Connect with us

News

Erastus Edung Ethekon Aapishwa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa Tume Ya IEBC

Published

on

Wenyekiti mpya wa Tume ya uchaguzi na mipaka Erastus Ethekon pamoja na makamishena wengine sita wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), wameapishwa leo Ijumaa Julai 11 katika jengo la Mahakama ya upeo.

Mwenyekiti huyo sasa atawaongoza makamishena wengine, Ann Nderitu, Moses Mukhwana, Mary Sorobit, Hassan Noor, Francis Adoul, na Fahima Abdallah kuhudumu katika time hiyo.

Awali zoezi la kuwapishwa makamishena hao, lilikuwa limesimamishwa kufuatia agizo la Mahakama kuu, iliyotaja ukiukwaji mkubwa wakati wa mchakato wa kuwateua makamishena hao.

Hata hivyo agizo hilo sasa limeondolewa na majina ya makamishena hao kuchapishwa upya katika gazeti rasmi la serikali hapo Jana Julai 10 2025.

Mnamo Julai 10 2025, Mahakama kuu ilikuwa imebatlisha uteuzi uliofanywa na Rais William Ruto wa Makamishena hao saba wa tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC), akiwemo mwenyekiti wake Erastus Ethekon.

Hata hivyo katika uamuzi huo, Mahakama ilimpa nafasi Rais William Ruto kuhalalisha uteuzi wa makamishena hao kwa kuondolewa mbali kwa agizo hilo la awali lililozuia kuchapishwa kwa majina ya makamishena hao katika gazeti rasmi la serikali kabla ya kula kiapo.

Katika uamuzi wao siku ya Alhamisi Julai 10 2025, majaji wa Mahakama hiyo Roseline Amburili, Jaji Bahati Mwamuye na John Chigiti, walisema kwamba Rais alipasa kuheshimu maagizo hayo ya Mahakama kwani si mapendekezo tu, bali yalikuwa na msingi wa kisheria na kuapishwa kwa Makamishena hao ungekuwa kinyume Cha Sheria, na kuwatoa imani Wakenya kwa Tume hiyo.

Tume hiyo sasa inajukumu kubwa la kushughulikia masuala nyeti yaliyokuwa yamekwama tangu kuvunjwa kwa tume iliyokuwa iliongozwa na Wafula Chebukati.

Miongoni mwayo ni chaguzi ndogo katika sehemu mbali mbali za uakilishi Wadi na Ubunge likiwemo eneo Bunge la Magarini Kaunti ya Kilifi.

Pia kuna suala la kusafisha sajili ya wapiga kura pamoja na kuchunguzwa upya kwa mipaka ya maeneo ya kiwakilishi kabla ya uchaguzi mkuu ujao wa 2027.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Published

on

By

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.

Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.

Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.

Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.

“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.

Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Published

on

By

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.

Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.

Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.

Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.

“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.

“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending