News
SHILINGI MILIONI 600 ZATENGEWA MRADI WA BANDARI NDOGO ENEO LA VUMA

Serikali ya kitaifa kupitia wizara ya uchumi na raslimali za baharini na maziwa imetenga kima cha shilingi milioni 600 ili kuanzisha mradi wa bandari ndogo katika eneo la Vuma, Takaungu, Mnarani, Kilifi Kaskazini kaunti ya Kilifi.
Akizungumza na coco fm, mwenyekiti wa wahudumu wa maboti Kilifi mjini kaunti ya Kilifi, Shallo Issa amebainisha kuwa walituma maombi kwa serikali kuu wakiomba bandari ndogo inayotumika na wawekezaji wa kibinafsi kule Mnarani iwekewe mikakati ya kumilikiwa na mamlaka ya bandari nchini pindi uwekezaji huo utakapokwisha.
Shallo akisema kuwa bandari hiyo inaweza kutumika kwa namna nyingine ili kuimarisha wavuvi wa Mnarani na Kilifi Lakiji pia njia mojawapo ya kuimarisha uchumi wa baharini eneo hili.
Aidha Shallo amesema kuwa bandari hiyo itasaidia sana katika kubuni nafasi za ajira kwa vijana kwenye sekta ya uvuvi.
News
Kilabu Ya Liverpool Yamnasa Frimpong

Beki wa kilabu ya Bayern Leverkusen Jeremie Frimpong ni rasmi amejiunga na mabingwa wa ligi kuu Uingereza Liverpool.
Beki huyo mholanzi amejiunga na The Reds kwa pauni milioni 29.5 na amemwaga wino mkataba wa miaka 5 na kilabu hio kuchukua nafasi ya Alexander Trent Arnaold ambaye ni rasmi amejiunga na kilabu ya Real Madrid.
Mholanzi huyo anakua mchezaji wa tano kuvalia jezi ya kilabu hio wengine akiwa ni pamoja na Cody Gakpo,Virgil Van Dijik,Ryan Gravenberch.
Nyota huyo ambaye pia amekuwa akiwindwa na Manchester United na miamba wa Uhispania Rea Madrid amesema kwamba alichagua kilabu hiyo kwani ndio inaendana na mipango yake ya mbeleni kama mchezaji akiahidi kushinda mataji na miamba hao wa Uingereza.
News
Shughuli za Masomo Zatatizwa katika Shule ya Msingi ya Arabuko Sokoke

Shughuli za masomo katika shule ya msingi ya Arabuko Sokoke eneo la Kakuyuni kaunti ya Kilifi zilitatizika mapema siku ya Ijumaa baada ya Wazazi kuandamana wakilalamikia usimamizi mbaya wa shule hiyo.
Wakaazi hao wamemtaka Mwalimu kuu wa shule hiyo kupewa uhamisho kwani ameonyesha wazi kushindwa kusimamia shughuli za masomo katika shule hiyo.
Wakiongozwa na Joyce Mbuche, Wazazi hao wamesema Mwalimu mkuu wa shule hiyo amekosa kuwa wazi kwa wazazi kuhusu suala la matumizi ya Fedha ya shule hiyo pamoja na kutokuwa muadilifu kazini.
Wazazi hao hata hivyo wamesema Mwalimu mkuu huyo amekuwa hawalipi mishahara walimu ambao wanasimamiwa na wazazi katika shule hiyo huku baadhi ya wanafunzi wakikosa kusajiliwa katika mfumo wa KEMIS.