Connect with us

Entertainment

Self Love!!? Mulamwah Ajizawidi Gari la Kifahari Kusherehekea Siku ya Mazazi

Published

on

Mchekeshaji na mtangazaji wa redio, David Oyando, maarufu kama Mulamwah, ameadhimisha siku ya mazazi kwa kujizawidi gari la kifahari aina ya Mercedes Benz S550.

Msanii huyo anayependwa kwa ucheshi wake wa kipekee unaochambua maisha ya kila siku, alitumia mitandao ya kijamii kuonyesha hadharani zawadi hiyo ya kipekee aliyojipa kwa siku yake ya kuzaliwa.

“Na kwa zawadi yangu ya birthday… kutoka E-Class Benz hadi Mercedes Benz S-550 ya kisasa, injini ya 4.8L V8 Bi-Turbo,” aliandika Mulamwah huku akiwapa mashabiki wake taswira ya gari hilo jeusi kutoka Ujerumani.

Katika mazungumzo ya wazi, mtangazaji alifichua kuwa fedha alizotumia kununua gari hilo hapo awali zilikuwa zimekusudiwa kugharamia harusi yake na mchumba wake wa zamani, Ruth K.

Hata hivyo, baada ya mahusiano yao kuvunjika, aliamua kutumia akiba hiyo kutimiza ndoto yake ya muda mrefu.

“Nilitumia pesa nilizokuwa nimewekeza kwa ajili ya harusi—lakini mambo hayaendi kama vile unapanga—kulinunua,” alikiri, akitoa mwanga kuhusu mabadiliko ya kihemko na kifedha aliyopitia.

Kupitia chapisho lenye tafakari ya kina, Mulamwah alitumia tukio hilo kuwatia moyo mashabiki wake kwa ujumbe wa matumaini:

“Kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Kama kawaida, songa taratibu, songa kwa usahihi. Hata kama watu hawakuamini, wewe jiamini daima.”

Aidha, hakusita kuwashukuru mashabiki wake pamoja na washirika wa kibiashara waliomsaidia kufika alipo:

“Kwa mashabiki wangu na brandi zote, asanteni sana kwa kuniamini na kunisukuma kuendelea mbele,” aliongeza kwa shukrani.

Mulamwah amejiimarisha kama jina maarufu katika tasnia ya burudani nchini Kenya kupitia vichekesho vyake vinavyosambaa kwa kasi mitandaoni, ambavyo vimejikita kwenye maisha halisi ya Wakenya, pamoja na kazi yake ya utangazaji redioni.

Mchanganyiko wa ucheshi, uhalisia na msimamo wake thabiti umemjengea msingi wa mashabiki waaminifu, sambamba na nafasi ya kushirikiana na bidhaa mbalimbali zinazomhusudu kibiashara.

Licha ya kupitia vipindi vya misukosuko—ikiwemo kuvunjika kwa mahusiano na vuta nikuvute mitandaoni—Mulamwah amesalia imara katika utengenezaji wa maudhui na kukuza maisha yake binafsi.

Kuanzia uigizaji jukwaani, uendeshaji vipindi redioni hadi usimamizi wa chapa yake mitandaoni, ameendelea kukua kama msanii mwenye vipaji vingi na ushawishi mpana.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Ullulations! Sister Shanniez Afunga Ndoa Mtwapa

Drumrolls tafadhali! 🔔🎉 Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, hatimaye ametoka soko rasmi! Harusi ya kifahari ya kimyakimya, katikati ya jiji la Mtwapa, imegeuza Jumamosi kuwa sinema ya mapenzi ya Pwani. Wageni wachache lakini mashuhuri, vibes za Coco, na miondoko ya kimahaba—ni kama movie, lakini real life! 💍✨”

Published

on

Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, ameanza ukurasa mpya wa maisha kwa kufunga ndoa katika harusi ya kifahari lakini ya faragha, iliyofanyika Jumamosi Mei 31, katikati mwa jiji la Mtwapa, kaunti ya Kilifi.

Harusi hiyo, iliyosheheni uzuri wa Pwani na mvuto wa mazingira ya kimahaba, ilifanyika kwa mwaliko maalum kwa watu wa karibu tu.

Miongoni mwa waliohudhuria walikuwa ni jamaa wa familia, marafiki wa karibu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake kutoka Coco FM, waliokuja kushuhudia tukio hilo la kihistoria kwa ukaribu na heshima .

Watangazaji waliokuwa miongoni mwa wageni maalum ni Hamisi Kombe, Mamaa Madikodiko, Teddy Mwanamgambo, Hon Baba Yaga, Kassim Mbui, Binti Umazi, Sifa na Patrick. Uwepo wao katika sherehe hiyo ulidhihirisha mshikamano na urafiki wa kweli uliopo ndani ya familia ya redio hiyo.

Sister Shanniez, anayefahamika kwa sauti yake yenye mvuto na ucheshi wa kipekee hewani kupitia kipindi cha Coco Drive kinachorushwa kila Jumatatu hadi Ijumaa, ameendelea kuwa mfano wa mwanamke jasiri na mwenye msimamo maishani. Mbali na umahiri wake kitaaluma, harusi yake imefungua ukurasa mpya unaodhihirisha utu uzima na maamuzi ya busara katika maisha binafsi.

Kinachovutia zaidi ni kuwa maandalizi na taarifa kuhusu harusi hiyo yalisalia kuwa siri kubwa hadi siku yenyewe ya tukio. Ukimya huo wa kimakusudi ulitoa nafasi ya sherehe hiyo kufanyika kwa utulivu, upendo na heshima ya kipekee, bila minong’ono wala mkorogo wa hadhara.

Ingawa bado hakujatolewa taarifa rasmi kutoka kwake kuhusu tukio hilo, waliokuwepo wameelezea harusi hiyo kama yenye haiba, hisia, na ladha ya mapenzi ya kweli. Tangu kuwasili kwa bibi harusi hadi kwenye mankuli, kila hatua ilikuwa ya kipekee na ya kupendeza.

Ni wazi na dhahiri kuwa sura mpya ya maisha yake ya ndoa inaleta mvuto mpya katika safari yake ya maisha ya ndani na nje ya taaluma yake.

Hapa COCO FM tunasema kila lenye Kheri dada Shanniez na Mwenyezi Mungu akujalie mema kwenye ukurasa huu mpya wa maisha ya ndoa, Amen🙏🏼

Continue Reading

Entertainment

Millennials Bongo Tour: AY Kuwasha Moto Nairobi!

Published

on

Nguli wa Bongo Flava kutoka Tanzania, AY, ametua jijini Nairobi tayari kwa tamasha linalosubiriwa kwa hamu – Millennials Bongo Tour, litakalowasha moto Kilimani, Jumapili hii, tarehe 1 Juni.

AY ambaye hiyo jana ameachia vibao vipya SIMUONI na SI NDO MANAKE akishirisha na Harmonize na Darasa mtawalia, atakuwa sura ya tamasha hilo la kipekee la muziki wa Afrika Mashariki. Atasindikizwa na mwanamuziki mahiri kutoka Burundi, Kidum, pamoja na DJ Redbone wa Nairobi, anayejulikana kwa kuamsha burudani kwenye kila tamasha.

Tamasha hili linaahidi mchanganyiko wa kipekee wa vibao vya kumbukizi na ladha ya kisasa ya Bongo Flava. AY, anayejulikana kwa vibao vilivyotikisa chati kama Zigo, Touch Me Touch Me, na Microphone, amewaahidi mashabiki onyesho lisilosahaulika.

“Inahisi vizuri sana kurejea Nairobi. Nipo tayari kuwapa mashabiki wangu burudani ya kukumbukwa,” alisema AY mara baada ya kuwasili.

Kuongeza ladha ya kipekee, Kidum atapanda jukwaani na vibao vyake vya kuburudisha kama Mapenzi na Haturudi Nyuma, huku DJ Redbone akikoleza utamu kwa mchanganyiko mtamu wa Afrobeat, Bongo Flava, na nyimbo kali za ukanda huu.

Millennials Bongo Tour si tamasha la kawaida—ni sherehe ya kitamaduni inayotambua muziki wa Bongo kama daraja linalounganisha vizazi na mataifa. Toleo hili linatoa heshima kwa magwiji wa muziki wa Afrika Mashariki waliotengeneza historia na ambao wanaendelea kuwapa msukumo wasanii wapya hadi leo.

“Hili si tamasha tu—ni sherehe ya muziki wa Afrika Mashariki na fursa ya kipekee kwa mashabiki kuungana na magwiji waliounda sauti ya kizazi,” alisema mmoja wa waandaaji wa tamasha hilo.

Continue Reading

Trending