Connect with us

Sports

Bruno Akataa Al-Hilal

Published

on

Ni taarifa nzuri kwa mashabiki wa kilabu ya Manchester United kwani ,Kiungo na nahodha wa kilabu ya Manchester united Bruno Fernandes amekataa ofa ya pauni milioni 200 kutoka kilabu ya Al-Hilal ya saudia.

Mabingwa hao walikua wametoa ofa hiyo na ada ya ununuzi ya pauni milioni 100 kwa kilabu ya United kupata sahihi ya mchezaji huyo ila inaaminika familia imekua sababu kuu ya Mreno huyo kudinda kuondoka england.

Timu hiyo ilikua imempa kiungo huyo makataa ya wiki moja kuamua iwapo atajiunga nao au la. Hata hivyo baada ya kuketi mezani na mawakala wake na kilabu ya Manchester United inaaminika kwamba mchezaji amekubali kusalia barani Ulaya.

Kilabu ya Al-Hilal ilikua tayari kumpa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 mkataba wa miaka mitatu na mshahara mnono kujiunga nao msimu ujao ila uwamuzi huo umepokelewa vyema na usimamizi wa United ambao hawakua tayari kumwachilia nyota huyo.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Chama Cha Raga KRU Yapata Mwenyekiti Mpya

Published

on

By

Chama Cha Raga nchini KRU kimemtangaza Harriet Okach kuwa mwenyekiti mpya kwenye shirikisho hilo kumrithi Sasha Mutai aliyejiuzulu wadhifa wake wiki jana.

Uteuzi huo uliothibitishwa siku ya Alhamisi inamaana kwamba Okach anakua mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti katika Shirikisho hilo la mchezo wa Raga nchini KRU.

Kabla ya kuteuliwa kwake Okach amekua msimazi wa mauzo kwenye shirikisho hilo,na sasa amesema kwamba analenga kuboresha shirikisho hilo na mchezo kwa jumla anachukua hatamu ya uongozi.

“Nataka nichukue fursa hii kuwashukuru nyote kwa kunipa nafasi hii kwanza shirikisho KRU,washikadhau nimeheshimika mno na nimeahidi sitawangusha ,matumaini yangu ni kufanya Mchezo wa Raga na wachezaji wa Raga kuwa katika mandhari mazuri siku za usoni.”

Mutai alijiuzulu wadhifa wake katika Shirikisho hilo kwa kile alichokitaja ni kutopata ungwaji mkono baina ya washikadau wa mchezo huo nchini.

Continue Reading

Sports

Uhispania Yaikomoa Ufaransa Uefa Nations Ligi.

Published

on

By

UEFA NATIONS LEAGUE

Mabingwa watetezi wa taji la Uefa Nations Ligi Uhispania wameingia kwenye fainali ya taji hilo kwa kishindo Jumapili hii baada ya kunyuka Ufaransa magoli 5-4 hapo jana ugani Allianz Arena.

Winga matata wa Athletico Bilbao Nico Williams aliweka uongozini Uhispania dakika ya 22 kabila ya mshambulizi wa Arsenal Mikel Merino kuweka la pili dakika ya 25 kipindi cha kwanza.

La Furia Roja aliendeleza walipoachia kipindi cha kwanza katika kipindi cha pili huku winga wa Barcelona Lamine Yamal akiweka chuma ya tatu dakika ya 54,na lingine dakika ya 67 kabila ya Pedri kuweka la nne dakika ya 55 na kufanya mambo kuwa magoli 5-0

Hata hivyo Ufaransa walirejea kwa kishindo wakijipatia magoli kupitia Kyllian Mbappe dakika ya 59 naye Ryan Cherki dakika ya 79 Randal Kolo Muani dakika ya 93 uhispania pia wakijifunga kupitia beki Vivian.

Fainali ya Uefa Nations ligi ni kati ya Uhispania na Ureno jumapili saa nne usiku.

Continue Reading

Trending