Connect with us

News

Wanaosajiliwa Kwenye Mpango wa Kazi “Majuu” Waonywa.

Published

on

Waziri wa Leba nchini Dakta Alfred Mutua amewaonya vijana waliopata nafasi za ajira ughaibuni dhidi ya kujihusisha na visa vya utovu wa nidhamu.

Akizungumza wakati wa zoezi la kusajili vijana kwenye mpango wa ajira za nje nchi maarufu Kazi “Majuu” katika kaunti ya Kwale, Waziri Mutua alitaja hatua hiyo kwamba huenda ikachangia kandarasi zao kufutiliwa mbali sawa na kukabiliwa kisheria.

Mutua alidokeza kwamba kuna baadhi ya vijana ambao tayari wamerejeshwa nchini kufuatia visa vya utovu wa nidhamu

“Unaskia unawashwa unataka kuandamana, unataka kuwa mwanaharakati, unataka kuchochea ingia ndege uje hapa wikendi moja uandamane kila mahali hiyo kitu ikutoke urejee kazini, kwa sababu ukienda kufanya huko maandamano unaharibia wakenya wengine, kuna watu waliandamana huko nchi tofauti tofauti, wakenya kumi na tano wengi wakasimamishwa, wakaregeshwa nyumbani, unaandamana kwa nchi nyengine wanauliza mbona mkenya anaandamana na mganda haandamani, mbona mtanzania haandamani”, alisema waziri Mutua.

Akizungumzia suala la utumizi wa dawa za kulevya, Waziri Mutua amewataka vijana hao kukomesha uraibu huo kwani  hakuna taifa linaloshabikia matumizi ya dawa za kulevya.

“Hapa utafanyia ukaguzi wa kiafya kama umekuwa ukivuta bangi, madawa ya kulevya utaanguka, hata ukikataa kupatikana hapa ukifika ng’ambo  utapatikana, kwa hivyo kama unataka kwenda ng’ambo achana na bangi bwana”,aliongeza waziri Mutua.

Zoezi hilo lililenga vijana 800 kaunti ya Kwale na 3,500 eneo la pwani kwa ujumla.

Taarifa ya Joseph Jira

 

 

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Published

on

By

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.

Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.

Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.

Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.

Continue Reading

News

Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Published

on

By

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.

Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.

Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.

Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.

Continue Reading

Trending