Connect with us

Uncategorized

Douglas Kanja, Mohammed Amin wakosa kufika mahakamani.

Published

on

Siku kumi baada ya mwanablogu Ndiang’ui Kinyagia kutoweka, kesi ya kumtaka inspecta jenerali wa polisi Doglas Kanja kueleza alipo mwanablogu huyo iliendelea kusikilizwa katika mahakama ya Milimani jijini Nairobi.

Inspecta jenerali wa polisi Douglas Kanja pamoja na mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa makosa ya jinai DCI Mohammed Amin walikosa kufika katika mahakama kama ilivyo amriwa hapo awali.

Haya yanajiri huku maafisa wa DCI wakiongozwa na mkurugenzi wa DCI wakiiambia mahakama siku ya jumatatu 30 juni 2025 kwamba hawakumkamata mwanablogu huyo.

Kwa upande wake Jaji Chacha Mwita aliwataka wawili hao kuhakikisha wanaeleza alipo mwanablogu huyo.

“Hakuna vile mtu anaweza toweka ghafla na hajulikani alipo, hatutaki maneno mengi tunachotaka ni huyu mtu ako wapi mleteni mbele ya mahakama awe hai au mfu tunachotaka ni huyu mtu yupo wai?”,aliuliza jaji Chacha Mwita.

Viongozi mbalimbali akiwemo kinara wa chama cha PLP Martha Karua, mbunge wa Embakasi Mashariki Paul Ongili Owino maarufu Babu Owino miongoni mwa viongozi wengine walihudhuria kikao cha kesi hiyo huku Karua akisema kwamba, wawili hao wameonyesha utovu mkubwa na nidhamu kwa kukiuka amri ya mahakama.

Ikumbukwe kwamba mwanablogu Kinyagia alikamatwa tarehe 21 juni 2025 kwa kosa la uhalifu wa kimitandao ikiwa ni kuchapisha ratiba ya maandamano yaliyofanyika Jumatano tarehe 25 Juni 2025.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Uncategorized

Kaunti ya Mombasa Yatakiwa Kuchukua Hatua za Dharura Kusafisha Soko la Marikiti

Published

on

MOMBASA – Serikali ya Kaunti ya Mombasa imetakiwa kuchukua hatua za haraka kuondoa taka zilizorundikana katika soko la Marikiti, hatua inayolenga kupunguza hatari ya kiafya na uvundo unaosababishwa na uchafu huo, hasa katika msimu huu wa mvua.

Akizungumza na wanahabari, Mwenyekiti wa soko hilo, Muhammad Ali, amesema kuwa hali ya uchafu sokoni hapo imefikia kiwango cha kutisha, huku baadhi ya wanunuzi wakikwepa kufika sokoni humo kutokana na harufu kali na mazingira yasiyovutia.

“Tumejaribu kuwasiliana na serikali ya kaunti mara kadhaa kuhusu suala hili, lakini hadi sasa hatujapata suluhisho la kudumu. Taka zimejaa kila kona ya soko, na hali hii si tu inatishia afya ya wananchi, bali pia inasababisha hasara kwa wafanyabiashara,” alisema Ali.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo, mvutano kati ya serikali ya kaunti na baadhi ya wafanyabiashara kuhusu ni nani anapaswa kukusanya taka umekuwa kizingiti kikuu katika kutatua changamoto hiyo. Hata hivyo, amesisitiza kuwa ni jukumu la moja kwa moja la serikali ya kaunti kuhakikisha kuwa huduma za ukusanyaji taka zinatolewa kwa wakati katika masoko yote ya umma.

“Hili si suala la kubebana lawama. Serikali ya kaunti ina wajibu wa kuhakikisha mazingira safi na salama kwa wafanyabiashara na wateja,” aliongeza.

Wafanyabiashara sokoni Marikiti wanasema hali hiyo imeathiri sana mapato yao, huku wakiitaka kaunti kuingilia kati na kurejesha heshima ya soko hilo linalohudumia maelfu ya wakazi wa Mombasa kila siku.

Continue Reading

News

Ujenzi wa Barabara ya Kuelekea Timbo za Jaribuni Kuanza

Published

on

By

Kikao cha kutafuta mwafaka kuhusu mzozo uliyoshuhudiwa kati ya wakaazi wa eneo la Jaribuni kaunti ya Kilifi na wawekezaji wa timbo za eneo hilo uliyosababisha kufungwa kwa barabara, kilifanyika ramsi.

Kikao hicho kilichoongozwa na Waziri wa madini na Uchumi samawati nchini Ali Hassan Joho kilijumuisha pia wawekezaji wa timbo hizo na wenyeji kama hatua moja wapo ya kuibuka na mwafaka.

Kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro kimeshuhudia kuanzishwa kwa mradi wa ujenzi wa barabara zinazoelekea katika timbo za eneo hilo la Jaribuni.

Japo barabara hizo zimesalia kufungwa kufuatia maandamano yaliyoshuhudiwa ya wenyeji wakilalamikia uchafuzi wa mazingira, ubovu wa barabara pamoja na kupuuzwa kwa miradi ya maendeleo, huenda sasa mwafaka wa mzozo huo ukapatikana

Continue Reading

Trending