Connect with us

News

Fikirini: Ni sharti vijana wapewe nafasi na fursa za kiuchumi

Published

on

Katibu katika Wizara ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs amesema juma la vijana limebuniwa ili kutoa nafasi zaidi kwa vijana wengi kuwasilisha matakwa yao kwa idara husika kinyume na kusherehekea siku moja tu ya kimataifa ya vijana.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kukamilika kwa uzinduzi wa maadhimisho ya juma la vijana katika chuo kikuu cha Pwani, Fikirini alisema kuwa siku moja haitoshi kwa vijana wote nchini kupata fursa ya kuwasilisha hoja zao kwa viongozi.

“Katika juma hili la vijana Wizara ya vijana na uchumi bunifu itazuru maeneo mengine ya taifa huku kilele cha sherehe za siku ya vijana ulimwenguni ambayo itakuwa tarehe 12 zikitarajiwa kuadhimishwa katika chuo kikuu cha Masinde Muliro”, alisema Fikirini.

Fikirini alikariri kuwa vijana wengi wana matakwa mengi ya kuyawasilisha hivyo wanapaswa kutengenezewa majukwaa mbalimbali ya kutoa maoni yao.

Aidha Fikirini aliwashauri vijana kutumia mitandao kama chombo cha kujiimarisha kiuchumi badala ya kuitumia kwa maswala yasiofaa.

Ni hafla ambayo iliongozwa na Naibu rais Prof. Kithure Kindiki, Waziri wa Michezo nchini Salim Mvurya, mbunge wa Kilifi kaskazini, Owen Baya, Mwakilishi wa kike kaunti ya Kilifi Getrude Mbeyu, Mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa miongoni mwa viongozi wengine.

Mamia ya vijana kutoka kaunti ya Kilifi walijumuika kwenye uzinduzi wa maadhimisho hayo sawa na baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Pwani.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Published

on

By

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.

Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.

Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.

Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.

Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.

Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending