Connect with us

Sports

Djokovic Kuzipiga Na Sinner Nusu Fainali Ya Tennis Mjini Wimbledon

Published

on

Matumani ya bingwa wa mpira wa Tennis Novak Djokovic kupata taji la 25 la Grand slam katika historia ya mchezo huo yangali hai anaposhuka dimbani kwa Nusu fainali dhidi ya mchezaji anayeorodheshwa wa kwanza ulimwenguni kwa sasa Jannik Sinner.

Raia huyo wa Serbia alijitosa kwenye awamu hiyo kwa kushinda Flavio Cobolli raia wa Marekani kwa seti za  6-7 (6/8), 6-2, 7-5, 6-4 katika awamu ya robo fainali mbele ya malkia wa Britain Camila.

Kwa upande wake mchezaji namba moja Jannik Sinner alimpiku mwenzake Ben Shelton raia wa Marekani anayeorodheshwa wa 10 ulimwenguni kwa seti za 7-6 (7/2), 6-4, 6-4.

Katika Nusu fainali ya pili mchezaji anayeorodheshwa wa pili ulimwenguni Carlos Alcaraz kuzipiga dhidi ya Taylor Fritz raia wa marekani.

Upande wa akina dada mwanadada anayeorodheshwa wa kwanza ulimwenguni Aryna Sabalenka atajitosa ugani kucheza dhidi ya Amanda Anisimova raia wa Marekani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending