News
Gachagua, amkosoa Rais Ruto kwa madai ya uongozi duni

Viongozi wa upinzani nchini wakiongozwa na Kinara wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua waliendeleza kampeni za Wantam dhidi ya rais William Ruto wakielenga uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.
Wakazingumza wakati wa ziara yao ya kisiasa katika eneo la Pwani, Kalonzo alimkosoa rais Ruto akisema ameshindwa kuongoza taifa hali na kuendelea kuwanyanyasa vijana wa Gen Z kwa kuwateka nyara kiholela.
Kalonzo hata hivyo alidai kwamba serikali ya Kenya kwanza ina malengo fiche dhidi ya Bandari ya Mombasa, akisema kama wapinzani watahakikisha serikali ya rais Ruto ina hudumu kwa muhula moja pekee.
“Rais Ruto alishindwa kuongoza nchi na kuendelea kuwanyanyasa wakenya hasa vijana wa Gen Z kwani tumeshuhudia utekaji nyara wa kiholela na hata bandari ya Mombasa wako na malengo fiche na hiyo”, alisema Kalonzo.
Kwa upande wake aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na ambaye pia ni Kinara wa Chama cha DCP, amemkosoa rais Ruto na Katibu wa Muungano wa vyama vya wafanyikazi nchini COTU Francis Atwoli kwa kuwahadawa wakenya na kusambaratisha uchumi wa nchi pamoja na kufuja fedha za hazina ya NSSF huku Atwoli akilinyamazia suala hilo.
“Pesa ya NSSF imechukuliwa na Rais Ruto na kuendelea kujenga barabara na Bomas hiyo ni kinyume na sheria na hatutakubali na yule kiongozi wa kutetea wafanyikazi Atwoli amenyamaza ama wamekula hiyo pesa pamoja”, alisema Gachagua.
Upinzani waendeleza kampeni za Wantam
Hata hivyo viongozi walioandamana na Kalonzo katika ziara hiyo ya kisiasa eneo la Pwani wakiongozwa na Mgombea wa kiti cha ubunge wa eneo bunge la Magarini Furaha Chengo Ngumbao, walisema serikali imesheheni wizi wa mashamba ya wakaazi wa Pwani na kudia kwamba mamlaka yote yako nchini ya wananchi.
Wengine walioandamana na Kalonzo ni pamoja na Naibu Kinara wa DCP Cleophas Malala, Mbunge wa Wundanyi Danson Mwashako, Seneta wa Kisii Richard Onyonka miongoni mwa viongozi wengine.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.
Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.
Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.
“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi
Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.
Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.
Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.
Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.
Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.
Taarifa ya Joseph Jira