News
Lazima Tufunge Tunisia Magoli ya Mapema, Kauli ya Kocha Odemba Kuelekea Mechi ya Starlets

Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee starlets Beldine Odemba ana amini kwamba uwepo wa mashabiki katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex Ijumaa hii itawapa msukumo timu hiyo wanapojianda kwa mechi ya kufuzu dimba la Afrika AWCON mwakani.
Akizungumza na wanahabari Odemba amesema anasubiri mchezaji wa mwisho kambini Jumatano hii.
“Tuko na karibu full house baada kuwasili kwa wachezaji zaidi ya kumi wa kulipwa,Tunasubiri mchezaji wa mwisho Jumatano hii.” Kocha anazidi kuelezea kwamba, “Lengo letu ni kushinda Tunisia hapa Nyumbani kabla ya mechi ya mkondo wa pili mjini Tunisia Feb 26. Kwa mujibu wa mwalimu huyo na kikosi mchanganyiko Yani chipukizi na wazoefu inampa msukumo kwamba tutaandikisha matokeo chanya, “Wachezaji chipukizi ndio Harambee starlets ya badaye kuwepo kwao kambini inanisaidia kuwa na upana wa kikosi na kujenga kikosi Cha usoni vile vile.Kwa upende wake kiungo wa Besikitas ya Uturuki Cynthia Shilwatso ni kwamba hawataki kujuta Tena baada ya kubanduliwa na Botswana mwaka Jana,” Lengo Letu ni kushinda nyumbani ndio tuenjoy mchezo ugenini, Ni lazima tufunge Tunisia magoli ya mapema kilichotupata mwaka Jana kisitupate tena.”
Kambi ya Harambee starlets imekamilika baada ya wachezaji wa kigeni wote kuwasili kwa pambano la kufuzu dimba la AWCON dhidi ya Tunisia Ijumaa hii ugani Ulinzi Sports Complex mjini Nairobi.
Mechi hiyo itapigwa majira ya saa tisa kiingilio ni shs. 100 mashabiki wa kawaida na shs. 500 watu mashuhuri (VIP).
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.