Connect with us

News

Mahakama kuu Imeagiza Kutoapishwa kwa Makamishna wa IEBC

Published

on

Mahakama kuu imeagiza kutoapishwa na kuchapishwa katika gazeti rasmi la serikali majina ya Makamishna wapya wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC.

Jaji wa Mahakama hiyo Lawrence Mugambi, ameliagiza bunge la kitaifa kuwapiga msasa Makamishna hao pamoja na Mwenyekiti mpya wa IEBC waliyopendekezwa na jopo la uteuzi la IEBC baada ya zoezi la kuwahoji kukamilika.

Jaji Mugambi amesema masuala yaliyoibuliwa katika kesi hiyo yana uzito na pia yanahusisha wananchi hivyo basi Mahakama haiwezi kuyapuuza kwani yanahitaji ufafanuzi wa kisheria na Katiba.

Jaji Mugambi hata hivyo amewasilisha faili ya kesi hiyo kwa Jaji Mkuu nchini Martha Koome ili kuteua jopo la majaji watatu watakaosikiliza na kuamuzi kesi hiyo.

Kesi hiyo iliwasilishwa Mahakamani na Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu Boniface Mwangi na Kelvin Roy Omondi, wakilishtaki bunge la kitaifa, Mkuu wa utumishi wa umma pamoja na watu wengine wanane.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mchakato wa kuwapiga msasa Makamishena waanza Bungeni

Published

on

Bunge la kitaifa limeanza kuwapiga msasa makamishena  wateule 7 wa tume ya  Uchaguzi na mipaka, IEBC katika majengo ya Bunge.

Shughuli hiyo imeanza leo Jumamosi Mei 31 2025, kufuatia maagizo ya Mahakama kuu kuondoa marufuku ya awali iliyositisha zoezi hilo.

Hata hivyo wiki iliyopita Jaji wa Mahakama hiyo Lawrence Mugambi aliliagiza bunge la kitaifa kutekeleza wajibu wake wa kikatiba wa kuwapiga msasa makamishena hao pamoja na mwenyekiti wake, ingawa ilizuia kuapishwa au kuchapishwa katika gazeti rasmi la serikali, majina ya Makamishna  wapya wa tume hiyo, hadi mchakato huo utakapokamilika .


Bunge sasa linaweza  kuendelea na zoezi la kuwapiga msasa makamishena hao 7 kufuatia uamuzi huu wa leo Mei 29 alisema Jaji mkuu  Lawrence Mugambi

Uamuzi huu ulitolewa siku chache tu baada ya mahakama hiyo kusitisha zoezi hilo la kuwapiga msasa  makamishena hao hadi pale kesi iliyokuwa imewasilishwa kotini na walalamishi wawili, Boniface Mwangi na Kelvin Roy Omondi, waliopinga uteuzi wa makamishena hao.

Makamishena hao wanaopigwa msasa ni Erastus Edung Ethekon mwenyekiti mteule,na makamishena Anne Nderitu, Moses Mukwana, Mary Karen Sorobit, Hassan Noor, Francis Odhiambo, na Fahima Abdalla,

Hii si mara ya kwanza zoezi la kuwatafuta makamishena wa IEBC kupatwa na pigo baada ya zoezi la kuwahoji watu waliopasa kuteuliwa katika nyadhifa hizo, pia kukumbwa vikwazo kufuatia kesi iliyowasilishwa mahakamani kupinga utaratibu uliodaiwa kuenda kinyume na ripoti ya NADCO ya kushirikisha maoni ya wananchi .

Continue Reading

News

Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Published

on

By

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.

Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.

Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.

Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.

Continue Reading

Trending