Connect with us

Sports

Gwiji wa Tae-kwon-do Master Kihurani Asherekewa

Published

on

Gwiji wa mchezo wa tae-kwon-do mwanadada Caroline Wairimu Kihurani ambaye aliaga dunia wiki jana jijini Nairobi anazidi kusherehekewa na wengi kutokana na mchango wake mkubwa katika mchezo huo nchini baada ya kukuza vipaji vingi.

Mchezaji huyo aliingia kwenye daftari za kumbukumbu kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuwakilisha Kenya katika mashindano ya dunia ya mchezo huo mwaka 1997 makala ya World Taekwondo Championships mjini Hong Kong Uchina.

Katika ibada ya wafu iliofanyika hapo jana wengi hawakusita kumiminia sifa kedekede mwendazake ambaye aliaga dunia na miaka 57 wakimtaja alikua shujaa kwenye mchezo huo.

Kulingana na Rais wa KTF Major Suleiman Sumba amesema kwamba gwiji huyo hatakumbukwa tu kwa kipaji chake bali pia kwa mchango wake kuwapa msukumo mtoto wa kike.

“Coach Carol kama alivyofahamika hatakumbukwa tu kwa ubora wake uwanjani na kipaji aliyokua nayo kwenye mchezo huu bali pia nyoyo za watoto wengi wa kike ambazo aliwapa nafasi kushiriki mchezo wa tae-kwon-do.

Mwendazake atapumzisha katika makao yake ya milele kule Ol-Joro-Orok siku ya Alhamisi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Liverpool Yakubaliana Dili Ya Kerkez

Published

on

By

Kilabu ya Liverpool imekubaliana na AFC Bournemouth kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 4o kwa beki Milos Kerkez raia wa Serbia.

Tineja huyo anatarajiwa kuwasili Liverpool muda wowote kufanyiwa vipimo vya kimatibabu na kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa ligi kuu Uingereza.

Mchezaji huyo alikua nguzo muhimu kwa kilabu ya Bournemouth wakimaliza kumi bora akichangia magoli matano na kufunga mawili,anakua sajili wa tatu kwa kocha Arne Slot kwenye kilabu hio.

The Reds wakiwa wametumia pauni milioni 116 kumpata kiungo Florian Wirtz,pauni milioni 31 kupata Jeremie Frimpong.

Continue Reading

Sports

Starlets Kucheza Fainali Ya CECAFA Dhidi Tanzania

Published

on

By

Kikosi cha soka akina dada kushuka dimbani kucheza dhidi ya Twiga Stars Ya Tanzania kwenye fainali ya kipute cha CECAFA Afrika Mashariki ugani Azam Sports Complex.

Vipusa wa kocha Beldine Odemba wameshinda mechi zote tatu ikiwemo kuwalaza Sudan Kusini magoli 4-0 mechi ya siku ya Alhamisi huku wakiwa wamekusanya alama 9 sawa na wenyeji Tanzania kwenye mashindano ya mwaka huu.

kwa mujibu wa mwalimu huyo wanatarajia mechi ngumu dhidi ya wapinzani wao kwani wako nyumbani na timu bora pia.

“Tuko tayari kwa mechi ya mwisho ambayo pia ni fainali kila mmoja anajua tumekua vizuri katika mashindano haya ila Tanzania ni mpinzani mkubwa katika fainali ya leo kwa sababu pia hawajapoteza mechi kama sisi.”

Mechi hiyo inangoa nanga saa 12.00 jioni.

Continue Reading

Trending