Connect with us

Sports

Alexander Trent Arnold Sasa Ni Mali Ya Madrid

Published

on

Kilabu ya Real Madrid imtangaza kupata sahihi ya beki wa taifa la Uingereza na kilabu ya Liverpool Alexander Trent Arnold.

Miamba hao wa Uhispania inaaminika imelipa kima cha Euro milioni 10 kupata sahihi ya beki huyo ambaye amechezea Liverpool tangu utotoni akitokea kwenye academia ya kilabu hiyo.

Trent mwenye umri wa miaka 26 ametia wino mkataba wa miaka sita kilabuni humo inayomueka hadi mwaka 2031.

Makubaliano hayo yakiwa pia kwamba kilabu ya Madrid italipa mshahara wake wa miezi za June na Julai.

Mchezaji huyo anatarajiwa kuvalia jezi la Los Blancos kwa mara ya kwanza katika fainali ya kombe la Dunia baina ya vilabu mwezi ujao Juni 14.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Waziri Wa Michezo Salim Mvurya Asema Kenya Iko Tayari Kwa CHAN

Published

on

By

SIKU 3 ZIMESALIA KUNGOA NANGA KOMBE LA CHAN:
Waziri wa Michezo, Salim Mvurya, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya CHAN, Nicholas Musonye, wamefanya ukaguzi wa mwisho leo katika viwanja vya Kasarani na Nyayo kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Harambee Stars na DR Congo itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Kasarani.

Waziri Mvurya, akizungumza katika Uwanja wa Nyayo, amesema kuwa fursa hiyo ni ya kipekee kwa taifa na sekta ya michezo kwa ujumla, huku maandalizi ya kuelekea AFCON 2027 yakiendelea.

Aidha, Mvurya amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushangilia timu ya taifa, Harambee Stars, katika mechi ya Jumapili na michezo yote ya michuano hiyo.

Harambee Stars itacheza mechi zake zote katika Uwanja wa Kasarani. Timu hiyo imo katika Kundi A pamoja na Angola, Morocco, Zambia, na DR Congo.

Continue Reading

Sports

Winga Wa Colombia Luis Diaz Sasa Ni Mali Ya Bayern

Published

on

By

Klabu ya Bayern Munich, inayoshiriki Ligi Kuu ya Bundesliga nchini Ujerumani, imetangaza kumsajili winga wa Colombia, Luis Díaz.

Hatua hii imekuja baada ya Bayern Munich na Liverpool kufikia makubaliano kuhusu uhamisho wa mchezaji huyo kwa ada ya pauni milioni 65.5.

Díaz, mwenye umri wa miaka 28, aliwasili mjini Munich hapo jana kwa ajili ya vipimo vya kitabibu kabla ya kutia saini mkataba wa miaka minne na mabingwa hao wa Ujerumani.

Mchezaji huyo alijiunga na Liverpool mwaka 2022 akitokea klabu ya Porto kwa ada ya pauni milioni 37. Tangu wakati huo, ameifungia Liverpool mabao 41 katika mechi 142 alizocheza uwanjani Anfield.

Nyota huyo aliondoka kwenye kambi ya mazoezi ya Liverpool mjini Hong Kong hapo jana na kujiunga rasmi na waajiri wake wapya kwa maandalizi ya msimu mpya.

Continue Reading

Trending