Connect with us

Entertainment

Ullulations! Sister Shanniez Afunga Ndoa Mtwapa

Drumrolls tafadhali! 🔔🎉 Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, hatimaye ametoka soko rasmi! Harusi ya kifahari ya kimyakimya, katikati ya jiji la Mtwapa, imegeuza Jumamosi kuwa sinema ya mapenzi ya Pwani. Wageni wachache lakini mashuhuri, vibes za Coco, na miondoko ya kimahaba—ni kama movie, lakini real life! 💍✨”

Published

on

Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, ameanza ukurasa mpya wa maisha kwa kufunga ndoa katika harusi ya kifahari lakini ya faragha, iliyofanyika Jumamosi Mei 31, katikati mwa jiji la Mtwapa, kaunti ya Kilifi.

Harusi hiyo, iliyosheheni uzuri wa Pwani na mvuto wa mazingira ya kimahaba, ilifanyika kwa mwaliko maalum kwa watu wa karibu tu.

Miongoni mwa waliohudhuria walikuwa ni jamaa wa familia, marafiki wa karibu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake kutoka Coco FM, waliokuja kushuhudia tukio hilo la kihistoria kwa ukaribu na heshima .

Watangazaji waliokuwa miongoni mwa wageni maalum ni Hamisi Kombe, Mamaa Madikodiko, Teddy Mwanamgambo, Hon Baba Yaga, Kassim Mbui, Binti Umazi, Sifa na Patrick. Uwepo wao katika sherehe hiyo ulidhihirisha mshikamano na urafiki wa kweli uliopo ndani ya familia ya redio hiyo.

Sister Shanniez, anayefahamika kwa sauti yake yenye mvuto na ucheshi wa kipekee hewani kupitia kipindi cha Coco Drive kinachorushwa kila Jumatatu hadi Ijumaa, ameendelea kuwa mfano wa mwanamke jasiri na mwenye msimamo maishani. Mbali na umahiri wake kitaaluma, harusi yake imefungua ukurasa mpya unaodhihirisha utu uzima na maamuzi ya busara katika maisha binafsi.

Kinachovutia zaidi ni kuwa maandalizi na taarifa kuhusu harusi hiyo yalisalia kuwa siri kubwa hadi siku yenyewe ya tukio. Ukimya huo wa kimakusudi ulitoa nafasi ya sherehe hiyo kufanyika kwa utulivu, upendo na heshima ya kipekee, bila minong’ono wala mkorogo wa hadhara.

Ingawa bado hakujatolewa taarifa rasmi kutoka kwake kuhusu tukio hilo, waliokuwepo wameelezea harusi hiyo kama yenye haiba, hisia, na ladha ya mapenzi ya kweli. Tangu kuwasili kwa bibi harusi hadi kwenye mankuli, kila hatua ilikuwa ya kipekee na ya kupendeza.

Ni wazi na dhahiri kuwa sura mpya ya maisha yake ya ndoa inaleta mvuto mpya katika safari yake ya maisha ya ndani na nje ya taaluma yake.

Hapa COCO FM tunasema kila lenye Kheri dada Shanniez na Mwenyezi Mungu akujalie mema kwenye ukurasa huu mpya wa maisha ya ndoa, Amen🙏🏼

Continue Reading
2 Comments

2 Comments

  1. Asha kassim

    May 31, 2025 at 9:02 pm

    Congratulations my fave Mungu akujalie kheri njema katika ndoa Yako as your biggest fan am proud of you dear we love you so much 💕💕💕💖💖🫂🫂🫶🫶🫶

  2. Aisha

    June 1, 2025 at 7:39 pm

    Pongezi dada sister shanniz.
    Karibu ndani yake tukaendeshe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Kutoka High Heels Hadi Kuimba Peku Stejini, Nyota Ndogo Afunguka

🎙️ “Sauti yangu ndiyo ya kusikiliza – si viatu vyangu.”
Katika dunia ya burudani ambako muonekano hupewa uzito mkubwa, Nyota Ndogo ameamua kuvunja ukimya. Kupitia video yake ya hivi karibuni, msanii huyo maarufu wa Pwani ameweka wazi sababu ya kuimba bila viatu stejini – na jibu lake linauma, linafundisha na linagusa moyo.

Published

on

Katika dunia ya burudani, wasanii hujikuta wakikumbana na mashabiki wa kila aina – wale wanaopenda sana kazi yao, na pia wale wanaouliza maswali au kukosoa kwa mitazamo yao. Hivi karibuni, muimbaji maarufu wa Pwani ya Kenya, Nyota Ndogo, aliamua kujibu swali ambalo limekuwa likizua mjadala mitandaoni: Kwa nini huimbia stejini bila viatu?

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Nyota Ndogo aliweka video akiwa kwenye onyesho la moja kwa moja, akiimba kwa hisia bila viatu. Video hiyo ilisababisha baadhi ya mashabiki kuuliza au hata kukosoa kuhusu muonekano wake huo, jambo lililomchochea kujibu kwa uwazi wa kipekee.

“Wapenzi wangu, nitakuwa najibu lile linalohitaji kujibiwa tu,” Nyota alianza kwa kusema.

Katika maelezo yake ya wazi na yenye kugusa moyo, Nyota Ndogo alisimulia kuwa alipokuwa msichana mdogo anayeanza muziki, alikuwa akivaa viatu vya michuchumio mirefu (high heels) ili aonekane mrefu. Wanaomfahamu vizuri wanajua kuwa urefu wake si mkubwa, na mara nyingi wale wanaomuona kwa mara ya kwanza hushangaa kumwona mfupi kuliko walivyodhani.

Kwa mujibu wake, viatu hivyo virefu viliathiri afya yake ya miguu kwa kiasi kikubwa:

“Miguu yangu ni mikubwa, nilirithi kwa mama. Lakini vile viatu vimeniletea madhara makubwa sana. Sasa ukubwani ndio naona madhara yake. Miguu huuma sana, wakati mwingine hata kutembea huwa shida, hasa mguu wa kushoto ambao huuma kama kidonda.”

Kwa sababu hiyo, amekuwa akilazimika kuvaa viatu vya chini au wakati mwingine kutumbuiza bila viatu kabisa, hasa maumivu yanapokuwa makali sana.

Lakini licha ya hayo, msanii huyo amesisitiza jambo moja muhimu:

“Mkiniona bila (viatu) niacheni tu na musikilize sauti yangu.”

Katika onyesho lake la hivi karibuni lililofanyika mgahawa mmoja Kilifi, ambalo lilikuwa acoustic performance, mashabiki waliweza kushuhudia nguvu ya sauti yake na hisia halisi bila kuangalia muonekano wa nje. Na kama alivyoeleza, onyesho hilo lilikuwa la aina yake:

“It was wow,” alisema Nyota.

Hadithi ya Nyota Ndogo si tu kuhusu muziki au uvaaji wa viatu – ni somo la maisha. Ni ukumbusho kuwa kila msanii ana hadithi ya kipekee nyuma ya pazia. Kabla ya kuhukumu kwa nje, ni vyema kuelewa ndani – na kama alivyoomba, tusikilize sauti yake, si kutazama miguu yake.

Je, umewahi kuhukumiwa kwa muonekano wako bila kueleweka undani wako? Hebu nambie kwenye comment section. 👇

Continue Reading

Entertainment

Baada ya Harusi ya Kai, Beka na Shanniez; Je, Inayofuata ni ya Kassim na Umazi?

Wapi unaweza kumpata mwenza wa maisha? Jibu linaweza kuwa popote—kanisani, mitandaoni, au kwenye safari za kawaida. Lakini kwa Kassim Mbui na Binti Umazi, jibu linaonekana kuwa wazi: sehemu ya kazi. Picha za wawili hao kutoka COCO FM ambazo zimenifikia huenda zikakushangaza kidogo ila ndio hivyo mapenzi hayatabiriki. Muda, kama kawaida, utatufunulia ukweli.

Published

on

Mara nyingi huulizwa, “Wapi mtu anaweza kumpata mwenza wa maisha?” Na mara nyingi, hakuna jibu moja sahihi. Wengine huwapata wake au waume zao kanisani, mitandaoni, au hata kwenye safari za kawaida na kwenye maeneo mengi mengine. Lakini ukweli ni kwamba sehemu ya kazi nayo si ya kubezwa. Hapo ndipo penzi linaweza kuchipua bila kutarajiwa.

Kwa watu kama Kassim Mbui na Binti Umazi, swali hilo linaweza kuwa na jibu moja: mahali pa kazi. Hawa wawili, ambao kwa sasa wanaendesha kipindi maarufu cha Janjaruka 254 ndani ya COCO FM, wamekuwa kivutio kikubwa si tu kwa uwezo wao wa kuwasiliana, bali pia kwa “chemistry” yao ya hewani na huenda of air pia.

Picha Zinasema Zaidi ya Maneno

Hali imezidi kuchanganya baada ya picha za wawili hao kunifikia. Katika picha hizo, Kassim anaonekana akiwa amepiga goti mbele ya Binti, huku Binti Umazi akiwa amevalia ‘gauni’ jekundu la kuvutia—rangi inayojulikana kwa kuwakilisha mapenzi. Katika picha hiyo, Binti anaonekana kustaajabu, kuishiwa na nguvu karibu kuanguka, kana kwamba amezidiwa na hisia.

Je, hilo lilikuwa ombi rasmi la uchumba? Au ni sehemu ya mradi wa kisanii ama kampeni ya matangazo? Bila shaka msomaji wangu unayefuatilia COCO FM kwa utapata jibu kwenye hili.

Chemistry ya Kazi au Zaidi ya Hapo?

Kassim na Binti wamekuwa wakituletea kipindi cha Janjaruka 254 kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja sasa, na kwa muda huo mfupi wameweza kuunganisha mashabiki na kuwapa burudani ya kipekee. Kipindi hicho hurushwa hewani kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa asubuhi ya saa nne hadi saa saba mchana, kupitia COCO FM, na kimejizolea mashabiki waaminifu wanaosubiri kusikia sauti zao kila siku.

Tusubiri Muda Uongee

Kama ilivyo kawaida yangu mimi huwa najipa kuamini sana MUDA. Kwenye swala hili, muda utakuwa mfunua ukweli. Kwa sasa, mashabiki wanaweza tu kuendelea kutazama, kusubiri, na kubashiri. Je, ni uchumba wa kweli au ni mbinu ya kisanaa? Bila shaka, ukweli utadhihirika muda si mrefu.

🔁 Je, una maoni au unadhani kweli mapenzi yamechipuka COCO FM? Niandikie kwenye comment!

Continue Reading

Trending