Entertainment
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake

Mmiliki wa Crack Sound Records, J Crack, amepata pigo kubwa baada ya studio yake kuvamiwa na wezi walioiba vyombo vyake vya studio.
Akizungumza na kipindi cha Coco Drive cha COCO FM, msanii huyo alieleza kwa masikitiko jinsi wezi walivyoiba kila kitu, kuanzia vifaa vya muziki hadi mali ndogo ndogo za studio.
“Wameiba hadi kufuli ya mlango, computer ya kazi niliyotoka nayo Ulaya, laptop, TV mbili za reception na studio, electric guitar, piano… CCTV nimenunua sasa baada ya kuibiwa,” alisema J Crack kwa majonzi.
Kisa hiki kimewavunja moyo wasanii waliokuwa wakifanya kazi chini ya lebo hiyo, ikiwemo Susumila, ambaye pia alikuwa na mradi wake binafsi studioni humo.
J Crack pia alidokeza kwamba alikuwa akipanga kuachia EP mpya, lakini sasa mipango hiyo imelazimika kusimama kwa muda kufuatia hifadhi ya EP yake kuibwa pamoja na vyombo vyake.
Licha ya kupoteza mali nyingi, J Crack anasema hana mpango wa kukata tamaa.
“Mwizi hajanikata miguu. Crack Sound siyo mashine, ni vichwa. Wangenikata kichwa hapo sasa wangekuwa wamenimaliza. Tunaendelea mbele,” alisisitiza.
J Crack pia alisema kwamba Susumila ambaye alipata taarifa hizo aliahidi kumsaidia kuwapata walihusika kutekeleza wizi huo akisema kwamba atayashughulikia kinyumbani.
“Susumila aliniambie tumuachie yeye, halafu sisi tudeal na polisi,” alisema kwa msisitizo.
Mashabiki wa muziki wameeleza masikitiko yao mtandaoni, wakimtakia J Crack na timu yake nguvu mpya na kurejea kwa kasi kwenye game.
Entertainment
Paula Kajala Afunguka Sababu ya Kumtema Rayvanny

Mwanamitindo na mtangazaji maarufu kutoka Tanzania, Paula Kajala, hatimaye amevunja ukimya na kueleza sababu za kuachana na msanii nyota Rayvanny.
Katika mahojiano ya wazi, Paula alifichua kuwa uhusiano huo haukuweza kudumu kwa sababu ya kile alichokitaja kama kukosa uthabiti na kutoheshimu hisia za wanawake kwa upande wa msanii huyo.
Paula alisema kuwa safari yake ya mapenzi na Rayvanny ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.
“Hajali hisia za mtu yeyote. Alikuwa na Fahima, akaja kwangu, baadaye akaonekana na Feza, na sasa amerudi tena kwa Fahima. Hivyo basi, msishangae kesho mkimuona na mwanamke mwingine. Kwake yeye ni kiki na kubaki trending tu,” Paula alieleza.
Kulingana naye, mabadiliko ya mara kwa mara ya msanii huyo kati ya wanawake mbalimbali yalifanya iwe vigumu kujenga mustakabali thabiti wa pamoja.
Paula alitumia nafasi hiyo kuonya wanawake wanaotamani kuwa na uhusiano na watu mashuhuri kama Rayvanny kuchukua tahadhari.
“Wanawake wanapaswa kuchunguza tabia ya mwanaume kabla ya kuingia kwenye uhusiano. Kwa Rayvanny, mara nyingi huwa ana wanawake kadhaa kwa wakati mmoja,” aliongeza.
Kauli za Paula zilisambaa kwa kasi mitandaoni, zikizua mjadala mpana kuhusu changamoto za kuwa na uhusiano na wasanii wakubwa.
Wengi walihoji kama maisha ya umaarufu yanaweza kuendana na mahusiano ya kudumu, huku wengine wakiona kuwa tabia ya Rayvanny ni taswira ya changamoto zinazowakabili wanawake wengi wanaojaribu kujenga familia na wanaume maarufu.
What do youy think?
Entertainment
Good Morning to All Dianas, Aandika Diana Yegon Baada ya Kauli ya Pastor Ezekiel

Mwanahabari na mke wa Presenter Kai, Diana Yegon, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kuandika ujumbe wa ucheshi uliolenga wanawake wote wanaoitwa Diana.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Diana aliandika:
“Good morning to all ladies called Diana. Naskia sifa zetu nzuri nzuri sana. 😁”
Kauli hii imetafsiriwa na mashabiki wake kama jibu la kifahari na la utani kwa maneno ya Pastor Ezekiel, ambaye siku za hivi karibuni alizua mjadala mkubwa baada ya kudai kwamba wanawake wenye jina Diana ni wenye tabia zinazoweza kuvuruga ndoa.
Katika mahubiri yake, Pastor Ezekiel alisikika akisema:
“Ukioa mwanamke anaitwa Diana uishi na yeye, jua yeye ndiye ataku-control kama robot, ndiyo hiyo ndoa idumu… Yeye ndiye atakuwa husband, lakini wewe ukiwa mume, Diana hawezi dumu kwa ndoa… Pia jua ukioa Diana, lazima utashare na watu, sababu jina Diana imebeba mapepo… Hiyo ni ukweli mtupu!!!”
Kauli hii ilisambaa kwa kasi mitandaoni, huku ikiwasha mjadala mpana kuhusu imani, mitazamo ya kijamii na namna majina yanavyohusishwa na tabia za watu.
Badala ya kuingia kwenye malumbano, Diana aliamua kutumia uchemfu na ucheshi kujiweka mbali na mitazamo hiyo. Ujumbe wake wa “Good morning…” ulionekana kama njia ya: Kujipa nguvu na kuonyesha kujiamini kama mwanamke, Kuwatia moyo wanawake wote wanaoitwa Diana ambao huenda walihisi kushutumiwa na kauli ya mhubiri huyo, Kupunguza ukali wa mjadala kwa kutumia mzaha na mtindo wake wa kawaida wa kuchekesha mashabiki.
Mara baada ya posti hiyo, sehemu ya maoni ilijaa vicheko, pongezi na mijadala mikali. Wengi walimpongeza Diana kwa kuchukua hatua ya kugeuza maneno ya ukosoaji kuwa kicheko, wakisema kuwa huo ndio mfano wa kujua thamani yako bila kuyumbishwa na mitazamo ya nje.
Wengine walihoji uhalali wa kauli za kiroho zinazohusisha majina na tabia, wakisisitiza kuwa utu wa mtu hautokani na jina lake bali na malezi, maamuzi na imani.
Mjadala huu unaakisi hali halisi ya jamii ya sasa, ambapo mitazamo ya kidini, mila na maoni binafsi mara nyingi huibua tafsiri tofauti.
Kwa upande mmoja, kuna wale wanaoamini kabisa nguvu za majina, na kwa upande mwingine, kuna kizazi kipya kinachoona jina si kigezo cha utu wa mtu.
Kwa Diana Marua, kauli yake imezidi kuimarisha taswira yake kama msanii na mwanamke jasiri ambaye hajivunji moyo na maneno ya kukatisha tamaa.