Sports
Alexander Trent Arnold Sasa Ni Mali Ya Madrid

Kilabu ya Real Madrid imtangaza kupata sahihi ya beki wa taifa la Uingereza na kilabu ya Liverpool Alexander Trent Arnold.
Miamba hao wa Uhispania inaaminika imelipa kima cha Euro milioni 10 kupata sahihi ya beki huyo ambaye amechezea Liverpool tangu utotoni akitokea kwenye academia ya kilabu hiyo.
Trent mwenye umri wa miaka 26 ametia wino mkataba wa miaka sita kilabuni humo inayomueka hadi mwaka 2031.
Makubaliano hayo yakiwa pia kwamba kilabu ya Madrid italipa mshahara wake wa miezi za June na Julai.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuvalia jezi la Los Blancos kwa mara ya kwanza katika fainali ya kombe la Dunia baina ya vilabu mwezi ujao Juni 14.
Sports
Timu Ya Taifa Ya DR Congo Yawasili Nchini Kwa Mechi Ya Ufunguzi Dhidi Ya Harambee Stars

Timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DR Congo) imewasili nchini mapema leo kwa ajili ya mechi ya ufunguzi dhidi ya Harambee Stars itakayochezwa siku ya Jumapili.
Kikosi hicho, kilicho na wachezaji 25 pamoja na benchi la kiufundi, kiliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) na kupokelewa rasmi kabla ya kuelekea hotelini jijini Nairobi.
DR Congo, maarufu kama The Leopards, ni mabingwa mara mbili wa kombe hilo na wanatarajiwa kufanya mazoezi yao ya kwanza jioni ya leo katika Uwanja wa Kasarani.
Vijana hao wako katika Kundi A pamoja na wenyeji Kenya, pamoja na Angola, Morocco, na Zambia.
Sports
Waziri Wa Michezo Salim Mvurya Asema Kenya Iko Tayari Kwa CHAN

Waziri Mvurya, akizungumza katika Uwanja wa Nyayo, amesema kuwa fursa hiyo ni ya kipekee kwa taifa na sekta ya michezo kwa ujumla, huku maandalizi ya kuelekea AFCON 2027 yakiendelea.
Aidha, Mvurya amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushangilia timu ya taifa, Harambee Stars, katika mechi ya Jumapili na michezo yote ya michuano hiyo.
Harambee Stars itacheza mechi zake zote katika Uwanja wa Kasarani. Timu hiyo imo katika Kundi A pamoja na Angola, Morocco, Zambia, na DR Congo.