Connect with us

Sports

George Foreman: Bingwa wa Masumbwi Afariki Dunia Akiwa na Miaka 76

Published

on

Bingwa wa zamani wa masumbwi kwa uzito wa juu George Foreman, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 76. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia yake na kunukuliwa na vyombo vya habari, Foreman alifariki huko nchini Marekani.
Foreman alijulikana sana Kwa kuzipiga ngumu na pambano lake la kihistoria, likiwemo lile la Rumble in the Jungle mwaka 1974 dhidi ya Muhammad Ali jijini Kinshasa DRC ambapo alipigwa kwa KO.
Aliiweka rekodi kwa kuwa bingwa wa uzani wa juu mwenye umri mkubwa zaidi (miaka 45) aliposhinda taji hilo mwaka 1994.
Mbali na masumbwi, Foreman alipata mafanikio makubwa kibiashara, hasa kupitia majiko yake ya umeme ya kuchoma nyama George Foreman Grill, ambapo alifanikiwa kuuza zaidi ya majiko milioni 100 duniani kote.
Foreman ameacha familia kubwa, wakiwemo watoto wake 12, wanawake 7 na wanaume 5 na wote wanaitwa George.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Liverpool Kutangazwa Bingwa Mpya Epl

Published

on

By

Miamba wa Uingereza kilabu ya Liverpool kutangazwa mabingwa wapya wa ligi kuu EPL Wikendi hii iwapo watatoka sare ya aina yoyote dhidi ya kilabu ya Tottenham Hotspurs ugani Anfield.

Haya yanajiri baada ya kilabu nambari mbili Arsenal kudondosha alama mbili muhimu siku ya jumatano dhidi ya Crystal Place timu hizo zikiisha sare ya magoli 2-2 uwanjani Emirates na kudidimiza matumaini yake ya kutwaa ubingwa wa Epl msimu huu.

Beki Jacob Kiwior aliweka uongozini The Gunners kunako dakika 3 kabla ya Palace kusawazisha kupitia kwa kiungo mshmabulizi Eze Oberechi kunako dakika ya 22 na licha ya kuchukua uongozi mwingine kupitia Leandro Trossard dakika ya 46,kilabu ya Palace ilijibu dakika ya 84 kupitia kwa mshambulizi Jean Philip Mateta.

Matokeo haya yanawacha Liverpool nafasi ya kwanza na alama 79 nayo Arsenal nafasi ya pili na alama 67 nayo mancity wakiwa nafasi ya tatu na alama 61 nayo Nottingham Forest ni ya nne na alama 60 mkiani ni vilabu vya Ipwisch Town,Leicester city na Southampton mtawalia.

Continue Reading

News

Matokeo Yataanza Kuja Tu

Published

on

By

Mkufunzi wa kilabu ya kiifi united Samson Jumbe amesema kwamba ana Imani vijana wake watarejea katika hali ya kupata matokeo chanya licha ya vijana wake kupoteza mechi 2 mfululizo ikiwemo debi kati yao na kilabu ya United Brothers mwishoni mwa jumwa

Kwa mujibu wa mwalimu huyo kwa sasa wanalenga kuimarisha safu yao ya mashambulizi ambayo imekua ikipoteza nafasi nyingi za wazi.

“Naamini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu vijana wangu wataanza kufunga magoli na kuanza kushinda mechi za ligi ya kaunti kuanzia wikendi hii nyumbani,mechi ya tumecheza vizuri kasoro magoli tu.”

Kwa upande wake kocha wa kilabu ya united Brothers Titus Kitaka amesema kwamba mazoezi mazito ambayo amekua na vijana wake imewasaidia pakubwa kupata matokeo mazuri tangu ligi hiyo kungoa nanga.

“Sisi ni ushindi tu kwa sababu tufanye mazoezi ya kutosha kwa ajili ya ligi hii ya kaunti na malengo yetu yanasalia pale pale kushinda na kupanda msimu ujao.”

Kilifi United inaketi nafasi ya 9 na imepoteza mechi mbili mfululizo kati nne ambazo wamecheza huku United Brothers wakishinda tatu na kupoteza moja pekee.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.