Connect with us

News

Biwot: Familia zilizoathirika na ujenzi wa barabara ya Kilifi-Mtwapa zafidiwa

Published

on

Idara ya usalama kaunti ya Kilifi imesema serikali inaendelea na zoezi la kufidia familia zilizoathirika na ujenzi wa barabara kuu ya Kilifi kuelekea Mtwapa.

Kamisha wa kaunti ya Kilifi Josephat Biwot alidokeza kuwa kwa sasa maafisa wa shirika la Kenya power wanaendelea kuondoa nyaya za stima ili kutoa nafasi kwa mkandarasi kuendelea na shughuli za ujenzi.

Vile vile Biwot alisema ujenzi daraja mbili kubwa kaunti ya Kilifi unaendelea pamoja na ujenzi wa barabara ya Sabaki Sosoni kueleke Baricho hadi Baolala.

“Ujenzi wa barabara kuu ya Kilifi kuelekea Mtwapa unaendelea vyema, tunachokifanya sasa ni kufidia walioathirika, pia kenya power inaondoa nyaya kupisha mwanakandarasi kuendelea na ujenzi, vile vile ujenzi wa daraja mbili kuu kilifi unaendelea hasa ya Galana Kulalu na Baricho”, alisema Biwot.

Vile vile Kamishna huyo alidokeza kuwa serikali inaendelea na ujenzi wa miradi mbali mbali inayoambatanishwa na sekta ya uchumi wa bahari.

“Upande wa uchumi wa bahari miradi mingi inaendelea mfano ujenzi wa eneo la kuegesha boti kilifi, pia tunajenga makao makuu ya eneo la samaki ya kaunti, tuko na soko la samaki Malindi, tuko na eneo la kuhifadhi samaki la kichwa cha kati ambalo limekamilika na liligharimu shilingi milioni 250”, aliongeza Biwot.

Wakati huo huo wadau wa sekta ya Uvuvi eneo la Ngomeni wakiongozwa na Mwenyekiti wa Ngomeni BMU Said Athman aliitaka serikali kufuatilia kwa kina fedha zinazotolewa na serikali kudaidi miradi ya wavuvi.

“Tunapewa pesa ya makundi kwa mfano shilingi milioni tatu, ile pesa mpaka ikifikia jamii imeliwa, kwa mfano unapewa boti lakini halina vifaa sababu ile pesa imeliwa juu na maofisa mpaka ikifika nyanjani imeisha”, alisema Athman.

Mwenyekiti wa Ngomeni BMU Said Athman akizungumza na wanahabari Kilifi.

Taarifa ya Joseph Jira.

 

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Published

on

By

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.

“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

KHRC: Wasichana elfu moja ni wajawazito, Lamu

Published

on

By

Takribani wasichana elfu moja kaunti ya Lamu wameripotiwa kupata mimba za utotoni kati ya mwaka wa 2024/25 huku visa vingi vikichangiwa na dhulma za kingono na ndoa za mapema.

Kulingana na Masharika ya kutetea haki za kibinadamu la MUHURI pamoja na lile la Kenya Human Rights Commission, KHRC serikali imeshindwa kuwakabili kisheria wahusika huku waathiriwa ambao ni wasichana wadogo wakiendelea kuhangaika.

Takwimu kutoka kwa kamati ya jinsia kaunti ya Lamu, iliwasilisha kwa kamati ya kitaifa inayoangazia masuala ya dhulma za jinsia kuwa kaunti hiyo ilinakili visa zaidi ya 700 vya mimba za utotoni mwaka wa 2024.

Takwimu hioz pia ziliweka wazi kwamba visa vingine zaidi ya 200 viliripotiwa kati ya mwezi Januari na Mei mwaka huu wa 2025.

Kulingana na ripoti kutoka kwa baraza la kitaifa la kudhibiti magonjwa NSDCC ilieonysha kwamba wasichana wanarika zaidi ya 600 nchini walipata mimba mwaka 2023.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending