Connect with us

News

Mahakama ya Shanzu Imeagiza Mshukiwa wa Ugaidi Kuzuiliwa kwa Siku 14

Published

on

Mahakama ya Shanzu katika kaunti ya Mombasa imeagiza mshukiwa wa kundi la kigaidi la Al-Shabab Ramadhan Mohammed Hassan kuzuiliwa kwa siku 14 zaidi ili kuwawezesha maafisa wa Idara ya upelelezi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba Hassan alikamatwa katika eneo la Kichangii katika gatuzi dogo la Nyali kaunti ya Mombasa akiwa na vifaa vinavyodaiwa kutumiwa na kundi la Al-shabab kutekeleza mashambulizi.

Maafisa hao wa idara ya upelelezi wameeleza Mahakama kwamba simu ya mshukiwa ilipelekwa katika makao makuu ya kitengo cha kupambana na ugaidi nchini ATPU kwa uchunguzi zaidi.

Kulingana na maafisa hao, baada ya kufanya uchunguzi wa simu ya mshukiwa wamebaini kwamba mshukiwa alikuwa akiwasiliana na wanachama wengine wa kundi la kigaidi la Al-shabab ambao wako mafichoni katika mataifa ya Tanzania na Somalia.

Hata hivyo maafisa hao wameitaka Mahakama kutomuachilia mshukiwa huyo kwa dhamana, wakisema kwamba huenda akatoroka na kuathiri uchunguzi wa kesi hiyo, ombi ambalo Mahakama imelikubali.

Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 16 mwezi huu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mbogo: Kaunti ya Mombasa Imeshindwa Kutatua Mzozo wa Ardhi

Published

on

By

Aliyekuwa mbunge wa Kisauni Ali Mbogo ameikosoa serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kushindwa kutatua suala tata la uskwota linalowakumba wakaazi wengi wa kaunti hiyo.

Akizungumza katika eneo la Kisauni katika kaunti ya Mombasa, Mbogo amesema tatizo la uskwota limeendelea kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya ardhi na ukosefu wa usalama katika maeneo mengi ya kaunti ya Mombasa huku serikali ya kaunti hiyo ikionekana kulifumbia macho suala hilo.

Mbogo amedai kwamba maelfu ya wakaazi wa Kisauni na Mombasa kwa jumla wanaishi kwa hofu ya kufurushwa katika ardhi zao walizoishi tangu jadi kufuatia ukosefu wa hati miliki.

Wakati huo huo amedokeza kwamba baadhi ya maafisa wa serikali ya kaunti hiyo wanahusishwa na visa vya uporaji wa ardhi za umma kwa kushirikiana na waekezaji jambo ambalo amelitaja kuwa dhulma.

Continue Reading

News

Tuko Tayari Kufuzu Kombe La Dunia

Published

on

By

Nahodha wa Kikosi cha Soka vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 Rising Stars Amos Wanjala amesema kwamba lengo lao kuu ni kufuzu kombe la dunia kwenye fainali ya mashindano ya Afcon kwa chipukizi iliofungua milango yake weikndi hii mjini Cairo Misri.

Akizungumza akiwa kambini mjini Cairo Wanjala anamini kwamba wana kikosi bora cha kuandikisha matokeo chanya kwenye kombe hilo licha ya kuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki katika kipute hicho.

“Tuko tayari kufuzu World cup maana tumekua tukijiandaa vyema kwa mashindano haya,nataka niwatoe hofu wakenya kwamba kundi letu ni la kifo kwani wawe tayari kupata burudani kutoka kwetu.”

kwa Mujibu wa tineja huyo wa academia ya Nasty Sports ya Uhispania ni kwamba licha mabadiliko ya hali ya anga akilinganisha na Kenya kila mmoja yuko tayari kuonyesha uwezo wake katika jukwaa hili.

“Tuko syched up kucheza na mpinzani yeyote,kila mmoja amejiandaa vizuri kutendea haki na kupeperusha bendera ya taifa letu. Nikitaka kushukuru wizara ya michezo pamoja na shirikisho kwa kutuunga mkono kuanzia mwanzo wa mazoezi yetu mpaka mandhari ambayo tumepata hapa.”

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeni dhidi ya Morocco May 1 wakiwa kundi B pamoja na Tunisia na vilevile Nigeria

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.