News
Dkt. Nzai, awahimiza vijana kujisajili kwa mpango wa elimu kwa wote

Kama njia mojawapo ya kuimarisha vijana wa Pwani kupitia elimu, Jumuiya ya kaunti za Pwani imeanzisha mpango wa elimu kwa wote unaotoa elimu ya juu kupitia mtandao.
Mkurugenzi wa Jumuiya ya kaunti za Pwani, Dkt. Emmanuel Nzai alisema wanalenga vijana elfu tano kupitia mpango huo huku idadi lengwa ya vijana wa kaunti ya Kilifi ikiwa 700.
Dkt. Nzai alitoa wito kwa vijana kujisajili kwenye mpango huo ikizingatiwa kwamba ni vijana 25 pekee katika kaunti ya Kilifi ambao tayari wamejisajili kwenye mpango huo.
Dkt. Nzai alidokeza kwamba wanashirikiana na taasisi ya kimataifa ya Regeneysis kufanikisha mpango huo.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu kaunti ya Kilifi Felkin Kaingu alisema kupitia wafadhili mbalimbali watahakikisha kuwa vijana watakaojisajili kwenye mpango huo wanafadhiliwa kuendeleza masomo yao.
Hata hivyo vijana ambao tayari walinufaika na mpango huo walisisitiza haja ya hamasa zaidi kutolewa kwa vijana hasa wa mashinani ili wapate kujua kuhusu mpango huo wa elimu kwa wote.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.
Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.
“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.
Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
KHRC: Wasichana elfu moja ni wajawazito, Lamu

Takribani wasichana elfu moja kaunti ya Lamu wameripotiwa kupata mimba za utotoni kati ya mwaka wa 2024/25 huku visa vingi vikichangiwa na dhulma za kingono na ndoa za mapema.
Kulingana na Masharika ya kutetea haki za kibinadamu la MUHURI pamoja na lile la Kenya Human Rights Commission, KHRC serikali imeshindwa kuwakabili kisheria wahusika huku waathiriwa ambao ni wasichana wadogo wakiendelea kuhangaika.
Takwimu kutoka kwa kamati ya jinsia kaunti ya Lamu, iliwasilisha kwa kamati ya kitaifa inayoangazia masuala ya dhulma za jinsia kuwa kaunti hiyo ilinakili visa zaidi ya 700 vya mimba za utotoni mwaka wa 2024.
Takwimu hioz pia ziliweka wazi kwamba visa vingine zaidi ya 200 viliripotiwa kati ya mwezi Januari na Mei mwaka huu wa 2025.
Kulingana na ripoti kutoka kwa baraza la kitaifa la kudhibiti magonjwa NSDCC ilieonysha kwamba wasichana wanarika zaidi ya 600 nchini walipata mimba mwaka 2023.
Taarifa ya Janet Mumbi