National News
Waliotuma Maombi ya Kujaza Nafasi ya Mwenyekiti wa Tume Hiyo ya Uchaguzi Kupigwa Msasa

Jopo la uteuzi wa Makamishna wapya wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, linatarajiwa kuanza zoezi la kuwapigwa msasa wakenya waliotuma maombi ya kujaza nafasi ya Mwenyekiti wa Tume hiyo ya uchaguzi.
Jopo hilo ambalo linaongozwa na Mwenyekiti wake Dkt Nelson Makanda liko na mda wa hadi tarehe 25 mwezi Aprili mwaka huu kuwa limepata Mwenyekiti wa IEBC pamoja na makamishna wapya.
Jopo hilo limewarai wakenya kuondoa hofu kwani baada ya zoezi hilo kukamilika, taifa litakuwa na makamishna wapya wa IEBC walio waadilifu na wenye kujitolea kufanikisha uchaguzi huru na haki.
Tayari majina ya wakenya 37, yameorodheshwa kati ya wale wanaomezea mate nafasi ya Mweyekiti wa IEBC ambao wanatarajiwa kuhojiwa ili kueleza wakenya malengo, dhamira na mikakati wataofanya kufanyika uchaguzi wa haki iwapo mtu atateuliwa kushinikilia nafasi hiyo.
Hata hivyo aliyekuwa msajili wa idara ya Mahakama nchini Ann Amadi, aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika mashariki Charles Nyachae, aliyekuwa Mwenyekiti wa bodi ya Kenya Power Joy Brenda Masinde pamoja na aliyekuwa Afisa mkuu mtendaji wa IEBC James Oswago ni kati ya wakenya wanaomezea mate nafasi hiyo.
National News
Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.
Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.
Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.
Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.
National News
Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.
Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.
Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.
Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.
Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.