Sports
Chama Cha Raga KRU Yapata Mwenyekiti Mpya

Chama Cha Raga nchini KRU kimemtangaza Harriet Okach kuwa mwenyekiti mpya kwenye shirikisho hilo kumrithi Sasha Mutai aliyejiuzulu wadhifa wake wiki jana.
Uteuzi huo uliothibitishwa siku ya Alhamisi inamaana kwamba Okach anakua mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti katika Shirikisho hilo la mchezo wa Raga nchini KRU.
Kabla ya kuteuliwa kwake Okach amekua msimazi wa mauzo kwenye shirikisho hilo,na sasa amesema kwamba analenga kuboresha shirikisho hilo na mchezo kwa jumla anachukua hatamu ya uongozi.
“Nataka nichukue fursa hii kuwashukuru nyote kwa kunipa nafasi hii kwanza shirikisho KRU,washikadhau nimeheshimika mno na nimeahidi sitawangusha ,matumaini yangu ni kufanya Mchezo wa Raga na wachezaji wa Raga kuwa katika mandhari mazuri siku za usoni.”
Mutai alijiuzulu wadhifa wake katika Shirikisho hilo kwa kile alichokitaja ni kutopata ungwaji mkono baina ya washikadau wa mchezo huo nchini.
Sports
Uhispania Yaikomoa Ufaransa Uefa Nations Ligi.

UEFA NATIONS LEAGUE
Mabingwa watetezi wa taji la Uefa Nations Ligi Uhispania wameingia kwenye fainali ya taji hilo kwa kishindo Jumapili hii baada ya kunyuka Ufaransa magoli 5-4 hapo jana ugani Allianz Arena.
Winga matata wa Athletico Bilbao Nico Williams aliweka uongozini Uhispania dakika ya 22 kabila ya mshambulizi wa Arsenal Mikel Merino kuweka la pili dakika ya 25 kipindi cha kwanza.
La Furia Roja aliendeleza walipoachia kipindi cha kwanza katika kipindi cha pili huku winga wa Barcelona Lamine Yamal akiweka chuma ya tatu dakika ya 54,na lingine dakika ya 67 kabila ya Pedri kuweka la nne dakika ya 55 na kufanya mambo kuwa magoli 5-0
Hata hivyo Ufaransa walirejea kwa kishindo wakijipatia magoli kupitia Kyllian Mbappe dakika ya 59 naye Ryan Cherki dakika ya 79 Randal Kolo Muani dakika ya 93 uhispania pia wakijifunga kupitia beki Vivian.
Fainali ya Uefa Nations ligi ni kati ya Uhispania na Ureno jumapili saa nne usiku.
News
Shule Ya Upili Ya Serani Ndiyo Mabingwa Eneo La Mvita

Timu ya shule ya upili ya Serani imetetea ubingwa wao wa eneo la Mvita baada ya kuwalaza Tononoka magoli 2-1 katika fainali iliyochezewa kwenye uwanja wa shule ya upili ya Khamis.
Emanuel Oroni aliwatanguliza Serani na goli la kwanza kupitia mkwaju wa penati kabla ya Ali Abdallah kusawazishia Tononoka, lakini goli lake Emanuel Ngala katika kipindi cha pili likawapa ubingwa huo.
Kulingana na kocha wa Serani Alex Shikanga ni kwamba wamekua na mazoezi kambambe kabila ya mashindano ya shule za Upili na walikua wanasubiri ushindi tu wala si kitu kingine.
“Tulikua tumejiandaa kwa ajili ya ushindi pekee tumekua na maandalizi mazuri na hivyo nilijua tuatshinda fainali hii,katika miaka mitano tumepoteza taji hili mara moja pekee.”
kwa upande wake kocha wa Shule ya Upili ya Tononoka Juma ALi Kalato amesema kwamba amesema kwamba amekubali matokeo baada ya changamoto si haba kabila ya mechi hiyo ya fainali baadhi ya wachezaji wakingonjeka.
“Nashukuru Mwenyemezi Mungu tumefika fainali na vijana wangu wamepambana kiume kwani kabila ya mechi tulikua na wagonjwa ila wamepambana inshallah tutashinda uko mbele.”
Katika upande wa wasichana Kaa Chonjo wameibuka mabingwa kwa kuwalaza Mekatitilili magoli 3-0.
Serani na Tononoka wataiwakilisha Mvita katika ngazi ya kaunti upande wa wavulana, na Kaa Chonjo na Mekatililii wakiwakilishja upande wa wasichana.