Connect with us

News

Fikirini, Ameapishwa Rasmi kuwa Katibu katika Wizara ya Michezo na Vijana

Published

on

Rais William Ruto ameshuhudia kuapishwa kwa mawaziri wawili wapya pamoja na makatibu katika Wizara mbalimbali nchini katika halfa iliyoandaliwa katika Ikulu ya Nairobi.

Wakati wa halfa hiyo, mawaziri na makatibu hao wameapa kuwajibikia majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia kanuni za nchi sawa na kuheshimu muongozo wa Katiba.

Geoffrey Ruku aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Utumishi wa umma nchini pamoja na Hanna Cheptumo kama Waziri wa jinsia wameapishwa rasmi kuanza majukumu yao ya kikazi.

Wengine walioapishwa ni makatibu katika Wizara mbalimbali baada ya kuidhinishwa na bunge la kitaifa ambapo Fikirini Jacobs kama Katibu katika Wizara ya Michezo na vijana, Caren Achieng Ageng’o, Aden Abdi Mila miongoni wa wengine wameahidi kutumikia taifa kikamilifu.

Akizungumza baada ya kuapishwa kwa mawaziri na makatibu hao, Rais William Ruto amewashauri mawaziri na makatibu hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kikamalifu ili kufanikisha malengo ya wananchi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Serikali na Wadau wa mazingira wapanda miti, Sabaki

Published

on

By

Serikali ya kitaifa kwa ushirikiano na mashirika ya kimazingira kaunti ya Kilifi inaendeleza mpango wa upanzi wa miti ili kuboresha mazingira.

Kulingana na Katibu wa masuala ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs, mpango huo unalenga kurudisha hadhi ya taifa la Kenya katika viwango vya kimazingira.

Akihutubia Wananchi wakati wa zoezi la upanzi wa mikoko katika eneo la Sabaki kaunti ya Kilifi, Fikirini alibainisha kwamba kupitia zoezi hilo jumla ya Miche elfu mbili ya mikoko kutoka kwa serikali na mashirika ya uhifadhi wa Mazingira imepandwa katika eneo hilo.

“Tumepanga miti mingi sana, idara yetu ya vijana imetoa miche elfu na kupitia mashirika mengi hapa wametoa miche elfu kwa jumla tumepanda miti elfu mbili, asante sana kwani kwa kufanya hivyo unasaidia pakubwa”, alisema Fikirini.

Wakati huo huo ameihimiza wananchi kuzingatia suala la upanzi wa miti pamoja na kujiepusha na ukataji miti kiholela, akisisitiza haja ya wakaazi kulinda misitu ili kuiwezesha jamii kuwa mazingira bora.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Kindiki, ataka makubaliano kati ya serikali kuu na kaunti kutekelezwa

Published

on

By

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki ametaka makubaliano yote kati ya serikali za kaunti na ile ya kitaifa kutekelezwa kabla ya mwezi Disemba mwaka huu wa 2025.

Akizungumza katika makao yake ya Karen jijini Nairobi Jumatatu 23, Juni 2025, kwenye mkutano wa 27 kati ya serikali kuu na zile za kaunti kuhusu bajeti IBEC, Kindiki alisema kumekuwa na makubaliano ambayo yamekuwa hayafuatiliwi ili kutekelezwa.

Kindiki alisema serikali kuu imejitolea kuhakikisha serikali za kaunti zinafanikisha miradi mbalimbali na kuwataka maafisa wa serikali za kaunti na ile ya kitaifa kushirikiana kwa majadiliano.

Wakati huo huo alisisitiza haja ya kutafuta suluhu la matatizo yanayoathiri utendakazi wa serikali za kaunti huku akipuzilia mbali uwepo wa mzozo wowote baina ya serikali kuu na zile za kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi.

Continue Reading

Trending