Connect with us

Sports

Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Published

on

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.

Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.

Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.

“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”

Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG

Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Ligi Limetuponyoka Asema Zico

Published

on

By

Mkufunzi wa Kilabu ya Gor Mahia Zedekiah Zico Otieno amekubali kwamba ligi imewaponyoka baada ya kutoka sare na kilabu ya Afc Leopards ugani raila odinga katika debi la Mashemeji jana jioni.

Kiungo matata Austine Odhiambo aliweka uongozini Kogalo kipindi cha kwanza dakika ya 30 kabila ya Brian wanyama kuisawazishia chui dakika ya 55 kipindi cha pili na kocha huyo anaamini taji limewatoka baada ya sare hiyo inayowacha nafasi ya tatu.

“Tulianza Vizuri lakini concetration lapse imetucost kipindi cha pili,lengo letu lilikua kupata ushindi hapa ili kuweka pressure kwa viongozi lakini sasa matokeo haya ni ishara tosha sasa itabidi tuangazie taji la Mozzartbet Cup.”

Kwa upande wake Mkufunzi wa Afc Leopards Fred Ambani amesema kwamba ameridhishwa na matokeo hayo akijigamba angali kupoteza mechi ya Debi akiwa mchezaji na sasa kama kocha wa Ingwe.

“Vijana walioanza mechi kwa mchecheto na uoga mwingi katika kipindi cha kwanza ila tulipoenda katia dressing room nikawambia watulie na ndiposa tukarejea mchezoni,ningali kupoteza debi kama mchezaji sikuwahi na sasa kama kocha pia bado sijapoteza.

Gor inasalia ya tatu na alama 55 huku Afc Leopards wakibaki ya sita na alama 47.

 

Continue Reading

Sports

Chelsea Kumtambulisha Delap

Published

on

By

Mshambulizi wa kilabu ya Ipswich Town na timu ya taifa Uingereza Liam Delap amekamilisha sehemu ya kwanza ya vipimo vya kimatibu anapokamilisha uhamisho wake katika kilabu ya Chelsea.

Kwa mujibu wa gwiji wa uhamisho barani ulaya Fabrizio Romano uhamisho huo ni wa pauni milioni 30 Delap akitarajiwa kumwaga wino mkataba wa miaka mitano stamford bridge.

Licha ya kumulikwa na vilabu kadha wa kadha ikiwepo Manchester United pamoja na Newcastle United Delap aliamua kwamba chaguo lake ni Chelsea msimu huu na atakua sajili wa kwanza kwa kocha Enzo Maresca.

The Blues wanatarajiwa kumtambulisha hii leo mchezaji huyo ambaye alipachika wavuni magoli 12 msimu huu na kutoa pasi mbili kwa wenzake kufunga msimu ambao umekamilika.

Vijana hao wanaaminika pia kusaka mshambulizi tajika msimu huu wakimulika mshambulizi Victor Gyokeres na Victor Osimhen inaamnika pia wanamfukuzia winga wa Bilbao Nico Williams.

Continue Reading

Trending