Business
Sekta ya Uchukuzi Yatikiswa na Kupanda kwa Bei ya Mafuta

Sekta ya uchukuzi huenda ikaathirika hata zaidi baada ya mamlaka ya kudhibiti kawi nchini kuongeza bei ya mafuta ya petrol , disel na mafuta ya taa.
Kulingana na wahudumu wa matatu,tuktuk na bodaboda kutoka kaloleni kaunti ya kilifi bei mpya ya mafuta ambayo imetangazwa na mamlaka hiyo ,huenda ikawazaimu kupandisha nauli ili kukuendelea kujikimu kimaisha.
Aidha wahudumu hao wamesema hatua hiyo huenda ikasababisha kudorora kwa biashara kwani wateja wengi watalazimika kutembea kwa miguuu hali ambayo itafanya maisha kuwa magumu .
Wakizungumza na cocofm wahudumu wa boda boda wameikosoa serikali kwa kushindwa kupunguza gharama ya maisha jinsi walivyoahidi wakati wa kampeini.
Wakati huo huo wafanyabiashara wadogo wadogo katika eneo hilo wameeleza wasiwasi wao kuhusu kupanda kwa bei hizo hasa wanaotegemea mafuta ya taa wakisema maisha yatakuwa magumu zaidi.
Business
Wahudumu wa Uchukuzi Kilifi Walia na Kupanda kwa Bei ya Mafuta

Siku moja baada ya mamlaka ya udhibiti wa kawi nchini, EPPRA kutangaza kupandishwa kwa bei ya mafuta, sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Kilifi inaelezea hofu ya kuathirika kwa biashara zao.
Wahudumu wa tuktuk,teksi, bodaboda na magari ya usafiri wa umma hapa mjini Kilifi wanasema kupanda kwa bei ya petrol na diseli kutaathiri pakubwa sekta hiyo ya uchukuzi.
Sasa wanasema kuwa watalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na gharama ya mafuta.
Ni hali ambayo imeathiri wakaazi ambao wanatarajiwa kutumia vyombo hivyo vya usafiri wakisema kuwa watalazimika kutembea kwa mguu kwa safari fupi fupi katika utekelezaji wa shughuli zao za kawaida.
Hatahivyo wametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa inaingilia kati ili kuona kwamba bei za mafuta zinadhibitiwa.
Haya yamejiri huku lita moja ya mafuta aina ya petrol kaunti ya KIlifi ikiuzwa kwa shilingi 183.88 huku diseli ikiuzwa kwa shilingi 169.16 kila lita.
Lita moja ya mafuta ya taa inauzwa kwa shilingi 153.29.
Business
Uhusiano wa Kibiashara kati ya Kenya na Ufaransa Waonyesha Ukuaji Chanya

Takwimu za kibiashara kati ya kenya na ufaransa katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa mwaka 2024 zinaonyesha kuwa ufaransa ilileta humu nchini bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 6.5 na kuagiza bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 5.7 kutoka humu nchini hali iliyoleta uwiano bora wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili.
Nchi hiyo sasa inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na kenya ambapo kenya imewaalika waekezaji zaidi kutoka nchini ufaransa kuekeza katika sekta kadhaa za kenya.
Waziri mwenye mamlaka makuu Msalia Mdavadi anasema ufaransa inalenga sekta za kawi, miundomsingi na tekinolojia ili kuongeza biashara kati yake na kenya.