Connect with us

News

Mwadime: Visa vya Wakenya Kuteswa Nchini Saudia Vimepungua

Published

on

Katibu katika Wizara ya Leba nchini Shadrack Mwadime amesema visa vya wakenya kuteswa na kuuwawa katika mataifa ya ughaibuni hasa nchini Saudia Arabia vimepungua pakubwa.

Mwadime amesema kupungua kwa visa hivyo kumetokana na serikali kuchukua hatua hitajika za kutia saini mkataba wa makubaliano ya kazi baina ya nchi hizi mbili.

Mwadime amesema serikali ya Kenya inaendeleza mazungumzo na serikali ya Saudia ili kufanikisha mkataba huo na kuwawezesha wananchi kuwa huru pindi wanapopata ajira katika taifa hilo.

Katibu huyo amesema shughuli hiyo itakapofanikishwa ni wazi kwamba visa vya wakenya kuuwawa na kuteswa nchini Saudia vitasitishwa kabisa.

Wakati huo huo amewashauri wakenya kutembelea ubalozi wa Kenya ili kufahamisha ubalozi huo kuhusu kazi wanazoenda kuzifanya na kushauriwa zaidi kuhusu mwongozo wa jinsi watakavyoripoti visa vya unyanyasaji.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mbogo: Kaunti ya Mombasa Imeshindwa Kutatua Mzozo wa Ardhi

Published

on

By

Aliyekuwa mbunge wa Kisauni Ali Mbogo ameikosoa serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kushindwa kutatua suala tata la uskwota linalowakumba wakaazi wengi wa kaunti hiyo.

Akizungumza katika eneo la Kisauni katika kaunti ya Mombasa, Mbogo amesema tatizo la uskwota limeendelea kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya ardhi na ukosefu wa usalama katika maeneo mengi ya kaunti ya Mombasa huku serikali ya kaunti hiyo ikionekana kulifumbia macho suala hilo.

Mbogo amedai kwamba maelfu ya wakaazi wa Kisauni na Mombasa kwa jumla wanaishi kwa hofu ya kufurushwa katika ardhi zao walizoishi tangu jadi kufuatia ukosefu wa hati miliki.

Wakati huo huo amedokeza kwamba baadhi ya maafisa wa serikali ya kaunti hiyo wanahusishwa na visa vya uporaji wa ardhi za umma kwa kushirikiana na waekezaji jambo ambalo amelitaja kuwa dhulma.

Continue Reading

News

Tuko Tayari Kufuzu Kombe La Dunia

Published

on

By

Nahodha wa Kikosi cha Soka vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 Rising Stars Amos Wanjala amesema kwamba lengo lao kuu ni kufuzu kombe la dunia kwenye fainali ya mashindano ya Afcon kwa chipukizi iliofungua milango yake weikndi hii mjini Cairo Misri.

Akizungumza akiwa kambini mjini Cairo Wanjala anamini kwamba wana kikosi bora cha kuandikisha matokeo chanya kwenye kombe hilo licha ya kuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki katika kipute hicho.

“Tuko tayari kufuzu World cup maana tumekua tukijiandaa vyema kwa mashindano haya,nataka niwatoe hofu wakenya kwamba kundi letu ni la kifo kwani wawe tayari kupata burudani kutoka kwetu.”

kwa Mujibu wa tineja huyo wa academia ya Nasty Sports ya Uhispania ni kwamba licha mabadiliko ya hali ya anga akilinganisha na Kenya kila mmoja yuko tayari kuonyesha uwezo wake katika jukwaa hili.

“Tuko syched up kucheza na mpinzani yeyote,kila mmoja amejiandaa vizuri kutendea haki na kupeperusha bendera ya taifa letu. Nikitaka kushukuru wizara ya michezo pamoja na shirikisho kwa kutuunga mkono kuanzia mwanzo wa mazoezi yetu mpaka mandhari ambayo tumepata hapa.”

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeni dhidi ya Morocco May 1 wakiwa kundi B pamoja na Tunisia na vilevile Nigeria

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.