News
Erastus Edung Ethekon Aapishwa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa Tume Ya IEBC

Wenyekiti mpya wa Tume ya uchaguzi na mipaka Erastus Ethekon pamoja na makamishena wengine sita wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), wameapishwa leo Ijumaa Julai 11 katika jengo la Mahakama ya upeo.
Mwenyekiti huyo sasa atawaongoza makamishena wengine, Ann Nderitu, Moses Mukhwana, Mary Sorobit, Hassan Noor, Francis Adoul, na Fahima Abdallah kuhudumu katika time hiyo.
Awali zoezi la kuwapishwa makamishena hao, lilikuwa limesimamishwa kufuatia agizo la Mahakama kuu, iliyotaja ukiukwaji mkubwa wakati wa mchakato wa kuwateua makamishena hao.
Hata hivyo agizo hilo sasa limeondolewa na majina ya makamishena hao kuchapishwa upya katika gazeti rasmi la serikali hapo Jana Julai 10 2025.
Mnamo Julai 10 2025, Mahakama kuu ilikuwa imebatlisha uteuzi uliofanywa na Rais William Ruto wa Makamishena hao saba wa tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC), akiwemo mwenyekiti wake Erastus Ethekon.
Hata hivyo katika uamuzi huo, Mahakama ilimpa nafasi Rais William Ruto kuhalalisha uteuzi wa makamishena hao kwa kuondolewa mbali kwa agizo hilo la awali lililozuia kuchapishwa kwa majina ya makamishena hao katika gazeti rasmi la serikali kabla ya kula kiapo.
Katika uamuzi wao siku ya Alhamisi Julai 10 2025, majaji wa Mahakama hiyo Roseline Amburili, Jaji Bahati Mwamuye na John Chigiti, walisema kwamba Rais alipasa kuheshimu maagizo hayo ya Mahakama kwani si mapendekezo tu, bali yalikuwa na msingi wa kisheria na kuapishwa kwa Makamishena hao ungekuwa kinyume Cha Sheria, na kuwatoa imani Wakenya kwa Tume hiyo.
Tume hiyo sasa inajukumu kubwa la kushughulikia masuala nyeti yaliyokuwa yamekwama tangu kuvunjwa kwa tume iliyokuwa iliongozwa na Wafula Chebukati.
Miongoni mwayo ni chaguzi ndogo katika sehemu mbali mbali za uakilishi Wadi na Ubunge likiwemo eneo Bunge la Magarini Kaunti ya Kilifi.
Pia kuna suala la kusafisha sajili ya wapiga kura pamoja na kuchunguzwa upya kwa mipaka ya maeneo ya kiwakilishi kabla ya uchaguzi mkuu ujao wa 2027.
News
Kongamano la mabadiliko ya hali ya anga lafanyika Mombasa

Mratibu wa Kongamano la kimataifa linaloangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga, INTER- GOVERNMEMTAL PANEL ON CLIMATE CHANGE, Patricia Nying’uro amesema jamii inasalia kuwa kiungo muhimu katika harakati za kuangazia mfumo wa mabadiliko ya hali ya hewa.
Kufuatia hilo, Nying’uro alitoa wito kwa wadau wa mazingira kuwekeza zaidi na kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika kudhibiti mabadiliko hayo.
Nying’uro alisema Kongamano ambalo linaendelea katika kaunti ya Mombasa, linaangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga na limewekeza kutambuliwa na jamii katika mikakati hiyo.
Akizungumza katika eneo la Shanzu wakati wa majadiliano hayo, Nying’uro alisema jumla ya mataifa 56 kati ya mataifa 195 yanayoshiriki kwenye mchakato wa kuweka mipango, sera na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa yanakongamana eneo la Shanzu ili kuanisha ripoti ambayo itatoa muongozo rasmi wa kuangazia makali ya mabadiliko ya hali ya hewa.
Wakati huohuo, Nying’uro alisema pia kongamano hilo la kimataifa lina umuhimu mkubwa kwa taifa hili kwani Kenya itahusishwa moja kwa moja katika kupangilia sera za kimataifa za kudhibiti athari ya mabadiliko ya hali ya anga.
Taarifa ya Janet Shume
News
Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya TB

Kaunti ya Mombasa imetajwa miongoni mwa kaunti zinazoongoza kwa maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu eneo la pwani.
Everlyn Kibuchi mkurugenzi wa mradi wa kuhamasisha kuhusu ungojwa wa kifua kikuu unaofahakima kama Stop TB Project, alitaja mikusanyiko ya watu, ukosefu wa lishe bora na magonjwa ya kuambukiza miongoni mwa vinavyochangia maambukizi ya TB.
Akizungumza katika warsha iliyowaleta pamoja wanahabari jijini Mombasa, Kibuchi alisistiza umuhimu kwa jamii kufahamu dalili za maradhi ya kifua kikuu na kupata matibabu kwa wakati unaofaa.
“Mombasa ni eneo moja ambalo liko na janga kubwa sana la kifua kikuu nchini, changamoto ambayo inafanya kifua kikuu iwe shida zaidi hapa Mombasa ama pwani nimkwamba Tb inaenea zaidi mahali ambapo kuna mkusanyiko wa watu, kama mtu amepatikana na huo ugonjwa inafaa wale ambao wanaishi nayeye wao pia wanafaa wapimwe kwa sababu kunauwekano kuwa wameambukizwa”, alisema Kibuchi.
Mkurugeniz huyo vile vile alisema unyanyapaa miongoni mwa wanaoishi na ugonjwa wa kifua kikuu umechangia wengi kukosa kufanyiwa vipimo kwa hofu ya kupatikana na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ukimwi.
“Watu wanaogopa kwenda kupimwa kwa sababu wakoishi katika hali ya unyayapaa, wanmajishuku pengine wakipatikana na kifua kikuu watapatikana na maambukizi ya ukimwi, sio watu watote ambao wako na kifua kikuu wanaishi na ukimwi, ni asilimia 23 ya watu Kenya nzima ambao wako na kifua kikuu na ambao wako na ukimwi, hii inamaanisha asilimia 70 hawana virusi”, aliongeza Kibuchi
Kwa upande wake Deche Sanga afisa anayesimamia kitengo cha ugonjwa wa kifua kikuu katika kaunti ya Kilifi, aliweka wazi kwamba waraibu wa dawa za kulevya 5,000 kaunti ya Kilifi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi ya TB, japo wameweka mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.
“Kilifi tuko na takriban waru 5,000 wanaotumia dawa za kulevya, asimilia kubwa ya wanaoishi na TB wanaishi katika haya maeneo ambayo wanavuta unga, hii imefanya Kilifi tumekuja na mbinu ya kudhibiti hili tatizo, tumefungua vituo vya waraibu wa kurekebisha tabia tukishirikiana na wadau wengine, kwa mfano tuko na Omar project Malindi, malengo yake ni kupunguza madhara tukichanganya na HIV”, alisema Sanga.
Taarifa ya Joseph Jira