Connect with us

News

Gavana Godhana Awataka Wakulima na Wafugaji Kudumisha Amani

Published

on

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhado Godhana amezitaka jamii za wakulima na wafugaji kuzika tofauti zao na kuishi kwa Amani na umoja ili kufungua fursa zaidi za waekezaji kuingia katika kaunti hiyo.

Godhana amesema mvutano uliopo baina ya jamii hizo mbili huenda ukaibua suala la ukosefu wa usalama huku akisema kuwa hakuna mwekezaji atakayekubali kuwekeza mahali palipo na mvutano au ukosefu wa uwiano.

Aidha ameongeza kuwa suala la ardhi ambalo limekuwa donda sugu katika kaunti hiyo wanalifahamu na kama viongozi wanatafuta mbinu za kuhakikisha mzozo huo unadhibitiwa kikamilifu.

“Hii malumbano yenu mko nayo ya ardhi tunajua mna tatizo la ardhi iwe ya malisho au ukulima, tunataka tuwahimize kwamba hayo mambo mtafute njia za kudhibiti yasipite kiwango kwa sababu hakuna mtalii atakuja akijua kuna mizozo”, alisema Godhana

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Published

on

By

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.

Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.

Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.

Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.

Continue Reading

News

Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Published

on

By

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.

Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.

Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.

Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.

Continue Reading

Trending