News
Afueni kwa wanaoishi na virusi vya HIV

Wakenya walio kwenye hatari ya kuambukizwa virusi vya HIV huenda wakaanza kupokea shindano mpya ya kudhibiti maambukizi kufikia januari mwakani.
Hii ni baada ya shirika la afya ulimwenguni W.H.O kuidhinisha sindano hiyo mpya ambapo Kenya ni kati ya mataifa 9 yatakayoanza kuitumia kwanza.
W.H.O ilitaja Kenya miongoni mwa mataifa yatakayoanzisha sindano ya Lenacapavir dawa ambayo inahitaji kudungwa mara mbili kwa mwaka ili kutoa kinga ya ugonjwa wa ukimwi.
Wazira wa afya nchini Aden Duale alisema Kenya tayari imeweka mikakati kuhakikisha kufikia mwakani wakenya ambao wako katika hatari ya maambukizi wamezuiwa.
Nchi nyingine 8 zitakazoanza kutumia Lenacapavir ni Uganda, Lesotho, Nigeria, Musumbiji, afrika kusini, Eswatini, Zambia na Zimbabwe.
Akitangaza hatua hiyo mjini Kigali nchini Rwanda mkurugenzi mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus aliyataka mataifa hayo kutekeleza kinga hiyo haraka iwezekanavyo.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Christine: Wahudumu wa afya 1,340 wapokea mafunzo Taita Taveta

Serikali ya kaunti ya Taita Taveta kupitia Wizara ya Afya inaendelea kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya wa nyanjani ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao bila vikwazo.
Naibu Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Christine Kilalo alisema kuwa kati ya wahudumu hao 1,340 asilimia 75 tayari wanaendelea na mafunzo katika ngazi tofauti.
Kilalo aliahidi kushirikiana na wahudumu hao licha ya changamoto zinazowakabili nyanjani.
“Wamekubali wakafundiashwa ili waweze kutoa elimu ya afya na waweze kusaidia jamii kwa mambo ya usafi na pia kusaidia katika kuwasilisha ujumbe za kiafya na pia wakipata wagonjwa waweze kuwatuma mahali wanaweza wakapata huduma za matibabu’’, alisema Kilalo.
Wakati uohuo alidokeza kuwa serikali ya kaunti hiyo kwa ushirikiano na serikali kuu wameweka mikakati ya kuhakikisha wahudumu hao wanalipwa fedha ambazo zitawasaidia kujikimu kimaisha pamoja na familia zao.
“Tulikubaliana kama taifa asilimi 50 ambayo ni elfu mbili mia tano inalipwa na serikali kuu na asilimia 50 ambayo ni elfu mbili mia tano inalipwa na serikali ya kaunti na kama serikali tunaemda kukamilisha malipo’’, aliongeza Kilalo.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Francisca atoa wito kwa vijana kuwania nyadhfa za kisiasa

Waziri wa masuala ya kijamii na ukuzaji wa talanta katika serikali ya kaunti ya Kwale, Francisca Kilonzo ametoa changamoto kwa vijana hasa wa Kike kwenye kaunti hiyo kujitokeza kwa wingi ili kuwania nyadhifa mbalimbali za kisiasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.
Kilonzo aliwataka kuwania nyadhfa za uongozi wa kaunti ya Kwale sawia na bunge la kaunti hiyo ili kuhakikisha idadi ya wanawake waliochaguliwa inaongezeka.
Kilonzo na Mwakilishi mteule katika bunge la kaunti ya Kwale Judy Kengo walisema ikiwa vijana hao watazingatia hilo kutakuwa na ongezeko la Wanawake serikalini.
‘’Na ni Kwale pekee ambapo unaona viongozi ambao wamechaguliwa ni kidogo ukilinganisha na zile kaunti zingine za maeneo ya kati miongoni mwa zingine viongozi ambapo idadi iko juu’’, alisema Kengo
Naye Afisa wa mipango katika shirika hilo Rachel Akinyi na mmoja wa wanawake katika kaunti hiyo, Furaha Nyuki wameitaka jamii kuwaunga mkono wanawake kwenye uchaguzi huo mkuu ujao.
Taarifa ya Janet Mumbi