars, Benni McCarthy, kwa kushirikiana na kamati ya kiufundi, wakieleza wasiwasi wao kuhusu ubora wa viwanja vya mazoezi pamoja na uwanja wa kuandalia mechi hizo.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza rasmi leo, ambapo Harambee Stars ilikuwa imepangiwa kufungua pazia kwa kuvaana na wenyeji, Taifa Stars ya Tanzania.
Shirikisho la Soka nchini Kenya (FKF), kupitia barua rasmi kwa vyombo vya habari, limethibitisha taarifa hizo.
Michuano hiyo ilikuwa sehemu ya maandalizi ya timu shiriki kuelekea mashindano ya CHAN, ambayo yanatarajiwa kuanza rasmi katika kipindi cha siku 12 zijazo.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Morocco Kukosa Nyota Wanne Kombe La CHAN

Published

on

By

12 DAYS TO GO CHAN-Siku 12 zikiwa zimesalia kungoa nanga taji la CHAN Tumulike Mabingwa mara 2 wa kombe hilo Morocco.

Morocco-Wanajiita The Atlas Lions kwa jina la Utani
Wameshiriki kombe la CHAN mara 4 (2014, 2016, 2018, 2020)
Kocha mkuu ni :Tarik Sektioui ambaye amewahi kuwa mchezaji wa timu ya Taifa hilo na kwa sasa ananoa kikosi cha wachezaji wasiozidi umri wa miaka 23.

Taifa hilo pamoja na DR.Congo watakua wanalenga kuingia kwenye daftari za Kumbukumbu kwa kuwa taifa la kwanza kushinda taji hilo mara tatu,Morocco wakiwa wameshinda mara 2 mwaka 2018 na 2020.

Baadhi ya wachezaji wakuangaziwa kwenye kikosi cha timu hiyo ni pamoja na nyota Bouchaïb Arrasi wa kilabu ya Raja Casablanca pamoja na Younes El Kaabi wa Racing Casablanca.

Mwalimu huyo hata hivyo atakosa wachezaji wanne ambao wote wamepata vilabu vya nje,wachezaji hao ni pamoja na;Amin Zahzouh, Akram Al-Naqqash, Hatem Al-Sawabi, and Adel Tahaif.
The Atlas Lions wako Kundi A pamoja na Kenya,Angola,Zambia na DR.Congo.

Continue Reading

Sports

Mshambulizi Wa Nigeria Victor Osimhen Asajiliwa Na Galatasaray

Published

on

By

Mabingwa wa Ligi Kuu Uturuki, Galatasaray wamekamilisha usajili wa mshambuliaji, Victor Osimhen, 26, raia wa Nigeria kwa ada ya uhamisho ya jumla ya Euro milioni 75 zitakazolipwa kwa awamu akitokea Napoli Napoli.

Osimhen ambaye msimu uliopita alikuwa Galatasaray kwa mkopo akitokea Napoli sasa anarejea jumla klabuni kwa mkataba wa miaka mitatu utakaombakisha klabuni hapo mpaka Juni 2028.
Kwenye mkataba huo Napoli imeiwekea Galatasaray sharti la kutomuuza nyota huyo kwenda klabu yoyote ya Serie A kwa kipindi cha miaka miwili vinginevyo itakumbaka adhabu ya malipo ya ziada.
#Kpenga
Continue Reading

Trending