Connect with us

News

Trent Arnold Aondoka Anfield

Published

on

Beki wa taifa la Uingereza Alexander Trent Arnold ametangaza kugura kilabu ya Liverpool baada ya msimu huu kukamilika. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ametangaza kugura kilabu hiyo baada ya kuhudumia kwa zaidi ya miaka 20 akitokea kwenye akademia ya The Reds.

kwenye kanda aliyopost kwenye mitandao yake ya kijamii beki huyo wa kulia ameshukuru kilabu hio na mashabiki wake kwa nafasi na ungwaji mkono ambao walimpa tangu akiwa  mchezaji mdogo kilabuni humo.

TAA amefanikiwa kufunga magoli 18 na kuwa beki aliyechangia kupiga basi nyingi epl akiwa amepakua pasi 64 kwa wenzake kufunga,akiwa ameshinda mataji 2 ya Epl moja ya kilabu bingwa ulaya miongoni mwa mataji mengine.

Inaaminika mchezaji huyo tayari amekubaliana na uhamisho wa bila malipo na kilabu ya Real Madrid baada ya kudinda kutia wino mkataba mpya na The Reds akiwa tayari amekubaliana na matakwa yake binafsi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Askofu Anyolo: Kadinali Njue Hatahudhuria Conclave

Published

on

By

Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Nairobi limetangaza kwamba John Kadinali Njue, hatashiriki Kongamano la kumchagua Papa mpya wa Kanisa Katoliki duniani.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na Kanisa hilo siku ya Jumanne, Kadinali Njue ambaye anastahili kupiga kura katika Kongamano hilo maarufu Conclave alikuwa amepokea mwaliko rasmi kutoka Shirika la kitume ili kuhudhuria Kongamano hilo ambalo linafaa kuanza rasmi tarehe 7 mwezi Mei mwaka huu lakini hataweza kusafiri.

Kanisa hilo limesema Mwakilishi wa Papa nchini Kenya Askofu Hubertus Marie Van Megen baada ya kushauriana na ofisi ya Askofu mkuu wa Nairobi Phillip Anyolo, alitoa taarifa kwamba Kadinali Njue mwenye umri wa miaka 80 hataweza kusafiri hadi Vatican- Roma kwa Kongamano hilo.

Picha kwa hisani

Askofu Anyolo amewataka waumini wa Kanisa Katoliki kuombea makadinali wanaochukua jukumu zito la kumchagua Papa mpya huku akihimiza maombi zaidi kwa ajali ya Afya na ustawi wa Kadinali Njue.

Continue Reading

News

Wachezaji 3 Kumkaba Yamal Leo Kilabu Bingwa

Published

on

By

Mkufunzi wa kilabu ya Inter Milan ya Italia Simeone Inzaghi amesema kwamba mechi ya leo kati yao na Fc Barcelona ni kufa kupona wakilenga tiketi ya kufuzu fainali ya kilabu bingwa ulaya mei 31 uwanjani Allianz Arena.

Akizungumza saa chache kabla ya mtanange huyo mwalimu huyo aidha amekiri ili kushinda mechi hiyo ni lazima wapate mbinu ya kuwazuia vizuri wapinzani wao kwa ustadi mkubwa la si hivyo watawadhuduru.

Miongoni mwa mikakati ambayo ameweka kocha huyo ni wachezaji watatu kumdhibiti winga matata na tineja Lamine Yamal mwenye umri wa miaka 17.

Kwa mujibu wa kocha huyo kama kuna mchezaji atasaidia Barcelona kuingia fainali basi ni makali ya mhispanyola Yamal,mchezaji huyo fundi alifunga goli kabla ya kuchangia lingine timu hizo ziktoka sare ya magoli 3-3 ugani stade olympique st.luis catalunya.

Na Simeone amesisitiza ni lazima wasimpe nafasi tineja huyo akitaka wachezaji watatu wawe naye anashika mpira.

Mechi hiyo inapigwa majira saa nne usiku Jumanne hii Ugani Sansiro Italia.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.