Connect with us

News

Chonga, Akemea Idara ya Polisi kwa Kukiuka Sheria za Ardhi

Published

on

Mbunge wa Kilifi kusini Ken Chonga ameikemea Idara ya Polisi kwa kukiuka sheria na kushirikiana na mabwenyenye kuwahangaisha wakaazi kwenye ardhi zao.

Chonga amekariri kwamba kutokana na ulegevu unaoshuhudiwa kwenye idara ya polisi, baadhi ya mabwenyenye wamekuwa wakiendeleza tabia ya kuwatumia polisi vibaya ili kuwanyanyasa wakaazi kuhusu suala la ardhi.

Aidha ameeleza kuchukizwa na hulka hiyo ya kuwafurusha wakaazi kwenye ardhi zao kwa madai ya kuwa wamiliki halali wa ardhi hizo, akisema wengi wa wakaazi wameishi kwenye ardhi hizo tangu jadi.

Wakati huo huo amesema tayari analenga kufanya mazungumzo na wakuu wa idara ya polisi nchini sawa na Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro ili kuibuka na suluhu kuhusu suala hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Serikali na Wadau wa mazingira wapanda miti, Sabaki

Published

on

By

Serikali ya kitaifa kwa ushirikiano na mashirika ya kimazingira kaunti ya Kilifi inaendeleza mpango wa upanzi wa miti ili kuboresha mazingira.

Kulingana na Katibu wa masuala ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs, mpango huo unalenga kurudisha hadhi ya taifa la Kenya katika viwango vya kimazingira.

Akihutubia Wananchi wakati wa zoezi la upanzi wa mikoko katika eneo la Sabaki kaunti ya Kilifi, Fikirini alibainisha kwamba kupitia zoezi hilo jumla ya Miche elfu mbili ya mikoko kutoka kwa serikali na mashirika ya uhifadhi wa Mazingira imepandwa katika eneo hilo.

“Tumepanga miti mingi sana, idara yetu ya vijana imetoa miche elfu na kupitia mashirika mengi hapa wametoa miche elfu kwa jumla tumepanda miti elfu mbili, asante sana kwani kwa kufanya hivyo unasaidia pakubwa”, alisema Fikirini.

Wakati huo huo ameihimiza wananchi kuzingatia suala la upanzi wa miti pamoja na kujiepusha na ukataji miti kiholela, akisisitiza haja ya wakaazi kulinda misitu ili kuiwezesha jamii kuwa mazingira bora.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Kindiki, ataka makubaliano kati ya serikali kuu na kaunti kutekelezwa

Published

on

By

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki ametaka makubaliano yote kati ya serikali za kaunti na ile ya kitaifa kutekelezwa kabla ya mwezi Disemba mwaka huu wa 2025.

Akizungumza katika makao yake ya Karen jijini Nairobi Jumatatu 23, Juni 2025, kwenye mkutano wa 27 kati ya serikali kuu na zile za kaunti kuhusu bajeti IBEC, Kindiki alisema kumekuwa na makubaliano ambayo yamekuwa hayafuatiliwi ili kutekelezwa.

Kindiki alisema serikali kuu imejitolea kuhakikisha serikali za kaunti zinafanikisha miradi mbalimbali na kuwataka maafisa wa serikali za kaunti na ile ya kitaifa kushirikiana kwa majadiliano.

Wakati huo huo alisisitiza haja ya kutafuta suluhu la matatizo yanayoathiri utendakazi wa serikali za kaunti huku akipuzilia mbali uwepo wa mzozo wowote baina ya serikali kuu na zile za kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi.

Continue Reading

Trending