Connect with us

Sports

Chelsea Mabingwa Kilabu Bingwa Duniani

Published

on

Miamba wa Uingereza kilabu ya Chelsea ndiyo mabingwa wa Fainali ya Kombe la Dunia baina ya vilabu baada ya kutia darasi kabila ya kukalifisha PSG kibano cha magoli 3-0 ugani Metlife jana usiku.

Kiungo mshambulizi Cole Palmer alikua nyota wa mchezo akianza safari ya kuwapa raha mashabiki wa The Blues dakika ya 22 kabila ya kuongeza la pili dakika ya 30 kisha Joao Pedro akifunga la tatu dakika ya 43.

Kilabu ya PSG ilimaliza mechi hiyo wachezaji 10 uwanjani baada ya kiungo wa Ureno Joao Neves kulisha kadi nyekundu dakika za jioni kipindi cha Pili.

Kwa mujibu wa kocha wa Chelsea Enzo Maresca walistahili ushindi kwani walikua timu bora uwanjani huku wakilimbisha sakafu timu yenye uwezo mkubwa Psg.

“Kuanzia Mwanzo tulikua timu bora,iliounda nafasi nyingi ,timu iliyo na kiu ya ushindi tulishinda wenzetu kila sehemu uwanjani.”

The Blues sasa watakua wanapumzika kabila kuanza kuwazia ligi kuu Uingereza mwezi ujao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.   

Published

on

By

Huku zikiwa zimesalia siku 15 pekee kung’oa nanga kwa kipute cha CHAN mwezi ujao,
Kenya imeratibiwa kupambana na DRC, Morocco, na Angola katika Kundi A linalotajwa kuwa ndio kundi gumu zaidi yaani Kundi la Kifo.
KUNDI B
Ni Taifa jirani la Tanzania, Burkina Faso, Madagascar na Jamhuri ya Africa ya Kati.
KUNDI C
Uganda itachuana na Algeria,Africa Kusini,Guinea na Nigeria.
KUNDI D:
Congo itakabana koo na Nigeria,Senegal na Sudan Kusini.
 Mechi hizi zitasakatwa katika nyuga za katika Kenya, Uganda na Tanzania,
Continue Reading

Sports

Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Published

on

By

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.

Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.

Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.

Continue Reading

Trending