News
Aliyekuwa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari Afariki Mjini London

Aliyekuwa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari, amefariki katika Hospitali Moja Mjini London leo Jumapili Julai 13, akiwa na umri 82.
Kiongozi huyo ambaye aliitawala Nigeria kwa vipindi viwili kidemokrasia, aliingia madarakani kwa mara ya kwanza kupitia mapunduzi ya mwaka1983, kabla ya kupinduliwa tena miaka miwili bàadaye.
Kisha mnamo mwaka 2015 akaandikisha historia kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa upinzani kumshinda Rais aliye mamlakani na kuchukua hatamu ya kuliongoza Taifa la Nigeria.
Buhari alichaguliwakwa kwa kipindi Cha pili cha miaka minne mnamo 2019 kabla ya kustaafu.
Rais wa sasa nchini humo Bola Ahmed Tinubu ametuma risala za rambi rambi kwa Mke wa Buhari na familia yake, huku akimtuma Naibu wake kusafiri hadi mjini London kuufanya matayarisho ya kusafirishwa kwa mwa mwili wa Marehemu Buhari hadi nchini Nigeria.
Buhari ambaye anatokea jamii ya Fulani, alizaliwa katika Jimbo la Daura Katsina, Kaskazini mwa Nigeria mnamo 1942 na kisha bàadaye kujiunga na mafunzi ya kijeshi katika jimbo la Kaduna.
Alianza kupata umaarufu wale wa kisiasa mnamo mwaka 1975 kufuatia mapinduzi ya Rais wa nchi hiyo wakati huo Yakubu Gowon.
Baadaye alichaguliwa kuwa Gavana wa kijeshi wa Jimbo la Borno ambalo katika miaka ya hivi majuzi limekumbwa na mashambulio makali kutoka kwa kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
News
Kongamano la mabadiliko ya hali ya anga lafanyika Mombasa

Mratibu wa Kongamano la kimataifa linaloangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga, INTER- GOVERNMEMTAL PANEL ON CLIMATE CHANGE, Patricia Nying’uro amesema jamii inasalia kuwa kiungo muhimu katika harakati za kuangazia mfumo wa mabadiliko ya hali ya hewa.
Kufuatia hilo, Nying’uro alitoa wito kwa wadau wa mazingira kuwekeza zaidi na kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika kudhibiti mabadiliko hayo.
Nying’uro alisema Kongamano ambalo linaendelea katika kaunti ya Mombasa, linaangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga na limewekeza kutambuliwa na jamii katika mikakati hiyo.
Akizungumza katika eneo la Shanzu wakati wa majadiliano hayo, Nying’uro alisema jumla ya mataifa 56 kati ya mataifa 195 yanayoshiriki kwenye mchakato wa kuweka mipango, sera na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa yanakongamana eneo la Shanzu ili kuanisha ripoti ambayo itatoa muongozo rasmi wa kuangazia makali ya mabadiliko ya hali ya hewa.
Wakati huohuo, Nying’uro alisema pia kongamano hilo la kimataifa lina umuhimu mkubwa kwa taifa hili kwani Kenya itahusishwa moja kwa moja katika kupangilia sera za kimataifa za kudhibiti athari ya mabadiliko ya hali ya anga.
Taarifa ya Janet Shume
News
Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya TB

Kaunti ya Mombasa imetajwa miongoni mwa kaunti zinazoongoza kwa maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu eneo la pwani.
Everlyn Kibuchi mkurugenzi wa mradi wa kuhamasisha kuhusu ungojwa wa kifua kikuu unaofahakima kama Stop TB Project, alitaja mikusanyiko ya watu, ukosefu wa lishe bora na magonjwa ya kuambukiza miongoni mwa vinavyochangia maambukizi ya TB.
Akizungumza katika warsha iliyowaleta pamoja wanahabari jijini Mombasa, Kibuchi alisistiza umuhimu kwa jamii kufahamu dalili za maradhi ya kifua kikuu na kupata matibabu kwa wakati unaofaa.
“Mombasa ni eneo moja ambalo liko na janga kubwa sana la kifua kikuu nchini, changamoto ambayo inafanya kifua kikuu iwe shida zaidi hapa Mombasa ama pwani nimkwamba Tb inaenea zaidi mahali ambapo kuna mkusanyiko wa watu, kama mtu amepatikana na huo ugonjwa inafaa wale ambao wanaishi nayeye wao pia wanafaa wapimwe kwa sababu kunauwekano kuwa wameambukizwa”, alisema Kibuchi.
Mkurugeniz huyo vile vile alisema unyanyapaa miongoni mwa wanaoishi na ugonjwa wa kifua kikuu umechangia wengi kukosa kufanyiwa vipimo kwa hofu ya kupatikana na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ukimwi.
“Watu wanaogopa kwenda kupimwa kwa sababu wakoishi katika hali ya unyayapaa, wanmajishuku pengine wakipatikana na kifua kikuu watapatikana na maambukizi ya ukimwi, sio watu watote ambao wako na kifua kikuu wanaishi na ukimwi, ni asilimia 23 ya watu Kenya nzima ambao wako na kifua kikuu na ambao wako na ukimwi, hii inamaanisha asilimia 70 hawana virusi”, aliongeza Kibuchi
Kwa upande wake Deche Sanga afisa anayesimamia kitengo cha ugonjwa wa kifua kikuu katika kaunti ya Kilifi, aliweka wazi kwamba waraibu wa dawa za kulevya 5,000 kaunti ya Kilifi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi ya TB, japo wameweka mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.
“Kilifi tuko na takriban waru 5,000 wanaotumia dawa za kulevya, asimilia kubwa ya wanaoishi na TB wanaishi katika haya maeneo ambayo wanavuta unga, hii imefanya Kilifi tumekuja na mbinu ya kudhibiti hili tatizo, tumefungua vituo vya waraibu wa kurekebisha tabia tukishirikiana na wadau wengine, kwa mfano tuko na Omar project Malindi, malengo yake ni kupunguza madhara tukichanganya na HIV”, alisema Sanga.
Taarifa ya Joseph Jira