Connect with us

Entertainment

Sikutaka Pesa, Nilitaka Furaha – Bango Likaleta Vyote, Manu Bayaz

Published

on

Afisa wa polisi ambaye pia ni muimbaji wa muziki wa Bango, Emmanuel Yaa Baya anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii Manu Bayaz, amefichua kilichomsukuma kuingia kwenye muziki wa Bango.

Akihojiwa na Coco FM katika kipindi cha Coco Asubuhi, Bayaz alisema kwamba hajaanza muziki kwa ajili ya kutafuta pesa, bali alitaka kujifurahisha tu. Hata hivyo, nyimbo zake zilianza kuvutia watu wengi na kumpatia umaarufu mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa Bango wengine wakiitisha huduma zake kwenye sherehe zao.

“Hapo awali haikuwa kwa ajili ya pesa. Nilianza kwa kujifurahisha, lakini watu wakaanza kupenda nyimbo zangu,” alisema Bayaz.

Kutokana na mafanikio hayo, Bayaz aliamua kubadili mtazamo na kuanza kuwekeza zaidi kibiashara kwenye muziki huo.

Akiendelea kuelezea safari yake ya muziki, alitaja changamoto kubwa aliyokumbana nayo kuwa ni kudhibiti kundi la wanamuziki, akisisitiza ugumu wa kuwaunganisha watu wenye malezi na mitazamo tofauti katika kundi moja.

“Kwenye bendi, kila mtu ametoka mazingira tofauti, amekuzwa kivyake. Kuwaunganisha watu kama kumi si jambo rahisi, lakini tunajitahidi,” alisema.

Bayaz analikumbuka kwa furaha tukio la malipo yake ya kwanza katika muziki wa Bango.

“Malipo yangu ya kwanza ndiyo experience nayoikumbuka maisha yangu ya mziki. Nililipwa shilingi elfu hamsini za Kenya (KSh 50,000), Mtu wa kwanza kumtaarifu habari hii  ni babangu,” alisimulia.

Alieleza pia kuwa mapenzi yake ya muda mrefu kwa muziki wa Rhumba ndiyo yaliyomsukuma kuimba Bango, akieleza kuwa Bango ni aina ya Rhumba yenye ladha ya Pwani.

“Mimi napenda sana Rhumba. Nilivyoanza kuimba nikaona niende kwenye hiyo njia. Bango ni Rhumba tu, ila lina ladha ya Kipwani.”

Bayaz alianza kuimba akiwa na Sumilani Band na baadaye Ministers Band. Hata hivyo, aliachana na Sumilani baada ya kutofautiana kuhusu jina jipya alilopendekeza kwa bendi hiyo.

Bayaz pia alieleza kuwa alinunua vyombo vyake vya muziki kutoka China ili kuimarisha safari yake ya muziki, huku akiendelea kufanya kazi na bendi ya Sumilani kabla ya kuondoka.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Millennials Bongo Tour: AY Kuwasha Moto Nairobi!

Published

on

Nguli wa Bongo Flava kutoka Tanzania, AY, ametua jijini Nairobi tayari kwa tamasha linalosubiriwa kwa hamu – Millennials Bongo Tour, litakalowasha moto Kilimani, Jumapili hii, tarehe 1 Juni.

AY ambaye hiyo jana ameachia vibao vipya SIMUONI na SI NDO MANAKE akishirisha na Harmonize na Darasa mtawalia, atakuwa sura ya tamasha hilo la kipekee la muziki wa Afrika Mashariki. Atasindikizwa na mwanamuziki mahiri kutoka Burundi, Kidum, pamoja na DJ Redbone wa Nairobi, anayejulikana kwa kuamsha burudani kwenye kila tamasha.

Tamasha hili linaahidi mchanganyiko wa kipekee wa vibao vya kumbukizi na ladha ya kisasa ya Bongo Flava. AY, anayejulikana kwa vibao vilivyotikisa chati kama Zigo, Touch Me Touch Me, na Microphone, amewaahidi mashabiki onyesho lisilosahaulika.

“Inahisi vizuri sana kurejea Nairobi. Nipo tayari kuwapa mashabiki wangu burudani ya kukumbukwa,” alisema AY mara baada ya kuwasili.

Kuongeza ladha ya kipekee, Kidum atapanda jukwaani na vibao vyake vya kuburudisha kama Mapenzi na Haturudi Nyuma, huku DJ Redbone akikoleza utamu kwa mchanganyiko mtamu wa Afrobeat, Bongo Flava, na nyimbo kali za ukanda huu.

Millennials Bongo Tour si tamasha la kawaida—ni sherehe ya kitamaduni inayotambua muziki wa Bongo kama daraja linalounganisha vizazi na mataifa. Toleo hili linatoa heshima kwa magwiji wa muziki wa Afrika Mashariki waliotengeneza historia na ambao wanaendelea kuwapa msukumo wasanii wapya hadi leo.

“Hili si tamasha tu—ni sherehe ya muziki wa Afrika Mashariki na fursa ya kipekee kwa mashabiki kuungana na magwiji waliounda sauti ya kizazi,” alisema mmoja wa waandaaji wa tamasha hilo.

Continue Reading

Entertainment

#JP2025: Mavazi ya Diamond Harusini kwa Jux Yaibua Gumzo

Published

on

Msanii maarufu wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ameibua mjadala mkali kwenye harusi ya kifahari ya Juma Jux na Priscilla Ojo iliyofanyika nchini Tanzania, baada ya kushindwa kufuata mavazi rasmi yaliyowekwa kwa hafla hiyo.

Alfajiri ya Alhamisi, Juma Jux alitoa ujumbe wa kukumbusha wageni wake wote kuhusu kuzingatia mavazi rasmi ya harusi hiyo: nyeusi na dhahabu.

Hata hivyo, wakati wa hafla ya mapokezi, Diamond alijitokeza akiwa amevalia suti nyeupe – akiwa ndiye mwanamume pekee aliyekiuka mwongozo wa mavazi uliotolewa.

Tukio jingine lililovutia hisia za wengi ni kutowasili kwake kwenye harusi hiyo pamoja na mpenzi wake, Zuchu.

Zuchu alifika peke yake katika hafla hiyo ya kifahari, huku Chibu Dangote (Diamond) akichelewa kufika. Hali hiyo ilizua maswali zaidi baada ya wawili hao kuketi kwenye meza tofauti, jambo lililowafanya mashabiki wao kuanza kuhusisha tukio hilo na tetesi za mgogoro kati yao.

Katika toleo la sita la harusi ya Juma Jux na Priscilla lililofanyika awali nchini Nigeria, Diamond alikuwa msimamizi mkuu (Best Man), lakini kwa hafla ya usiku iliyofanyika hivi karibuni, nafasi hiyo ilichukuliwa na msanii mwingine, Billnass.

Harusi ya Kipekee

Priscilla Ojo, binti wa muigizaji maarufu wa Nollywood Iyabo Ojo, alifunga ndoa na Juma Jux katika kile kinachotajwa kuwa mojawapo ya harusi zinazozungumziwa zaidi mwaka huu.

Sherehe hiyo, iliyopewa jina la utambulisho wa mtandaoni #JP2025, ilikuwa tamasha la kiutamaduni lililopambwa kwa shamrashamra, hisia nzito, mastaa wakuu, na mitindo ya kuvutia kutoka pande zote.

Safari ya wawili hao ilianza miezi kadhaa iliyopita, kupitia sherehe ya utambulisho iliyofanyika nchini Tanzania mwezi Februari, ambapo ndugu na marafiki wa karibu walikusanyika kushuhudia mwanzo wa safari yao ya ndoa.

Lakini Jux hakuishia hapo. Kabla ya Siku ya Wapendanao (Valentine’s Day), alifanya pendekezo jingine la ndoa, safari hii akimvisha pete ya almasi ya karati 5.2 — tukio lililowaacha wengi wakiwa na hisia kali mitandaoni, na kuthibitisha kuwa uhusiano wao umejengwa juu ya upendo wa kweli.

Baada ya hapo, wawili hao walifunga ndoa ya kiserikali (civil wedding) jijini Lagos nchini Nigeria.

Kisha, tarehe 17 Aprili 2025, Priscilla na Juma waliandaa harusi ya kitamaduni katika hoteli moja ya kifahari  iliyoko eneo la Oniru, Nigeria. Hafla hiyo ilikuwa muunganiko mzuri wa tamaduni za Nigeria na Tanzania, ambapo kila hatua ya sherehe hiyo ilikuwa na uzito wake wa kihistoria.

Jumamosi, tarehe 19 Aprili 2025, wapenzi Juma Jux na Priscilla Ojo waliidhinisha rasmi muungano wao kwa mara nyingine kupitia harusi ya kuvutia ya kanisani (white wedding) iliyofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Msanii nyota kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, aliteuliwa kuwa msimamizi wa harusi (Best Man), huku mwanamitindo na mshawishi wa mitandao ya kijamii, Diana Eneje, akiwa msimamizi wa bibi harusi (Best Maid).

Hafla hiyo ilihudhuriwa kwa wingi na mastaa mbalimbali kutoka tasnia ya filamu ya Nollywood na muziki, na kuwa tukio la kijamii lililoangaziwa sana na vyombo vya habari.

Miongoni mwa watangazaji wa hafla hiyo alikuwa Claudia Naisabwa kutoka Kenya. Wageni maarufu waliokuwepo pia walijumuisha Chioma Ikwokwu, Funke Akindele, rafiki wa karibu wa Priscilla Prince Enioluwa Adeoluwa kutoka Nigeria, pamoja na Raza Lee kutoka Tanzania, miongoni mwa wengine wengi waliopamba tukio hilo la kifahari.

Continue Reading

Trending