News
Bunge la kitaifa kuwahoji makamisha wa IEBC

Bunge la kitaifa, Jumamosi, Mei 31 linatarajiwa kuanza kuwapiga msasa mwenyekiti na makamishna wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC.
Ni shughuli iliyoratibiwa kufanyika katika majengo ya bunge na ambayo inajiri siku moja tu baada ya mahakama kuu nchini kuliagiza bunge la kitaifa kutimiza wajibu wake kikatiba la kuwapiga msasa makamishna hao kabla ya kuapishwa .
Mnamo Alhamisi Mei 29, katika mahakama kuu ya Milimani jijini Nairobi ,Jaji Lawrence Mugambi alitoa uamuzi wa kusitisha shughuli za kuapishwa au kuchapsiwa katika gazeti rasmi la serikali majina ya Makamishna hao kabla ya kupigwa msasa na bunge la taifa.
Rais William Samoei Ruto, mnamo Mei 9, 2025, aliwasilisha majina saba ya makamishna wateule 6, na mwenyekiti wao kwa bunge la taifa ili kuidhinishwa.
Saba hao ni Erastus Edung Ethekon kama mwenyekiti wa tume hiyo ya IEBC, makamishna Anne Nderitu, Moses Mukwana, Mary Karen Sorobit, Hassan Noor, Francis Odhiambo, na Fahima Abdalla kuunda tume hiyo ya IEBC.
News
Rais Ruto amewaongoza wakenya kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62

Rais William Ruto amewaongoza wakenya katika kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62 tangu taifa lijipatie uhuru.
Katika maadhimisho hayo ambayo yamefanyika katika uwanja wa Raila Odinga kaunti ya Homabay, Rais Ruto amesema taifa limepiga hatua kidemokrasia na maendeleo tangu lijipatie uhuru.
Kiongozi wa taifa ametoa changamoto kwa wakenya kuhakikisha wanaweka kipau mbele masuala ya kutekeleza mabadiliko yanayoleta ufanisi wa Taifa.
Wakenya washeherekea Madaraka, Homabay
Naye Naibu rais Prof Kithure Kindiki amemhakikishia Rais Ruto kuwa ataendelea kushirikiana naye katika kuunganisha taifa huku akimtaja Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kama kiongozi aliyechangia zaidi mshikamano wa taifa.
Kwa upande wake Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga amemtaka Rais Ruto kuhakikisha serikali inafidia familia za wakenya walipoteza wapendwa wao wakati wa Maandamano ya vijana wa Gen Z mwezi Juni mwaka jana.
Kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ni “uchumi wa sanawati na maswala ya bahari”, huku ikilenga kuangazia fursa za kiuchumi zinazotokana na raslimali ya maji.
News
Achani: Kaunti ya Kwale imepiga hatua katika uchumi samawati.

Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani amesema kaunti ya Kwale imepiga hatua katika kuimarisha sekta ya uvuvi na uchumi samawati.
Gavana Achani ameihimiza serikali ya kitaifa kuhakikisha inawekeza zaidi katika masuala ya uchumi samawati hasa kupitia bandari ya Shimoni, akisema itafungua ajira kwa vijana na kuboresha uchumi wa kaunti.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya sherehe za 62 za Madaraka katika eneo la Kinango, Gavana Achani amesema bandari ndogo 9 katika kaunti hiyo zimeboreshwa na vifaa vya kisasa ili kuchangia uhifadhi wa samaki.
Maadhimisho ya sherehe za Madaraka eneo la Kinango
Hata hivyo Viongozi waliohudhuria sherehe hizo katika gatuzi dogo la Kinango wakiongozwa na Mbunge wa Kinango Gonzi Rai, wamesisitiza haja ya viongozi pamoja na wananchi kumuunga mkono Rais Ruto katika kufanikisha ajenda ya maendeleo.
Kwa upande wake Kamishna wa kaunti hiyo Stephen Orinde amesisitiza umuhimu wa wakenya kuunga mkono miradi ya serikali hasa uchumi samawati na masuala ya bahari ili kupiga hatua kimaendeleo.