Connect with us

News

Aliyekuwa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari Afariki Mjini London

Published

on

Aliyekuwa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari, amefariki katika Hospitali Moja Mjini London leo Jumapili Julai 13, akiwa na umri 82.

Kiongozi huyo ambaye aliitawala Nigeria kwa vipindi viwili kidemokrasia, aliingia madarakani kwa mara ya kwanza kupitia mapunduzi ya mwaka1983, kabla ya kupinduliwa tena miaka miwili bàadaye.

Kisha mnamo mwaka 2015 akaandikisha historia kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa upinzani kumshinda Rais aliye mamlakani na kuchukua hatamu ya kuliongoza Taifa la Nigeria.

Buhari alichaguliwakwa kwa kipindi Cha pili cha miaka minne mnamo 2019 kabla ya kustaafu.

Rais wa sasa nchini humo Bola Ahmed Tinubu ametuma risala za rambi rambi kwa Mke wa Buhari na familia yake, huku akimtuma Naibu wake kusafiri hadi mjini London kuufanya matayarisho ya kusafirishwa kwa mwa mwili wa Marehemu Buhari hadi nchini Nigeria.

Buhari ambaye anatokea jamii ya Fulani, alizaliwa katika Jimbo la Daura Katsina, Kaskazini mwa Nigeria mnamo 1942 na kisha bàadaye kujiunga na mafunzi ya kijeshi katika jimbo la Kaduna.

Alianza kupata umaarufu wale wa kisiasa mnamo mwaka 1975 kufuatia mapinduzi ya Rais wa nchi hiyo wakati huo Yakubu Gowon.

Baadaye alichaguliwa kuwa Gavana wa kijeshi wa Jimbo la Borno ambalo katika miaka ya hivi majuzi limekumbwa na mashambulio makali kutoka kwa kundi la wanamgambo wa Boko Haram.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Published

on

By

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.

Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.

Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.

Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.

“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.

Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Published

on

By

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.

Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.

Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.

Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.

“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.

“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending