News
Kesi dhidi ya Mackenzie na washukiwa wenzake 38 inaendelea Mahakamani

Kesi dhidi ya mhubiri tata Paul Mackenzie na washukiwa wenzake 38 kuhusu ukatili na ukiukaji wa haki za watoto inaendelea kusikizwa katika mahakama ya watoto ya Tononoka kaunti ya Mombasa mbele ya hakimu mkuu Nelly Chepchirchir, mashahidi 3 wakishuhudia.
Shahidi wa 47 ambaye ni mtaalamu wa afya ya akili ya watoto kutoka kituo cha watoto cha Malindi kaunti ya Kilifi, ameeleza mahakama namna mvulana mmoja miongoni mwa watoto 8 waliookolewa kutoka kwenye msitu wa Shakahola alivyokuwa na msongo wa mawazo kutokana yaliyokumba msituni humo.
Amesema mtoto huyo ambaye alisimulia mateso ya kimwili ambapo alikuwa akipigwa kwa kukiuka sheria za Mackenzie na kuishi kwa mateso, hali ambayo ilimsukuma kukimbilia kituo cha biashara kutafuta msaada.
Mtaalamu huyo pia amesema baada ya tathmini ya kitaalamu, alipendekeza mazingira salama ya malezi ya mtoto huyo kwasababu alikuwa na hofu ya kurudishwa Shakahola.
Amesema pia licha ya watoto ambao ni Manusura kurudi katika hali yao ya kawaida kuna haja ya kuendelea kuwapa usaidizi wa kisaikolojia hasa kwa kuwa walikuwa na wasiwasi kuhusu walipo jamaa zao.
News
Mchakato wa kuwapiga msasa Makamishena waanza Bungeni

Bunge la kitaifa limeanza kuwapiga msasa makamishena wateule 7 wa tume ya Uchaguzi na mipaka, IEBC katika majengo ya Bunge.
Shughuli hiyo imeanza leo Jumamosi Mei 31 2025, kufuatia maagizo ya Mahakama kuu kuondoa marufuku ya awali iliyositisha zoezi hilo.
Hata hivyo wiki iliyopita Jaji wa Mahakama hiyo Lawrence Mugambi aliliagiza bunge la kitaifa kutekeleza wajibu wake wa kikatiba wa kuwapiga msasa makamishena hao pamoja na mwenyekiti wake, ingawa ilizuia kuapishwa au kuchapishwa katika gazeti rasmi la serikali, majina ya Makamishna wapya wa tume hiyo, hadi mchakato huo utakapokamilika .
“ Bunge sasa linaweza kuendelea na zoezi la kuwapiga msasa makamishena hao 7 kufuatia uamuzi huu wa leo Mei 29 alisema Jaji mkuu Lawrence Mugambi ”
Uamuzi huu ulitolewa siku chache tu baada ya mahakama hiyo kusitisha zoezi hilo la kuwapiga msasa makamishena hao hadi pale kesi iliyokuwa imewasilishwa kotini na walalamishi wawili, Boniface Mwangi na Kelvin Roy Omondi, waliopinga uteuzi wa makamishena hao.
Makamishena hao wanaopigwa msasa ni Erastus Edung Ethekon mwenyekiti mteule,na makamishena Anne Nderitu, Moses Mukwana, Mary Karen Sorobit, Hassan Noor, Francis Odhiambo, na Fahima Abdalla,
Hii si mara ya kwanza zoezi la kuwatafuta makamishena wa IEBC kupatwa na pigo baada ya zoezi la kuwahoji watu waliopasa kuteuliwa katika nyadhifa hizo, pia kukumbwa vikwazo kufuatia kesi iliyowasilishwa mahakamani kupinga utaratibu uliodaiwa kuenda kinyume na ripoti ya NADCO ya kushirikisha maoni ya wananchi .
News
Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.
Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.
Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.
Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.