Connect with us

Entertainment

Millennials Bongo Tour: AY Kuwasha Moto Nairobi!

Published

on

Nguli wa Bongo Flava kutoka Tanzania, AY, ametua jijini Nairobi tayari kwa tamasha linalosubiriwa kwa hamu – Millennials Bongo Tour, litakalowasha moto Kilimani, Jumapili hii, tarehe 1 Juni.

AY ambaye hiyo jana ameachia vibao vipya SIMUONI na SI NDO MANAKE akishirisha na Harmonize na Darasa mtawalia, atakuwa sura ya tamasha hilo la kipekee la muziki wa Afrika Mashariki. Atasindikizwa na mwanamuziki mahiri kutoka Burundi, Kidum, pamoja na DJ Redbone wa Nairobi, anayejulikana kwa kuamsha burudani kwenye kila tamasha.

Tamasha hili linaahidi mchanganyiko wa kipekee wa vibao vya kumbukizi na ladha ya kisasa ya Bongo Flava. AY, anayejulikana kwa vibao vilivyotikisa chati kama Zigo, Touch Me Touch Me, na Microphone, amewaahidi mashabiki onyesho lisilosahaulika.

“Inahisi vizuri sana kurejea Nairobi. Nipo tayari kuwapa mashabiki wangu burudani ya kukumbukwa,” alisema AY mara baada ya kuwasili.

Kuongeza ladha ya kipekee, Kidum atapanda jukwaani na vibao vyake vya kuburudisha kama Mapenzi na Haturudi Nyuma, huku DJ Redbone akikoleza utamu kwa mchanganyiko mtamu wa Afrobeat, Bongo Flava, na nyimbo kali za ukanda huu.

Millennials Bongo Tour si tamasha la kawaida—ni sherehe ya kitamaduni inayotambua muziki wa Bongo kama daraja linalounganisha vizazi na mataifa. Toleo hili linatoa heshima kwa magwiji wa muziki wa Afrika Mashariki waliotengeneza historia na ambao wanaendelea kuwapa msukumo wasanii wapya hadi leo.

“Hili si tamasha tu—ni sherehe ya muziki wa Afrika Mashariki na fursa ya kipekee kwa mashabiki kuungana na magwiji waliounda sauti ya kizazi,” alisema mmoja wa waandaaji wa tamasha hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Ullulations! Sister Shanniez Afunga Ndoa Mtwapa

Drumrolls tafadhali! 🔔🎉 Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, hatimaye ametoka soko rasmi! Harusi ya kifahari ya kimyakimya, katikati ya jiji la Mtwapa, imegeuza Jumamosi kuwa sinema ya mapenzi ya Pwani. Wageni wachache lakini mashuhuri, vibes za Coco, na miondoko ya kimahaba—ni kama movie, lakini real life! 💍✨”

Published

on

Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, ameanza ukurasa mpya wa maisha kwa kufunga ndoa katika harusi ya kifahari lakini ya faragha, iliyofanyika Jumamosi Mei 31, katikati mwa jiji la Mtwapa, kaunti ya Kilifi.

Harusi hiyo, iliyosheheni uzuri wa Pwani na mvuto wa mazingira ya kimahaba, ilifanyika kwa mwaliko maalum kwa watu wa karibu tu.

Miongoni mwa waliohudhuria walikuwa ni jamaa wa familia, marafiki wa karibu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake kutoka Coco FM, waliokuja kushuhudia tukio hilo la kihistoria kwa ukaribu na heshima .

Watangazaji waliokuwa miongoni mwa wageni maalum ni Hamisi Kombe, Mamaa Madikodiko, Teddy Mwanamgambo, Hon Baba Yaga, Kassim Mbui, Binti Umazi, Sifa na Patrick. Uwepo wao katika sherehe hiyo ulidhihirisha mshikamano na urafiki wa kweli uliopo ndani ya familia ya redio hiyo.

Sister Shanniez, anayefahamika kwa sauti yake yenye mvuto na ucheshi wa kipekee hewani kupitia kipindi cha Coco Drive kinachorushwa kila Jumatatu hadi Ijumaa, ameendelea kuwa mfano wa mwanamke jasiri na mwenye msimamo maishani. Mbali na umahiri wake kitaaluma, harusi yake imefungua ukurasa mpya unaodhihirisha utu uzima na maamuzi ya busara katika maisha binafsi.

Kinachovutia zaidi ni kuwa maandalizi na taarifa kuhusu harusi hiyo yalisalia kuwa siri kubwa hadi siku yenyewe ya tukio. Ukimya huo wa kimakusudi ulitoa nafasi ya sherehe hiyo kufanyika kwa utulivu, upendo na heshima ya kipekee, bila minong’ono wala mkorogo wa hadhara.

Ingawa bado hakujatolewa taarifa rasmi kutoka kwake kuhusu tukio hilo, waliokuwepo wameelezea harusi hiyo kama yenye haiba, hisia, na ladha ya mapenzi ya kweli. Tangu kuwasili kwa bibi harusi hadi kwenye mankuli, kila hatua ilikuwa ya kipekee na ya kupendeza.

Ni wazi na dhahiri kuwa sura mpya ya maisha yake ya ndoa inaleta mvuto mpya katika safari yake ya maisha ya ndani na nje ya taaluma yake.

Hapa COCO FM tunasema kila lenye Kheri dada Shanniez na Mwenyezi Mungu akujalie mema kwenye ukurasa huu mpya wa maisha ya ndoa, Amen🙏🏼

Continue Reading

Entertainment

Sikutaka Pesa, Nilitaka Furaha – Bango Likaleta Vyote, Manu Bayaz

Published

on

Afisa wa polisi ambaye pia ni muimbaji wa muziki wa Bango, Emmanuel Yaa Baya anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii Manu Bayaz, amefichua kilichomsukuma kuingia kwenye muziki wa Bango.

Akihojiwa na Coco FM katika kipindi cha Coco Asubuhi, Bayaz alisema kwamba hajaanza muziki kwa ajili ya kutafuta pesa, bali alitaka kujifurahisha tu. Hata hivyo, nyimbo zake zilianza kuvutia watu wengi na kumpatia umaarufu mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa Bango wengine wakiitisha huduma zake kwenye sherehe zao.

“Hapo awali haikuwa kwa ajili ya pesa. Nilianza kwa kujifurahisha, lakini watu wakaanza kupenda nyimbo zangu,” alisema Bayaz.

Kutokana na mafanikio hayo, Bayaz aliamua kubadili mtazamo na kuanza kuwekeza zaidi kibiashara kwenye muziki huo.

Akiendelea kuelezea safari yake ya muziki, alitaja changamoto kubwa aliyokumbana nayo kuwa ni kudhibiti kundi la wanamuziki, akisisitiza ugumu wa kuwaunganisha watu wenye malezi na mitazamo tofauti katika kundi moja.

“Kwenye bendi, kila mtu ametoka mazingira tofauti, amekuzwa kivyake. Kuwaunganisha watu kama kumi si jambo rahisi, lakini tunajitahidi,” alisema.

Bayaz analikumbuka kwa furaha tukio la malipo yake ya kwanza katika muziki wa Bango.

“Malipo yangu ya kwanza ndiyo experience nayoikumbuka maisha yangu ya mziki. Nililipwa shilingi elfu hamsini za Kenya (KSh 50,000), Mtu wa kwanza kumtaarifu habari hii  ni babangu,” alisimulia.

Alieleza pia kuwa mapenzi yake ya muda mrefu kwa muziki wa Rhumba ndiyo yaliyomsukuma kuimba Bango, akieleza kuwa Bango ni aina ya Rhumba yenye ladha ya Pwani.

“Mimi napenda sana Rhumba. Nilivyoanza kuimba nikaona niende kwenye hiyo njia. Bango ni Rhumba tu, ila lina ladha ya Kipwani.”

Bayaz alianza kuimba akiwa na Sumilani Band na baadaye Ministers Band. Hata hivyo, aliachana na Sumilani baada ya kutofautiana kuhusu jina jipya alilopendekeza kwa bendi hiyo.

Bayaz pia alieleza kuwa alinunua vyombo vyake vya muziki kutoka China ili kuimarisha safari yake ya muziki, huku akiendelea kufanya kazi na bendi ya Sumilani kabla ya kuondoka.

Continue Reading

Trending