News
Kenya Yatoa ufadhili wa Asilimia 20 kwa WHO

Kenya imejitolea kuongeza ufadhili wake kwa Shirika la Afya duniani WHO kwa asilimia 20 katika kipindi cha miaka 4 ijayo.
Waziri wa Afya nchini Aden Duale ameyasema hayo wakati wa Kongamano la 78 la Afya duniani linaloendelea mjini Geneva nchini Uswizi, ambapo amesisitiza haja ya serikali ya Kenya kujitolea katika kuboresha sekta ya afya ulimwenguni.
Waziri Duale amesisitiza umuhimu wa ufadhili endelevu kwa Shirika la Afya duniani WHO, akisema licha ya bajeti kurekebishwa na kuweka ufadhili huo mdogo pia utasaidia sekta ya afya.
Waziri Duale ameangazia dhamira ya serikali ya Kenya ya kuhakikisha wananchi wananufaika na huduma za afya kwa wote UHC, kuimarishwa kwa ufadhili wa afya na kuendeleza miundombinu ya afya ya kidijitali ili kuendesha sera inayotumia data.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus amepongeza kujitolea kwa mataifa wanachama katika kufadhili WHO, akisema ahadi zilizotolewa na mataifa hayo zitachangia kuimarika kwa sekta ya afya duniani.
News
Wataalam wa Uchumi wa Bahari washinikiza Viongozi kuwawezesha Wananchi.

Wataalamu wa sekta ya uchumi wa samawati na maswala ya bahari hapa nchini wamesistiza haja ya serikali kuweka mazingira bora ya kubuni nafasi zaidi ya ajira ili kuinua uchumi wa bahari.
Mtaalam wa sekta hiyo Stanley Chai alisema uboreshaji wa mazingira ya sekta hiyo utachangia waekezaji zaidi kuekeza hapa nchini.
Chai alidokeza kuwa bahari hindi inafursa kubwa ya kuinua uchumi wa nchi kutokana na raslimali zinazopatikana bahari hindi.
“Nilazima tuweke mazingira yakuvutia meli nyingi, hii bahari yetu kuna mda ukiangalia kuna meli hamsini zinapita, tumekuwa tukishauri ulimwengu na kinachofanyika ni kuweka mazingira ya kuekeza upatikanaji wa samaki wa kiviwanda nchini, kama saa hii Kenya mtu akitaka liseni ya kwenda kuvua samaki kama hivi tuna tunamtoza dola elfu hamusini kwa mwaka”,alisema Chai.
Kuhusu swala la kudhibiti uingizaji wa bidhaa za samaki kutoka taifa la uchina katika soko la hapa nchini, mtaalam huyo alisema uhaba wa samaki hapa nchini umechangia uendelezaji wa biashara baina ya nchi hizo mbili ili kutosheleza lishe miongoni mwa jamii nchini.
“Japan ndio walaji wakubwa wa samaki ulimwenguni, samaki wakiletwa hapa ndio wavuvi wetu watafaidi, wakati samaki wanapelekwa nje ujue samaki wetu wenye thamani ndio wanaenda nje na sisi tunakula tilapia ambao wameletwa kutoka huko, kama samaki wangekuwa wanatutosheleza hapa hakungekuwa na soko la wachina, lakini kwa sababu hawatutoshelezi ndio maana watu wamepata mwanya wa kuleta”, aliongeza mtaalam huyo.
Mtaalam wa maswala ya uchumi wa bahari Stanley Chai akipokezwa zawadi na Coco fm.
Wakati huo huo alishinikiza viongozi hapa nchini kutafuta ufahamu zaidi kuhusu maswala ya uchumi wa bahari sawa na kuweka mikakati ya kubuni nafasi za ajira ili kuwezesha wananchi kimaendeleo.
“Haieleweki kama wewe ni mbunge unasema utaendeleza eneo bunge lako na CDF ya shilingi milioni 170, hakuna maendeleo utaleta, kwa hivyo vingozi tunafaa kufikiria tofauti, tuje na njia mbadala ya kwamba tutabuni ajira na tutaleta utajiri watu wajitegemee na njia moja rahisi ni hii, sisi tunashukuru sana rais alisikiza akaelewa na kwa mara ya kwanza akaunda wizara nzima ya uchumi samawati, ninini tena unataka? Unataka kumlaumu rais tena?”, aliuliza Chai.
Tamko la mtaalam huyo linajiri wakati Kenya ikiadhimisha sherehe za miaka 62 za siku ya madaraka, ambazo ziliongozwa na rais William Ruto katika kaunti ya Homabay huku kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ikiwa ni “Uchumi sanawati na maswala ya bahari”.
Taarifa na Joseph Jira
News
Rais Ruto amewaongoza wakenya kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62

Rais William Ruto amewaongoza wakenya katika kuadhimisha sherehe za Madaraka za 62 tangu taifa lijipatie uhuru.
Katika maadhimisho hayo ambayo yamefanyika katika uwanja wa Raila Odinga kaunti ya Homabay, Rais Ruto amesema taifa limepiga hatua kidemokrasia na maendeleo tangu lijipatie uhuru.
Kiongozi wa taifa ametoa changamoto kwa wakenya kuhakikisha wanaweka kipau mbele masuala ya kutekeleza mabadiliko yanayoleta ufanisi wa Taifa.
Wakenya washeherekea Madaraka, Homabay
Naye Naibu rais Prof Kithure Kindiki amemhakikishia Rais Ruto kuwa ataendelea kushirikiana naye katika kuunganisha taifa huku akimtaja Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kama kiongozi aliyechangia zaidi mshikamano wa taifa.
Kwa upande wake Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga amemtaka Rais Ruto kuhakikisha serikali inafidia familia za wakenya walipoteza wapendwa wao wakati wa Maandamano ya vijana wa Gen Z mwezi Juni mwaka jana.
Kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ni “uchumi wa sanawati na maswala ya bahari”, huku ikilenga kuangazia fursa za kiuchumi zinazotokana na raslimali ya maji.