Connect with us

Sports

Kocha Wa Gor Zico Ataka Mashemeji Derby zichezwa Nje ya Nairobi

Published

on

Mkufunzi mshikilizi wa kilabu ya Gor Mahia Zedekiah Zico Otieno amesema kwamba ni wakati mwafaka kwa mechi nyingi za debi la Mashemeji kati mahasimu wa tangu jadi Gor na Afc Leopards zichezwe nje ya mji wa Nairobi.

Mwalimu huyo aliysema hayo kwenye kikao na wanahabari ambapo amesema kwamba itakua ni raha kuona mechi hiyo ikichezwa Kakamega,Mumias au hata Busia miaka zijazo.

Hayo yanajiri huku Zico akiweka wazi wanakwenda uwanjani Raila Odinga katika kaunti ya Homabay kusaka alama tatu muhimu siku ya jumatano dhidi ya Afc Leopards.

“Nadhani itakua ni mechi mgumu kwani debi haijakua rahisi ila tunakwenda kusaka alama tatu muhimu na kupunguza mwanya kati yetu na wapinzani wetu,ndaani ya Kogalo tunajua ushindi tu na najua mashabiki wanataka hilo,lengo letu ni ushindi tu siku ya Jumatatu.”

Tiketi za mchuano huo zinauzwa kwa shilingi 300 mshabiki wa kawaida huku mashabiki mashuhuri wakilipia shilingi 3000.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Mancity Inamnyemelea Kiungo Tijjani Reijnders

Published

on

By

Kilabu ya Manchseter City iko kwenye mazungumzo ya moja kwa moja na kiungo wa AC Milani Tijjani Reijnders kumleta ugani Etihad msimu ujao.

Mawakala wa mchezaji huyo wanataka kitita cha pauni milioni 60 kumwachilia mholanzi huyo ambaye amefunga magoli 19 katika mechi 104 ambazo amechezea Milan

Hata hivyo city wako tayari kutoa pauni milioni 55 kupata sahihi yake  na kumpa kandarasi nono mkataba wa miaka mitano ugani Etihad.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na Milan msimu jana akitokea AZ Alkamar ya Eredivise.

City wangali sokoni kupata mrithi wa kiungo mbunifu Kevin De Bruyne ambaye ameondoka kwenye kilabu hiyo baada ya mafanikio makubwa ikidaiwa pia wanamfukuzia kiungo wa Lyon Ryan Cherki raia wa Ufaransa.

Continue Reading

Sports

Arsenal Mbioni Kumpata Mshambulizi Sesko

Published

on

By

Kilabu ya Arsenal imeambiwa ni lazima itoe kitita cha pauni milioni 75 kunasa huduma za mshambulizi wa taifa la Slovenia na kilabu ya RB Leipzig Benjamin Sesko.

Inaaminika na The Gunners kupitia kwa Afisa mkuu mtendaji Andrea Berta wamekua na mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa mchezaji huyo na pia afisa wa Leipzig Marcel Schafer kuhusiana matakwa ya uhamisho huo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 alikua na magoli 21 msimu huu akichangia mengine sita katika michezo yote alizoshirikisha akiwa miongoni mwa wafungaji bora ligi ya Bundesliga nchini Ujerumani.

The Gunners wako sokoni kusaka mshambulizi atakayewapa taji msimu ujao huku ikidaiwa pia watafanya mazungumzo na mshambulizi wa Sporting Lisbon Victor Gyokeres ambaye alifunga zaidi ya magoli 40 msimu ambao umekamilika.

Continue Reading

Trending