Connect with us

Entertainment

Huku ama Kule! Bavyombo Azua Gumzo Mitandaoni Kisa Siasa za 2027 Kilifi

Published

on

Fadhili Bavyombo, msanii maarufu wa muziki wa bango kutoka Pwani ya Kenya, amezua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kuchapisha ujumbe tata wa kisiasa kwenye ukurasa wake wa Facebook. Ujumbe huo uliowalenga wanasiasa wakuu wa Kaunti ya Kilifi umevutia maelfu ya mashabiki na kuchochea maoni mbalimbali kuhusu uchaguzi wa Gavana wa Kilifi mwaka 2027.

Katika chapisho hilo, Bavyombo aliandika:

“Wananichanganya 😅 Sijui huku ama kule… Hebu leo nambieni… Ninacho kiskia huku ndicho ninacho kiskia kule…”

Ujumbe huu uliambatana na picha za Gideon Mung’aro (Gavana wa sasa wa Kilifi) na Aisha Jumwa (aliyekuwa Mbunge wa Malindi, sasa akilenga kiti cha ugavana 2027). Kwa kutumia majina ya mafumbo, aliwataja kama Huku na Kule – jambo lililozua utani, hisia kali na mijadala ya kisiasa

Chapisho hilo liliambatana na picha za wanasiasa wawili wa kaunti Kilifi – Gideon Mung’aro (Gavana wa sasa) na Aisha Jumwa (aliyewahi kuwa Mbunge wa Malindi na sasa akimezea mate kiti cha ugavana 2027). Katika lugha ya mafumbo, Mung’aro aliitwa HUKU, na Jumwa KULE – jambo lililowapa mashabiki wake nafasi ya kuchangia kwa hisia kali na zenye utani mwingi.

Chapisho hilo limepokelewa kwa mitazamo tofauti, huku baadhi ya mashabiki wakitoa maoni ya kuunga mkono, ya kuchekesha na ya kisiasa:

  • Mwangiri Ndoro: “Mng’aro hata 20 ana deserve. Jumwa ni mama mzuri lakini ana majivuno.”

  • Ben Bello: “Siasa ni maslahi tu mkuu!”

  • Simon Gambo: “Pale unafaidika tu bro, siyo hisia.”

  • Masika Mcute: “Tuko huku sisi. Kule kwa matanga hatuwezi!”

  • Senior Mwayele: “Fata kazi yako ya usanii. Huyawezi!”

Wengine walienda mbali zaidi kwa kukosoa wagombea moja kwa moja:

  • 🏚️ Davis Mwalimu: “Jumwa aolewe kwanza. Nyumba ilimshinda ataweza Kilifi?”

Wasanii na Siasa: Nafasi ya Bavyombo Katika Mjadala wa Umma

Ujumbe wa Bavyombo unadhihirisha kuwa wasanii wana ushawishi mkubwa katika kuanzisha mijadala kuhusu uongozi. Wengine wamepongeza ujasiri wake huku baadhi wakihimiza abakie kwenye kazi ya muziki.

Kwa kutumia tu swali rahisi – “Huku ama Kule?” – Bavyombo amehamasisha mijadala kuhusu mustakabali wa Kilifi, mwaka 2027.

🤔 Je, Wewe Upo Huku au Kule ama Hauko Popote?

Nambie kwenye maoni: Ni nani anayefaa kuliongoza jimbo la Kilifi mwaka 2027? Na je, unaona wasanii kama Bavyombo wakipaswa kushiriki katika mijadala ya kisiasa?

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Joy to The World! Mke wa Michael Yena, Grace Santa, Ajifungua

Mwimbaji wa Injili Michael Yena na mkewe Grace Santa wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza. Jua zaidi kuhusu ujio huu wa neema na wimbo mpya ‘Ametutendea’ unaosindikiza tukio hilo la kipekee!

Published

on

Ni shangwe! Ni nderemo! Ni vigelegele! Baraka kubwa imetua rasmi kwenye familia changa ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Michael Yena, baada ya mkewe kipenzi Grace Santa kujifungua mtoto wao wa kwanza! 🍼👶

Kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, Yena alipakia picha na tulipomtafuta mda mchache uliopita akathibitisha habari hiyo njema.

Kwenye Facebook, Yena, aliandika:

“We give God all the Glory. #Ametutendea”

Lakini subiri kidogo! Ikiwa unataka kujua mtoto ni wa kike au wa kiume… tafadhali kaa mkao wa kusubiri 😅. Kulotia maongezi ya njia ya simu, Yena amesema, kwa sasa jinsia ya mtoto itabaki kuwa “fiche”, wakisubiri wakati maalum wa kufanya tangazo rasmi. Hii ni kama suspense ya movie nzuri—yaani hata mtoto wao anaingia duniani na style! 🎬✨

🎶 Wimbo Mpya Wenye Maana Kubwa: “Ametutendea”

Katika kusindikiza ujio wa mtoto wao, Michael Yena ameendelea kusukuma wimbo wake mpya “Ametutendea”—na kwa kweli, jina la wimbo linazungumza moja kwa moja na tukio la maisha yao. Ni ushuhuda wao.

👉 Tazama video ya wimbo huo hapa:
🔗 Ametutendea – Michael Yena (Official Video)

Wimbo huu ni wimbo wa ushuhuda, wa shukrani, na wa imani. Ukiusikiliza huku ukijua kuwa umetoka kwa mtu ambaye ameonja wema wa Mungu kwa kiwango hiki—huwezi kubaki vilevile!

💍 Safari ya Upendo Yao

Kwa wanaofuatilia historia yao ya kimapenzi na kiroho, Michael na Grace walifunga ndoa yao mwezi Aprili mwaka 2024. Kwa kipindi kifupi, wameonyesha mfano wa ndoa yenye msingi wa maombi, heshima na maelewano. Na sasa, wameingia katika ukurasa mpya wa maisha—ukurasa wa uzazi!

Tunawatakia kila la kheri katika safari yao ya kuwa wazazi. Dunia imepata mtoto mwingine wa neema, na hakika tunaamini huyu naye atakuwa baraka kwa vizazi. Kama ilivyo kwa mashairi ya wimbo wao mpya, tunaungana nao kusema kwa nguvu zote:

“AMETUTENDEA!” 🎉


📌 Endelea kutembelea www.cocomedia.co.ke kwa habari za utendeti, matukio ya kusisimua, habari na kila kinachohusu burudani.

Continue Reading

Entertainment

Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien

Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Published

on

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.

Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!

Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.

Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.

Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.

Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.

Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.

Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.

Continue Reading

Trending