Sports
Wanahabari Wapokea Mafunzo ya Uandishi Siku Moja Kabla ya Kip Keino Classic

Waandishi wa habari kutoka Kenya wamepokea mafunzo ya kiufundi kuhusu namna ya kuripoti mashindano ya riadha ya hadhi ya kimataifa, yakiwemo ya toleo la sita la Absa Kip Keino Classic Continental Tour, yatakayofanyika katika Ulinzi Sports Complex.
Afisa Mawasiliano wa Riadha za Dunia, Antonio Carvalho, aliongoza warsha hiyo Alhamisi, Mei 29 na kuwapa wanahabari mbinu muhimu za kuripoti, hasa kwenye eneo la mahojiano ya haraka (flash interviews).
“Katika kunukuu wanariadha, zingatia maneno yanayoonesha utu wao, yanayoeleza ni nini kinachowafanya kuwa wa kipekee, na yanayobeba simulizi ya kipekee kuhusu mhusika,” alisema Carvalho.
Carvalho pia alisisitiza umuhimu wa waandishi kufanya utafiti wa awali kuhusu historia ya wanariadha kabla ya kuripoti mashindano ya kiwango cha juu kama Kip Keino Classic.
“Tovuti ya World Athletics (www.worldathletics.org) ni rasilimali muhimu. Ina taarifa nyingi kuanzia wasifu wa wanariadha, orodha za kuanza mashindano, hadi matokeo ya awali,” alieleza.
Aliongeza kuwa waandishi wa habari wanapaswa kufahamu maswali ya kuuliza ili kupata nukuu bora kutoka kwa wanariadha, na pia kuwa makini katika kufuatilia matokeo ya mashindano pamoja na hali ya mazingira wakati mashindano yanaendelea.
Katika warsha hiyo, Carvalho alisisitiza kuwa waandishi wa habari wanaoshughulika na flash quotes wanapaswa kuelewa kwa kina mienendo ya mchezo wa riadha ili kutoa taarifa bora na sahihi.
Pia, warsha hiyo ilitoa elimu muhimu kuhusu masuala ya Dhulma za Kijinsia (GBV) ambazo zimeathiri tasnia ya michezo, ikiwemo visa vinavyohusiana na Agnes Tirop wa Kenya na Rebecca Cheptegei wa Uganda.
Kikao hicho cha maingiliano kiliongozwa na Chris Mbaisi, Rais wa zamani wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Kenya (SJAK).
Rais wa sasa wa SJAK, James Waindi, aliwashukuru waandaaji wa warsha hiyo kwa juhudi zao na kuhimiza kuandaliwa kwa warsha zaidi zinazolenga kuwaunganisha wanahabari na wadau wa michezo.
Mashindano ya Kip Keino Classic ni moja ya mashindano ya siku moja ya kiwango cha juu duniani, yakiwa sehemu ya mashindano ya Continental Tour Gold Series ya Shirikisho la Riadha Duniani.
Toleo la mwaka huu linalotarajiwa kufanyika Jumamosi, Mei 31 kwenye Uwanja wa Ulinzi litawavutia wanariadha mashuhuri kutoka Afrika na mabara mengine, hivyo kuwapa wanariadha wa Kenya nafasi ya kushindana katika kiwango cha kimataifa.
Washiriki wa mashindano hayo watapigania zawadi ya fedha pamoja na pointi muhimu kwa viwango vya ubora vya dunia (world ranking points).
Sports
INZAGI Bado Yuko Saana Inter.

Uongozi wa klabu ya Inter Milan uko radhi kurefusa mkataba wa kocha Simone Inzaghi licha ya kufeli
kutwaa taji la klabu bingwa Uropa siku ya jumamosi.
Rais wa Inter Giuseppe Marotta, ameelezea Imani kwa uongozi wa Kocha Inzaghi, licha ya kibano cha
magoli 5-0 klabu hiyo ilipokea katika fainali ya klabu bingwa uropa dhidi ya Paris Saint-Germain
(PSG) na kupoteza fainali ya pili mtawalia, ya kwanza ikiwa msimu wa mwaka 2022/2023 mikononi
mwa Manchester City.
Mkataba wa Inzaghi unakamilika mwezi juni mwaka ujao ila Marotta, amesisitiza kuwa mazungumzo na
kocha huyo yataanza hivi karibuni, baada ya tetesi kuwa Inzaghi anajiondoa Inter na hatakuwepo
kuitayarisha kwa ajili ya msimu ujao.
“Kushindwa katika fainali hauna msukumo wowote, inzaghi ana mkataba wa mwaka mmoja Zaidi na
tuliamua kukutana naye juma hili” Alisema Marotta katika kikao na wanahabari baada ya fainali ya klabu
bingwa uropa huko Munich Ujerumani. “Mafanikio yote na makali ya klabu yanayoonekana ni kwa ajili
ya uwezo na utaalam wake,Tutafurahia iwapo yuko radhi kuendelea na kazi.”
Sports
Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.
Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.
Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.
“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”
Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG
Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.