Connect with us

Sports

Gilbert Lewa Silipwi Ubuntu Fc.

Published

on

Mkufunzi wa kilabu ya Ubuntu Fc ambaye pia ni mkufunzi wa shule ya Upili ya Majaoni Gilbert Lewa amefichua kwamba halipwi na kilabu yake na kwamba anafanya tu kazi ya kujitolea.

Akizungumza na Kipenga Cha Coco FM mwalimu huyo anasema licha ufanisi ambao wamekua nayo changamoto ni mengi mno kwenye kilabu hiyo.

“Ubuntu silipwi najitolea tu ila ndiyo kilabu imenipa ufanisi na watu kunijua kwa hivyo siwezi nikasema chochote kibaya kwani Ubuntu ni sehemu yangu”.

Hata Hivyo Lewa amesema kwamba Shule Ya Upili Ya Majaoni inamlipa vizuri ndiyo maana akachukua changamoto hiyo mpya akifichua inathiri matokeo ya vijana wake wa Ubuntu Ligi ya Divisheni ya pili kwani hajaenda mazoezini kwa wiki mbili kunoa kilabu yake.

“Majaoni walinitafuta na tukakubaliana na mpaka sasa wananilipa vizuri na tena kwa muda ufao ,Niko na Muda sasa sijaenda kunoa timu ya Ubuntu nilimwachia mwenzangu naambiwa badhi ya wachezaji wanasusia mazoezi kwa sababu mimi ndiyo niliwaleta wanataka kuniona pale uwanjani.”

Ubuntu Fc inaketi nafasi ya sita na alama 33Ligi ya FKF Divisheni ya pili baada ya kutoka sare ya 1-1 na Malindi United.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending