News
Fikirini, Ameapishwa Rasmi kuwa Katibu katika Wizara ya Michezo na Vijana

Rais William Ruto ameshuhudia kuapishwa kwa mawaziri wawili wapya pamoja na makatibu katika Wizara mbalimbali nchini katika halfa iliyoandaliwa katika Ikulu ya Nairobi.
Wakati wa halfa hiyo, mawaziri na makatibu hao wameapa kuwajibikia majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia kanuni za nchi sawa na kuheshimu muongozo wa Katiba.
Geoffrey Ruku aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Utumishi wa umma nchini pamoja na Hanna Cheptumo kama Waziri wa jinsia wameapishwa rasmi kuanza majukumu yao ya kikazi.
Wengine walioapishwa ni makatibu katika Wizara mbalimbali baada ya kuidhinishwa na bunge la kitaifa ambapo Fikirini Jacobs kama Katibu katika Wizara ya Michezo na vijana, Caren Achieng Ageng’o, Aden Abdi Mila miongoni wa wengine wameahidi kutumikia taifa kikamilifu.
Akizungumza baada ya kuapishwa kwa mawaziri na makatibu hao, Rais William Ruto amewashauri mawaziri na makatibu hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kikamalifu ili kufanikisha malengo ya wananchi.
News
Mpango wa kuboresha afya ya macho kuanzishwa kaunti ya Mombasa

Serikali ya Kaunti ya Mombasa kwa ushirikiano na shirika la Christian Blind Mission (CBM) imeanzisha rasmi mpango mpya wa kuboresha afya ya macho kwa wakaazi wa kaunti hiyo.
Kupitia mradi unaojulikana kama Vision Impact, shirika hilo linalenga kupunguza matatizo ya uhafifu wa macho kuona, na upofu unaoweza kuzuilika, kwa kuimarisha huduma za afya na kuongeza uhamasishaji katika jamii.
Mradi huo umefadhiliwa na unatekelezwa katika kaunti saba nchini, huku Mombasa ikiwa miongoni mwao, ukilenga kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu kwa kutambua kuwa ulemavu mara nyingi ni chanzo na pia matokeo ya umasikini.
Mradi huo utajumuisha hamasa kwa jamii na wahudumu wa afya, uchunguzi wa macho shuleni na kwa njia ya kuzuru nyumba hadi nyumba, huku wagonjwa watakaobainika kuwa na matatizo ya kuona wakipewa rufaa kwa matibabu yanayostahili.
Serikali ya Kaunti ya Mombasa iliesema kuwa hiyo ni hatua muhimu katika kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya ya macho na bila ubaguzi.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Viongozi wa jamii ya Mijikenda wakosoa maandazili ya sherehe za Chenda chenda.

Baadhi ya viongozi wa jamii ya mijikenda eneo la pwani wamekosoa mpangilio wa sherehe za kitamaduni za jamii ya kimijikenda maarufu chenda chenda zilizofanyika jana Kaunti za Kilifi na Kwale.
Wakiongozwa na mwenyekiti ya baraza la jamii ya Chonyi Raphael Mwangala walisema msingi wa maandalizi ya sherehe hizo ni mshikamano ya jamii ya Mijikenda na wala sio mgawanyiko kama ilivyoshuhudiwa hapo jana.
Mwangala alisema taswira iliyojitokeza hapo jana hairidhishi kwa wamijikenda na inaonyesha hawana msimamo.
“Walioanzisha hii chenda chenda si lengo la kugawanyana, ni lengo la kuja pamoja, wengine wanachukua tu ni chenda chenda mijikenda waje wakae tu, lakini leo yule anaenda fanya Kwale, yule anaenda fanya wapi, hilo sio lengo, ningewasihi Mijikenda wenzangu, ngewasihi hata viongozi ambao wanajiita ni viongozi wa chenda chenda wafikirie lazima twende pamoja zi mambo ya kugawanyana”, alisema Mwangala.
Anadai sherehe hizo zimeingiliwa kisiasa akisistiza umuhimu wa kubuniwa kamati mpya ya jamii hiyo itakayohusisha mwakilishi wa kila kabila.
“Kwanza kamati ni wakina nani? Ni lazima kamati iuende mpya ya chenda chenda kwa kila mmijikenda awe mule ndani ya kamati ili wakipanga wawe wanaenda pamoja”, aliuliza Mwangala.
Baadhi ya watumbuizaji wa ngoma za kiasili katika sherehe za chenda chenda mjini Kilifi.
Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro Mung’aro aliahidi kuunda kamati maalum itakayohusisha wazee wa Kaya ili kuangazia ulinzi wa misitu ya Kaya.
Akizungumza wakati wa sherehe hizo katika chuo kikuu cha Pwani, Gavana Mung’aro alisema kamati hiyo itahakikisha misitu ya kaya inazunghushiwa uwa ili kudhibiti uvamizi wa binadam.
Kauli ya gavana huyo ilijiri baada ya wazee wa Kaya kulalama kuwa misitu ya Kaya imekuwa ikisambaratika kutokana na uvamizi na kutatiza shughuli za mwendelezo wa mila na tamaduni za wamijikenda.
“Nitaunda kamati ya wazee wa Kaya tuangazia maneno ya misitu na mashamba ili kuwekewa ua ili itunzwe dhidi ya wavamizi,tunatengeneza kitengo cha vijana watyakaokuwa walinzi wa msitu kwa sababu tuiko na wizara hiyo ndani ya kaunti”, alisema Mung’aro
Kwa upande wake katibu katika wizara ya vijana na uchumi bunifu Fikirini Jacobs amesistiza jamii ya mijikenda hasa vijana kuzingatia umuhimu majukumu ya uongozi waliyonayo katika jamii.
Sherehe hizo ambazo ni makala ya nane kufanyika, ilifaa kufanyika kaunti ya Kwale kulingana na mpangilio wa awali wa kufanyika kile eneo la pwani japo kulifanyika mabadiliko siku za mwisho.
Mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa na gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani kwenye sherehe za Chenda chenda Kwale
Hatua hiyo ilikashifiwa na baadhi ya viongozi ambapo maandalizi mengine yalifanyika katika msitu wa Kaya Mtswakara kaunti ya Kwale ambapo mwenyekiti ya bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa alihudhuria.
Taarifa ya Joseph Jira